Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Magu – Bukwimba hadi Ngudu itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ili kuu nganisha Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba na Makao Makuu ya Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 1

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuwa barabara hii ni ya muhimu sana kwenye uchumi wa nchi yetu na uchumi wa Kanda wa Ziwa, kwasababu inapunguza umbali wa kutoa Shinyanga mpaka Mkoa wa Mara kuelekea nchi jirani ya Kenya, kwa zaidi ya kilometa 73 na Serikali imekuwa ikiahidi ujenzi wa barabara hii katika Awamu kuanzi ya Tatu mpaka Awamu ya sasa na Wananchi wa Wilaya ya Kwimba wanahitaji kuunganishwa na Makao Makuu yao mkoa wao kwa barabara ya kiwango cha lami.

Je, ni lini sasa Serikali itaachana na maneno ya kutafuta pesa na kuanza kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, barabara inayoanzia Fulo kupitia Nyambiti mpaka Malia yenye urefu wa kilometa 73 pia ni barabara muhimu sana kwenye uchumi wa Wilaya ya Kwimba na barabara hii imeahidiwa kwenye ukurasa wa 77 wa ilani ya Chama cha Mapinduzi kuanza kufanyiwa upembuzi yakinifu na hatimaye kujengwa kwa kiwango cha lami. Je, ni lini sasa Serikali itaanza kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami? Nakushukuru.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika Awamu ya Tano iliyopita taratibu za ujenzi kwa kiwango cha lami umeanza na ndiyo maana tumekamilisha usanifu wa kina mwaka 2019 kwa hiyo si tu zimekuwa ni ahadi lakini tayari tumeshaanza utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Sumve kwamba barabara aliyoitaja ya Fulo Nyambiti Malia ameisema mwenyewe kuwa imeainishwa kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi na nimuhakikishie katika kipindi hiki cha Awamu ya Sita kama tulivyosema imeanishwa kwenye ilani, lakini pia imeongelewa na Mheshimiwa Rais wakati analihutubia Bunge hapa ni kati ya barabara ambazo zitafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mbunge na Wananchi wa Sumve kwamba tutatekeleza kama tulivyopanga ahsante.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Magu – Bukwimba hadi Ngudu itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ili kuu nganisha Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba na Makao Makuu ya Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa swali la nyongeza kwa kuwa barabara ya kutoka Kalenga kwenda Ruaha National Park ni muhimu sana kwa uchumi wa Taifa hili hasa unaotokana na utalii na kwa kuwa upembuzi yakinifu na usanifu ulishafanyika siku nyingi. Na kwa kuwa pia Serikali imeweka kwenye ilani tangu Awamu ya Nne mpaka sasa na imekuwa ikitenga fedha kidogo kidogo. Je, kwa nini sasa Serikali isianze kujenga kidogo kidogo kutokana na hizo pesa wanazotenga maana imekuwa ahadi ya muda mrefu? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Kiswaga Mbunge wa Kalenga asubiri bajeti tutakayo pitisha nina hakikika ni kati ya barabara kama endapo bajeti itapita itakuwa ni kati ya barabara ambazo zitatekelezwa kuanzia bajeti tunayoiendea. Kwa hiyo, naomba awe na subira na asubiri tutakapo anza kupitia bajeti ya Ujenzi na Uchukuzi.