Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro kati ya Hifadhi ya Lwafi iliyopo Nkasi Kusini na wananchi wa Vijiji vya Mlambo, King’ombe, Tundu na Kata ya Wampembe?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Hali ya madhara yanayotokana na wanyamapori yamekuwa ni makubwa sana. Leo hii kwenye Vijiji vya Ngumbu, Kibutuka, Kiangala na Ngatapa, wananchi wameshahama wamerudi majumbani kwao kutoka mashambani, baada ya tembo kumaliza mazao yote. Sasa naomba Serikali ituambie, je, ina mkakati gani wa kuhakikisha usumbufu huu wa wanyamapori unapungua hasa kwenye hivi vijiji vichache nilivyovitaja? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuwapa pole wananchi wa Liwale, lakini pia niendelee kutoa pole kwa wananchi wengine wote wanaozunguka maeneo ya hifadhi, zikiwemo Hifadhi ambazo nimezitembelea jana za Mwanga na Same.

Mheshimiwa Spika, changamoto hii inasababishwa na wananchi kusogelea maeneo ya hifadhi, hasa maeneo yenye ushoroba, njia za wanyama pori hususani tembo, wanatembea kwa speed ndefu na wanatembea katika maeneo marefu na shoroba hizi zimezibwa na wananchi ambao wanafanya shughuli za kilimo lakini wengine wamejenga kwenye maeneo ambayo ni mapito ya wanyama.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshaweka mkakati wa kufanya mafunzo kwa wananchi ya namna ya kudhibiti hawa tembo, lakini pia tunagawa vifaa, lakini pamoja na hilo tumeimarisha dolia za askari, kuhakikisha kwamba hawa wanyama wanapoingia kwenye maeneo ya wananchi basi askari wa doria wanakuwepo kwenye maeneo husika.

Mheshimiwa Spika, nimtoe wasiwasi Mbunge kwamba suala hili Serikali inalitambua na tunaendelea kufanya kazi na hatulali mchana na usiku tunahakikisha wananchi waishi kwa amani. Ahsante.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro kati ya Hifadhi ya Lwafi iliyopo Nkasi Kusini na wananchi wa Vijiji vya Mlambo, King’ombe, Tundu na Kata ya Wampembe?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na jitihada ambazo zinafanywa na Serikali, Wizara imekuwa ikisema kwamba upandaji wa pilipili kwenye maeneo ambayo yanakaribiana na vijiji una uwezo wa kuzuia tembo kuingia vijijini. Sasa, je Serikali hiko tayari kupitia TANAPA na taasisi zake wakapanda wao hizi pilipili ili wawasaidie wananchi wetu wasihangaike, mazao yao yasiliwe na wao wasiuliwe?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nape, Mbunge wa Mtama, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli tulishabuni mbinu mbadala za kuhakikisha kwamba hawa wanyama wakali wanapunguza kasi ya kuathiri wananchi ikiwemo pilipili lakini pia kuna mizinga ya nyuki ambao ni njia bora zaidi ya kuwafanya hawa wanyama wasiweze kusogelea makazi ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, tunalipokea wazo lake, lakini kulingana na gharama Serikali itaendelea kuangalia tathmini na tunaweza tukafanya kwa awamu, kwenye maeneo ambayo yameathirika Zaidi. Hata hivyo, niwaombe tu Waheshimiwa tuendelee kushirikiana kwenye hizi mbinu ambazo tunaendelea kuzielekeza wakati Serikali sasa inaangalia mbinu ya kudumu ambayo inaweza ikasaidia wanyama hawa kuishi katika maeneo yao na wananchi wakaishi kwa amani.