Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jaffar Sanya Jussa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Paje

Primary Question

MHE. JAFAR SANYA JUSSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itavipatia Vituo vya Polisi vya Paje na Jambiani samani za Ofisi pamoja na magari kwa ajili ya doria?

Supplementary Question 1

MHE. JAFAR SANYA JUSSA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, je, ni lini Mheshimiwa Naibu Waziri atafanya ziara kuvitembelea vituo hivyo vya Jambiani na Paje na nyumba za askari wa Jeshi la Polisi Makunduchi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, ni lini Serikali italipatia Jeshi la Polisi, Wilaya ya Kusini gari kwa ajili ya doria?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sanya kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue fursa hii nimpongeze sana Mheshimiwa Sanya. Hakika amekuwa anafanya kazi kubwa sana ya kuwasaidia wananchi wa Jimbo la Paje hasa wa maeneo ya Jambiani, Paje, Bwejuu, Makunduchi, Kizimkazi, Mtende na maeneo mengine ya jirani ili kuhakikisha kwamba wanapata kwa utulivu na uhakika huduma za usalama na ulinzi katika maeneo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikwambie tu ndani ya Bunge hili tumeshapanga na Mheshimiwa Sanya twende tukakabidhi mabati kwa ajili ya kuezeka Kituo cha Paje na fedha hizi zitatoka ndani ya mfuko wake. Kwa hiyo nimpongeze sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sanya. Kwanza anauliza je, niko tayari kwenda kuangalia maeneo hayo? Nimejibu tu kwamba niko tayari na nimuahidi tu kwamba ndani ya Bunge hili la Bajeti tutapanga siku tuchupe mara moja twende tukakague, tukayaone hayo maeneo. Tukazione hizo hali na changamoto, halafu tujue namna ya kuzitafutia ufumbuzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini je, tuko tayari kutoa gari? Nimwambie tu kwamba awe na Subira, katika bajeti ijayo tutajitahidi Vituo vya Paje na Jambiani, Wilaya wa Kusini Unguja tuvizingatie zaidi katika kuhakikisha kwamba wanapata gari kwa ajili ya kufanya doria za ulinzi na usalama katika Jimbo lake. Nashukuru.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. JAFAR SANYA JUSSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itavipatia Vituo vya Polisi vya Paje na Jambiani samani za Ofisi pamoja na magari kwa ajili ya doria?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya miundombinu inayoikabili Jeshi la Polisi nchini inaikabili sana Wilaya ya Mbulu. Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Mbulu kilijengwa mara baada ya uhuru, kwa sasa kina uchakavu mkubwa. Je, ni lini Serikali itatatua tatizo hili la uchakavu wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Mbulu na makazi ya askari katika Wilaya yetu ya Mbulu? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu letu kama Serikali na Wizara ni kuhakikisha kwamba ulinzi na usalama wa nchi unaenea kila mahali. Hilo la kujenga vituo vya polisi na kuvipatia magari, yote ni sehemu ya jukumu na wajibu wetu. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge, awe na subira kidogo kwa sababu kasungura bado kadogo lakini kakija kakichononoka kidogo, basi hilo ni jambo ambalo linawezekana na tukipata fedha ya kutosha, basi tutampelekea kituo cha polisi na huduma nyingine za polisi katika Jimbo lake. Nashukuru.