Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kusambaza maji kutoka Mradi wa Maji Mhangu – Ilogi katika Kata za Lunguya, Ikinda, Shilela, Sogese na Mega katika Halmashauri ya Msalala?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nilitaka niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kumekuwa na malalamiko juu ya ongezeko la bili za maji katika Kata ya Isaka, Kata ya Bugarama; je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuunda tume na niombe au Waziri mwenyewe husika uweze kufika katika Kata ya Bugarama na Kata ya Isaka, ili kuweza kubaini nini chanzo cha ongezeko la gharama za maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kuna fedha iliyobaki katika mradi ambao unatoka Kagongwa – Isaka; je, Serikali ina mpango gani wa kutumia fedha hizo kuweza kuanza kusambaza maji katika Kata ya Mwakata? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, kaka yangu Iddi kwa kazi kubwa, nzuri anayoifanya katika Jimbo lake la Msalala, lakini kubwa ambalo nataka kulisisitiza ni haki ya mwananchi wa Tanzania kupatiwa maji na mwananchi naye asisahau kwamba ana wajibu wa kulipia bili za maji. Sisi kama Wizara ya Maji tutasimamia bili hizo zisiwe bambikizi. Tumetoa maelekezo mahususi kwa Taasisi ya EWURA yenye jukumu la kuidhinisha bili za maji na ripoti wamenikabidhi hivi karibuni, tutaifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusu swali lake la pili, tunakiri kuna fedha ambazo zimebaki katika mradi wa Isaka – Kagongwa. Tumetoa maelekezo mahususi kwa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira - Kahama, kufanya kazi ile kwa force account kuhakikisha vijiji vyote ambavyo vimebaki vipatiwe huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza, ahsante sana.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kusambaza maji kutoka Mradi wa Maji Mhangu – Ilogi katika Kata za Lunguya, Ikinda, Shilela, Sogese na Mega katika Halmashauri ya Msalala?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante; nilikuwa naomba kuuliza ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa Mradi wa Maji ya Kikafu ambao unalenga kuhudumia Kata ya Masama Kusini, Muungano, Bomang’ombe na KIA? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge wa Hai, kiukweli amekuwa mfuatiliaji mkubwa sana, ni mradi ambao amekuwa akiupigia kelele.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimpe taarifa tumekwishatoa kibali na tumetoa maelekezo kwa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira - MUWSA, Moshi kuhakikisha kwamba anatangaza kazi hiyo na mkandarasi apatikane mara moja kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kusambaza maji kutoka Mradi wa Maji Mhangu – Ilogi katika Kata za Lunguya, Ikinda, Shilela, Sogese na Mega katika Halmashauri ya Msalala?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, nikiwa mwakilishi wa Jimbo la Kawe mwaka 2010 mpaka 20 tulifanikiwa kwa kiwango kikubwa sana kupunguza tatizo la maji, lakini kuna kata kadhaa ambazo zimebaki bado ni sugu sana. Kata ya Wazo, hususan maeneo ya Nyakasangwe, Mivumoni, Salasala, Kata ya Mbezi Juu eneo la Mbezi Mtoni na Sakuvede. Sasa nataka tu commitment ya Waziri ni lini changamoto hii itafikia ukingoni? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nijibu swali na ninashukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa kukiri kwamba kuna jitihada kubwa ambayo Serikali imefanya katika Jiji la Dar es Salaam na nikiri bado kuna changamoto katika eneo la Mivumoni na maeneo ambayo ameyataja ya Wazo, lakini kuna kazi kubwa ambayo inafanywa juu ya utandazaji wa miundombinu na usambazaji wa maji inayofanywa na DAWASA, zaidi ya kilometa 1,600 ambazo tutaenda kutekeleza. Nataka nimhakikishie sisi kama Wizara tutasimamia kuhakikisha maeneo haya yanapata maji kwa haraka na wananchi waweze kupata maji, ahsante. (Makofi)