Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Bulamba – Bukonyo hadi Masonga yenye urefu wa kilometa 32.23 kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali ya nyongeza. Barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa wananchi wa Ukerewe, inasaidia wananchi wanaoenda Kivuko cha Bugorora kwenda Ukara ambako kuna hospitali mpya sasa ya Wilaya ya Bwisya; barabara hii inasaidia wananchi wanaoenda Kakukuru ambapo ndiyo msingi wa uchumi wa Ukerewe, pia inasaidia wananchi wanaoenda Mliti mpaka Lubya kwenye msitu wa Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, pesa hizi za matengenezo ya kawaida zinazotengwa zimekuwa hazisaidii sana kwa sababu inakuwa nzuri kwa muda mfupi, lakini inakuwa haipitiki kwa muda mrefu. Ni kwa nini sasa Serikali isianze kuifanyia Barabara hii upembuzi na hatimaye upembuzi yakinifu ili hatimaye sasa ianze kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ambalo kimsingi siyo swali, ni ushauri; kwenye Kivuko cha Bugolola kwenda Ukara kumekuwa na shida ya kivuko kile na inaweza kusababisha ajali hata gari kutumbukia majini. Kinachohitajika ni kuweka Moorum au trip kadhaa za mawe ili kutengeneza gati lile ili wanananchi waweze kuvuka kwa usalama. Kwa hiyo, nitoe ushauri kwa Wizara, kwa haraka na kwa dharura, ifanyie kazi jambo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali lake la kwanza Mheshimiwa Mkundi ameomba barabara yake hii ifanyiwe upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge wa Ukerewe Mkundi kwamba tumepokea ombi, tutalifanyia kazi ili tufanye tathimini ya kina halafu tuweze kujua gharama ambayo inahitajika kuwekwa kiwango cha lami ili barabara iweze kutengenezwa na kupitika kwa wakati wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili tumepokea ushauri ambao naomba nimwelekeze Mkurugenzi wa vivuko Tanzania kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, kwa kuwa amesema kuna hali hatarishi ya maisha katika eneo hili, afanye tathmini, aangalie hali halisi, halafu tuweze kuchukua hatua ya dharura ili kuweza kuokoa maisha ya watu wetu katika eneo hili. Ahsante.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Bulamba – Bukonyo hadi Masonga yenye urefu wa kilometa 32.23 kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali dogo la nyongeza. Naomba kuuliza, Serikali iliahidi kutangaza tender ya ujenzi wa barabara ya Bigwa – Kisaki.

Je, ni lini Serikali itatangaza barabara hii?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni kweli kwamba kwa sasa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ipo kwenye hatua mbalimbali za kutangaza baadhi ya barabara ili ziweze kujengwa kwa hatua mbalimbali, nyingine kwa kiwango cha lami na mengine ni madaraja ya kujengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira na maelezo mengine ya ziada yatatolewa kwenye bajeti yetu ambayo inatarajiwa kusomwa Jumatatu ijayo tarehe 17 na tarehe 18. Ahsante.

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Bulamba – Bukonyo hadi Masonga yenye urefu wa kilometa 32.23 kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya Stalike – Kibaoni yenye urefu wa kilometa 71 ni ahadi ya Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na tayari barabara hiyo imeshafanyiwa upembuzi yakinifu.

Swali langu kwa Serikali: Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami katika barabara hii, ukizingatia Mkoa wa Katavi ni moja kati ya mikoa michache sana ambayo bado haijafanikiwa kuunganishwa Mkoa na Mkoa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba barabara hii ni muhimu na Mkoa wa Katavi upo kwenye mchakato wa kupata barabara za lami. Kama nilivyosema, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira, bajeti yetu inaanza kujadiliwa tarehe 17 na tarehe 18 hapa Bungeni. Nitapata fursa ya kuwatajia barabara ambazo tumetangaza kwa mwaka huu na mwaka wa fedha ujao.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie katika barabara muhimu ambazo zinajengwa kwa kiwango cha lami ni pamoja na kuunganisha Mkoa wa Katavi na maeneo mengine. Ahsante sana.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Bulamba – Bukonyo hadi Masonga yenye urefu wa kilometa 32.23 kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Marais wetu waliopita akiwemo Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli waliahidi ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Mbalizi – Shigamba:-

Je, ni lini sasa hiyo barabara itajengwa kwa kiwango cha lami? Nashukuru. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Njeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, ahadi zote za Viongozi Wakuu wa Nchi akiwemo Dkt. Hayati Magufuli, Mama Samia, Mheshimiwa Waziri Mkuu na viongozi wengine, ahadi hizi lazima zitekelezwe kwa sababu ni ahadi ya Serikali na Serikali ipo kazini inafanya kazi na kazi inaendelea.

Naomba nimhakikishie Mheshimiwaa Mbunge kwamba, barabara yake hii kama ilivyoahidiwa itafanyiwa kazi, itajengwa kwa kiwango cha lami, tupeani ushirikiano na muda si mrefu ahadi hiyo ya viongozi itatimia kabla ya 2025. Ahsante. (Makofi)

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Bulamba – Bukonyo hadi Masonga yenye urefu wa kilometa 32.23 kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Umuhimu wa barabara ya Mkundi ni sawasawa na barabara ya Mugala kwenda Busambala. Je, ni lini Serikali itafikiria kuijenga barabara hii katika kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Mwibara, mdogo wangu Mheshimiwa Kajege, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza eneo hili nalifahamu, mimi natoka katika Mkoa wa Mara na tumeshapata taarifa, Mheshimiwa Mbunge hapa ameulizia ili wananchi wasikie kama analisemea katika Bunge hili Tukufu. Mheshimiwa Mbunge tuliwahi kuzungumza nje ya box, inafanyiwa kazi na asubiri tarehe 17 na 18 atapata majibu sahihi. Kwa hiyo, watu wa Mwibara na Mkoa wa Mara kwa ujumla na mikoa mingine yote tutazifanyia kazi. Ahsante. (Makofi)