Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA aliuliza:- Je ni lini Serikali itajenga barabara inayounganisha Jimbo la Ukonga na Mbagala kwa mkupuo badala ya kujenga kilometa moja kila mwaka ili kuondoa kero ya usafiri kwa wakazi wa Majimbo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, pamoja na salamu za shukrani na pongezi kwa Mheshimiwa Waitara kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi na shukurani zetu kwa Mheshimiwa Rais kwa kumpa nafasi hii, tunaamini swali hili angeweza kulijibu bila hata kusoma, kwa nasaba yake na Jimbo la Ukonga. Naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Jimbo la Ukonga na Jimbo la Mbagala ndiyo majimbo pekee kwenye Mkoa wa Dar es Salaam ambayo hayaunganishwi na barabara ya lami; na barabara hii ni barabara muhimu sana kwa wananchi wa Kata ya Chanika, Msongola kujiunga na Jimbo la Mbagala.

Naomba commitment ya Serikali kipande hiki kidogo kilichobaki cha kilometa 4.95 ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa mazingira ya Jimbo la Ukonga yanafafana na Jimbo la Mbeya Mjini, ni lini Serikali itapanua barabara ya TANZAM inayotoka Dar es Salaam kuelekea Tunduma, kipande cha Uyole – Tunduma kilometa 104, na kipande cha Uyole – Igawa kilometa 116. Barabara hii inasomeka ukurasa wa 66 wa Ilani yetu ya Uchaguzi yenye kurasa 303. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ili ni swali la kihistoria, Waswahili wanasema mtoto mpe mchawi akulelee. Ni kweli kwamba barabara ya Mbagala – Mbande naifahamu na Mheshimiwa Jerry pamoja na Mheshimiwa Chaurembo Mbunge wa Mbagala, nilipoteuliwa kuwa Naibu Waziri katika eneo hili suala la kwanza, hata hawakunisalimia, walitaja barabara hii na kwa sababu ya umuhimu wake. Barabara hii ikijengwa vizuri kiwango cha lami wananchi wanaweza wakatoka Ukonga wakaenda Mbagala wakaenda Kusini au Kusini anakuja Dodoma haina sababu ya kupitia mjini kuepuka foleni anaweza akapita eneo hili.

Mheshimiwa Spika, nimekwishaongea na Chief wa TANROAD Engineer Mfugale, kwamba walikuwa wametenga fedha vipande vipande vya matengenezo mbalimbali katika eneo hili. Kuanzia mwezi Julai mwaka mpya wa fedha 2021/2022 Mheshimiwa Jerry na Mheshimiwa Chaurembo barabara hii kilometa 4.9 zitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ili watu waweze kupata huduma katika eneo hili.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, wiki iliyopita Mheshimiwa Naibu Spika alikalia kiti hapo ulipokaa, akatoa malalamiko kwamba eneo lake daraja lilivunjika tangu 2019 na mpaka leo anapozungumza na asubuhi amenikumbusha mkandarasi hayupo site na nilitoa maelekezo hapa kwamba mkandarasi aende site wafanye kazi ya dharura ili kuwa na uunganisho katika eneo hilo ili watu wapite.

Mheshimiwa Spika, leo nazungumza habari ya barabara. La kwanza, kabla leo jua halijazama nipate maelezo kwa nini mkandarasi hajawa site katika eneo lile, daraja lile halijatengenezwa tangu 2019 mpaka leo. La pili, kwa kibali chako na kibali cha Mheshimiwa Waziri Mkuu weekend ijayo nitaenda Mbeya kutembelea barabara hii pamoja na daraja nione kama kweli mkandarasi hayupo site, baada ya hapo tutaongea vizuri. Ahsante.