Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO (K.n.y. MHE. STEPHEN J. MASELE) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itahakikisha vijiji vilivyo ndani ya kilomita tano kutoka bomba kuu la maji ya Mradi wa KASHWASA vinapatiwa maji vikiwemo vijiji vya Kolandonto, Ibadakuli na Kuzumbi?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini napenda kujua, kwa sababu maendeleo hayana utengemano yaani ni maendeleo kwa jumla bila kujali mipaka na itikadi ya kisiasa, miradi hii inakwenda kwa wananchi wote. Baada ya kutandaza mabomba mpaka maeneo ya Kishapu, je, mradi huu mnaweza kuupeleka mbele zaidi hadi vijiji vya Mwamashindike mpaka Lalago wakapata maji? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Wilaya ya Maswa nayo inasubiri Mradi wa Maji ya Ziwa Viktoria ambao utakuja katika phase two ya ule mradi wa maji kutoka Lamadi. Je, Wizara ina mpango gani kuwasaidia wananchi ambao hawana maji hivi sasa kwa kutumia mabwawa yaliyopo katika Wilaya ya Maswa kwa mfano Bwawa la Sola, Nyangugwana, Mwantonja kwa kuyasafisha na kuyafanya kuwa chanzo cha maji katika Wilaya ya Maswa ili wananchi waweze kupata maji kwa sasa wakati wanasubiri mradi wa Ziwa Viktoria ukamilike? Ahsante sana.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stephen Nyongo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimshukuru Mheshimiwa Mbunge, mwenyewe amesema kwamba miradi hii haina mipaka ndiyo maana tunatoa maji kutoka Ziwa Viktoria Mwanza yanakuja Shinyanga yatafika mpaka Tabora yatakuja mpaka Singida. Kwa hali hiyo, vijiji alivyovitaja kama ile pressure itaweza kufika tutaweza kuvifikia.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, amezungumzia kuhusu Wilaya ya Maswa ambayo itafikiwa na awamu ya pili ya mradi wa maji kutoka Ziwa Viktoria lakini kwa hatua za dharura, tufanye nini kwenye mabwawa? Tumetenga fedha kwenye halmashauri zote, zihakikishe kwamba zinapeleka fedha hizo kwenye miradi ya kipaumbele ambayo itahakikisha kwamba wananchi wanapata maji kwa uharaka.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO (K.n.y. MHE. STEPHEN J. MASELE) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itahakikisha vijiji vilivyo ndani ya kilomita tano kutoka bomba kuu la maji ya Mradi wa KASHWASA vinapatiwa maji vikiwemo vijiji vya Kolandonto, Ibadakuli na Kuzumbi?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mamlaka za Maji Mijini ndiyo vyombo vyenye dhamana ya kuhakikisha upatikanaji wa maji mijini na kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Nanyamba imeanzishwa kisheria mwaka 2015, je, Serikali ina mpango gani wa kuharakisha uundwaji wa Bodi ya Mamlaka ya Maji ya Mji wa Nanyamba ili kuhakikisha maji katika Mji wa Nanyamba yapatikana kwa kirahisi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Chikota, Mbunge wa Nanyamba kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, suala analolizungumzia Mheshimiwa Chikota ni jambo la msingi na hizi Bodi za Mamlaka za Maji za Halmashauri ziko chini ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI, mwanzo Ofisi hii ilikuwa chini ya Waziri Mkuu. Tulichokifanya ni nini? Mwezi mmoja uliopita tulikuwa na mkutano mkubwa wa wadau mbalimbali kuhusiana na suala la uundwaji wa Bodi za Mamlaka za Maji ili ifike wakati halmashauri ziweze kuhudumiwa vizuri. Sasa Ofisi yetu inafanya uratibu kutokana na mabadiliko ya Serikali yetu kwamba sasa iko chini ya Ofisi ya Rais na tunafanya mchakato mpana, siyo kwa Bodi ya Mamlaka ya Maji ya Nanyamba peke yake isipokuwa ni Bodi za Mamlaka za Maji za halmashauri mbalimbali ambapo nyingi sana hatujaziunda, si muda mrefu sana zoezi hili litakamilika na Nanyamba Mamlaka yenu itakuwa rasmi.

Name

Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO (K.n.y. MHE. STEPHEN J. MASELE) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itahakikisha vijiji vilivyo ndani ya kilomita tano kutoka bomba kuu la maji ya Mradi wa KASHWASA vinapatiwa maji vikiwemo vijiji vya Kolandonto, Ibadakuli na Kuzumbi?

Supplementary Question 3

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kuiuliza Serikali, hii miradi yote ya mwaka 2015/2016 ambayo tunaendelea nayo ambayo fedha zake hazijaenda kwa mfano Babati Vijijini na zimebaki siku kumi, je, kipindi hiki cha bajeti cha 2017 mbali na hii pesa iliyotengwa, hii ya nyuma yote tutapatiwa ili ile miradi ambayo haijatekelezwa itekelezwe?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Jitu Soni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, nianze kushukuru Ofisi ya Wizara ya Fedha wamefanya kazi nzuri, wamekusanya fedha na wanatupatia na hata wiki iliyopita walitupatia zaidi ya shilingi bilioni 15. Katika Bunge hili nimekuwa nikiagiza kwamba Waheshimiwa Wabunge wawaambie Wakurugenzi wa Halmashauri yeyote aliye na hati mkononi ailete ili tuweze kulipa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Jitu Soni kama kuna certificate, sijui kwa siku hizi zilizobaki itawahi kwa sababu tarehe 26 ni mwisho, inabidi tuwe tumeshamaliza kulipa lakini hata hivyo wala usiwe na wasiwasi hata ukichelewa kama certificate ipo naomba ije ili tuweze kulipa. Nikuhakikishie kwamba miradi yote ambayo ilikuwa haijakamilika Mheshimiwa Jitu Soni tutahakikisha kwamba tunaikamilisha.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO (K.n.y. MHE. STEPHEN J. MASELE) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itahakikisha vijiji vilivyo ndani ya kilomita tano kutoka bomba kuu la maji ya Mradi wa KASHWASA vinapatiwa maji vikiwemo vijiji vya Kolandonto, Ibadakuli na Kuzumbi?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mpanda Vijijini lina miradi miwili ya umwagiliaji. Mradi wa kwanza ni ule wa Karema ambao Serikali imetoa fedha nyingi kwa ajili ya matengenezo lakini bado haujakamilika na mradi wa pili ni ule wa Mwamapuli ambao unamwagilia vijiji vya Kabage. Miradi yote hiyo haijaweza kukamilika kwa wakati. Je, ni lini Serikali inaweza kukamilisha miradi hiyo ili iweze kuwasaidia wananchi ili kutopata hasara kwa fedha za Serikali ambazo zimeshatumika?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kakoso, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, amezungumzia kuhusu miradi ya umwagiliaji, ni kweli kabisa kwamba kumekuwa na miradi ya umwagiliaji katika eneo hilo lakini baadhi ya miradi hiyo ilipata matatizo kidogo na tumeagiza kuifanyia kazi. Kwa sababu ya masuala yaliyotokea siwezi kumjibu sasa hivi, ripoti ikija naweza kumfahamisha. Lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba yale matatizo yote yaliyojitokeza yanatatuliwa na tuhakikishe kwamba tunakamilisha ile miradi ili wananchi waweze kutumia miradi ile ya uwagiliaji wazalishe zaidi tuweze kupata chakula.