Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Ibungu – Kafwafwa hadi Kyimo itafanyiwa upembuzi yakinifu na kuanza ujenzi kwa kuwa imetajwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025?

Supplementary Question 1

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Wizara. Hii barabara ni muhimu sana kwa upande wa Rungwe lakini pia kwa upande wa Ileje. Ni barabara kwa upande wa Rungwe inapita kwenye Kata ya Kyimo, Iponjola pamoja na Ikuti ambapo kuna milima mikali, barabara muda mwingi inakuwa sio nzuri. Kwa hiyo naomba Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ituambie exactly ni lini hii barabara itaanza kufanyiwa upembuzi yakinifu ili ijengwe kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni lini barabara ambayo pia ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2020 - 2025 kutoka Kiwira kupitia Kata ya Kinyala, Igogwe mpaka Mbalizi itafanyiwa pia upembuzi yakinifu na kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kwa pamoja ya Mheshimiwa Anton Mwantona, Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Ibungu –Kalembo – Katengele - Sange - Luswisi – Kafwafwa - Ikuti hadi King’o ni kweli ni barabara ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Ileje na Rungwe. Nataka nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutahakikisha kwamba katika awamu hii ya miaka mitano barabara hii inafanyiwa usanifu na upembuzi yakinifu na mimi ni mnufaika kwa sababu inapita kwenye Jimbo langu na kwenye Kijiji changu pia cha Kalembo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mbunge kwamba barabara hii itafanyika kama tulivyoahidi kwenye Ilani ya Uchaguzi. Pia, barabara hii ya Kiwira – Kinyala - Igogwe hadi Mbalizi nayo pia iko kwenye Ilani ambayo nayo pia imeainishwa kati ya barabara zile ambazo zitafanyiwa usanifu wa kina. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Rungwe na wa Ileje kwamba barabara hizi tutahakikisha kwamba zinafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa lami kadri fedha zitakavyopatikana. Ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Ibungu – Kafwafwa hadi Kyimo itafanyiwa upembuzi yakinifu na kuanza ujenzi kwa kuwa imetajwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025?

Supplementary Question 2

MHE. MOHAMED M. LUJUO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa muda ili niulize swali langu la nyongeza. Barabara inayounganisha Wilaya ya Kiteto na Makao Makuu ya Mkoa wao wa Manyara inapita kwenye Jimbo langu, lakini sehemu ya barabara hiyo Kijiji cha Kelema Maziwani daraja limekatika na ni miezi sita sasa. Sasa, naomba kujua ni lini daraja hili litajengwa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Moni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, TANROADS wanafanya tathmini ya barabara zote ambazo zimepata changamoto ya mvua ikiwa ni pamoja na madaraja. Wizara kupitia TANROADS kutokana na uzoefu uliotokea miaka miwili, mitatu iliyopita tumeandaa madaraja ya muda kwa ajili ya kutatua changamoto za madaraja ambayo yamesombwa ama kuharibika. Sasa hivi inakuwa ni ngumu kurekebisha hayo madaraja kwa sababu yanahitaji kutengeneza tuta halafu madaraja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hata ungeweka sasa hivi ni wazi kwamba daraja hilo litasombwa kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba daraja hilo ambalo liko katika hiyo barabara ya Kiteto Manyara litakuwa ni kati ya madaraja ambayo yatahakikishwa kwamba yanajengwa ili kurudisha mawasiliano ambayo yamekatika kwa kipindi alichokitaja Mbunge. Ahsante.