Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara za lami katika Kata za Ufukoni, Magomeni na shangani Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Spika, kwanza nitoe shukurani kwa majibu, lakini nataka niseme kwa mradi ambao unazungumzwa wa TACTIC mradi huu nadhani ulishapangiwa fedha, lakini mpaka sasa hivi jinsi ninavyozungumza kuhusu Kata ya Magomeni na Ufukoni bado hali ni mbaya. Je, Serikali ni lini ujenzi wa barabara hizi utakua tayari?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili ni lini miundombinu ya mifereji ambayo tulikua tunaizungumza toka mwanzo Serikali itakua tayari kuweza kuboresha mifereji ambayo sasa hivi mara kwa mara kunapatikana mafuriko makubwa na wananchi inatokea hali sinto fahamu kwenye majumba ya watu na wengine kupoteza maisha. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ametaka kufahamu ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ambazo ameziainisha zilizopo katika mradi wa TACTIC kwa kifupi ni kwamba mradi wa TACTIC bado katika hatua za mwisho za makubaliano na mahafikiano na Serikali ili zianze kutekezwa.

Kwa hiyo, Mbunge nikuhakikishie kabisa kwamba mara baada ya huu mradi kuwa umekamilika na Serikali kumaliza hatua zote, barabara hizo ambazo umeziainisha zitaanza kujengwa kwa sababu ziko katika mradi wa TACTIC.

Mheshimiwa Spika, vile vile, katika sehumu ya ule mradi wa TACTIC miongoni mwa component ambazo ziko ndani yake ni pamoja na ujenzi wa mifereji kwa hiyo, mradi huu utakapokua umefikia hatua za mwisho na ninaamini Serikali ipo katika mazungumzo na ninahuhakika kabisa mara itakavyokamilia basi barabara zako pamoja na mifereji ya wananchi wa Mtwara Mjini itajengwa kama ambavyo imeainishwa katika huo mradi ahsante sana.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara za lami katika Kata za Ufukoni, Magomeni na shangani Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru changamoto iliyopo Mtwara ya barabara inafanana sana na changamoto Nkasi. Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano alituahidi wana Nkasi kipande cha barabara kutoka Chala mpaka Mpalamawe, ningependa kupata commitment ya Serikali kwa kuwa ahadi zote zinakua recorded ni lini ahadi hiyo itatekelezwa.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ametaka kujua tu ni lini ahadi ya Mheshimiwa Hayati Rais ama niseme ahadi zote za viongozi ni kwamba sasa hivi Ofisi ya Rais, TAMISEMI ipo katika hatua ya mwisho tunakusanya na kuandaa mpango wa namna ya kutekeleza ahadi zote za viongozi na nikuhakikishie tu kwamba kuanzia mwaka wa fedha ujao tutaanza kutenga pole pole fedha kwa ajili ya kuhakikisha zile ahadi zote ambazo viongozi wakuu walikua wamezitoa zinaanza kutekelezeka.

Mheshimiwa Spika, na kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Sita ni Serikali makini na imeshazungumza hadharani kwamba kazi inaendelea yale yote yaliyozungumzwa tutayaendeleza kuhakikisha kwamba tunawahudumia wananchi wetu vizuri. Kwa hiyo, waambie wananchi wa Nkasi Kaskazini kwamba zile ahadi zilizoaidiwa Serikali itazitekeleza kwa vitendo ahsante.