Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Mtwara Mjini kwenda Msimbati ambako kuna mitambo ya visima vya gesi?

Supplementary Question 1

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante; pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kutokana na umuhimu wa barabara ya ulinzi inayozunguka maeneo ya mipaka yet una nchi Jirani ya Msumbiji, je, lini Serikali itaanza kutengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha lami ili kurahisisha hata vyombo vyetu vya ulinzi vinapofanya doria vifike kwa wakati?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kutokana na uwepo wa miundombinu muhimu ya umeme na visima vya gesi, Vijiji vya Msimbati na Madimba. Je, Serikali haioni sasa ni wakati sahihi wa kuboresha miundombinu ya barabara hiyo kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shamsia Azizi Mtamba, Mbunge wa Mtwara Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara ya ulinzi aliyoitaja ni barabara muhimu sana na ina urefu zaidi ya kilometa 350 na hadi sasa barabara hii baada ya kwamba ilitumika kipindi kile haitumiki na sasa hivi inafunguliwa upya na tayari na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imeshafungua karibu kilometa 250 na inaendelea kuifungua mpaka itakapokamilika. Na baada ya kukamilika kuifungua ndipo tutakapoanza utaratibu wa kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, barabara hii aliyoisema ni lini tutaanza, tayari tumeshaanza ndio maana tumeshafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kilichobaki sasa ni kutafuta tu fedha na tutakapopata basi tutaanza kujenga kwa kiwango cha lami ili kufikia hayo maeneo muhimu ya Mnazi Bay, ahsante.