Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Nyololo – Mtwango – Mafinga hadi Mgololo?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, nishukuru kwa majibu ambayo yametolewa kwa kuzingatia kwamba barabara hizi tumezipigia kelele kwa muda mrefu na tunategemea zitusaidie kutuvusha kwenda uchumi wa kati wa juu, kwa sababu ndizo zinakusanya viwanda vyote kule ambapo tunakusanya zaidi bilioni 40 kwa mwaka na pengine kwa miaka kumi ni nusu trilioni. Fedha hizi zote zinakwenda kujenga maeneo mengine, pale wananchi wakitaabika na hivi ninavyozungumza magari hayapatiki.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza la nyongeza; kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alisema hapa Bungeni mwezi Februari, zingeingizwa kwenye mwaka wa fedha huu 2021/ 2022; na kwa kuwa amezungumza pia usanifu umekamilika wa barabara hii moja. Kwa nini sasa hii iliyokamilika ya kilomita 40 ya kutoka Nyololo mpaka Mtwango isianze kujengwa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; hii ya pili ambayo amesema usanifu unakamilika ni ipi commitment ya Serikali sasa, itaanza lini na itakamilika lini? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi Kusini, kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama Mheshimiwa amesikiliza jibu la msingi, tunatambua kwamba mbao zote karibu tunazoziona zinatoka eneo la Mafinga zinapita huko, magogo ni mengi. Ndio maana katika jibu langu la msingi nimesema mwaka 2022/2023, Serikali inatoa commitment kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sababu ni barabara ambayo sasa zimekuwa ni changamoto kwetu kutokana na uzito mkubwa kwamba kwa uwezo wa changarawe barabara zinashindwa kuhimili uzito wa magari yanayopita hapo. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Mufindi Kusini kwamba commitment ya Serikali ni kama tulivyosema kwenye jibu la Msingi tutaanza kujenga 2022/2023. Ahsante.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Nyololo – Mtwango – Mafinga hadi Mgololo?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Pawaga kilomita 76 ambazo zilikuwa ni ahadi ya hayati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mbaya mno na wakulima wa pale wanalima mpunga lakini wanashindwa kusafirisha. Je, ni lini Serikali itakwenda kujenga barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Iringa Pawaga ni kama barabara zingine ambazo zimepata changamoto kubwa katika kipindi hiki cha mvua. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hizi zipo kwenye ahadi na zitategemea na upatikanaji wa fedha. Pale ambapo fedha zitapatikana barabara hizo zitajengwa na ndioyo azma ya Serikali lakini kinachotukwamisha ni uwezo wa bajeti yetu. Kwa hiyo nimhakikishie fedha zikipatikana barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Nyololo – Mtwango – Mafinga hadi Mgololo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa Spika, Nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tuna Barabara yetu ya Korogwe Mjini ambayo inatokea Old Korogwe, Kwamndolwa, Magoma, Mashewa, Bombo Mtoni mpaka Mabokweni, ambayo ni ahadi ya Marehemu Rais Magufuli, Mama Samia na Waziri Mkuu. Je, ni lini Serikali itatekeleza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami ili kutimiza ahadi ya viongozi wetu wa kitaifa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara alizozitaja Mheshimiwa Mbunge wa Korogwe zipo kwenye ahadi ya Rais na zipo kwenye Ilani na ni kati ya barabara ambazo zinakamilisha kilomita 6,006 ambazo zimeahidiwa kujengwa katika kipindi hiki cha miaka mitano. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kadri fedha itakapopatikana barabara hizi ikiwemo na hii zitajengwa kwa awamu. Ahsante.