Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la mafuriko katika maeneo ya Mbweni Teta, Bunju Basihaya, Kunduchi, Nyamachabes, Ununio na Mikocheni katika Jimbo la Kawe?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa sababu mpaka sasa kuna kaya kumi ambazo maji yameingia ndani na hawana pa kuishi katika Mtaa wa Ununio, Serikali ina mkakati gani wa dharura kabla ya kutekeleza mradi huu alioutaja ili kuhakikisha wananchi hawa wanapata mahali pa kuishi na sehemu zile nilizoainisha zinapata majibu mapema? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kilio hiki ni cha nchi nzima kwa maana matatizo haya yamekuwa yanajirudia kila eneo la nchi; ni lini basi Serikali itaweka mikakati madhubuti ya kujenga mifereji imara ili basi maeneo haya maji yaweze kuelekezwa kwenda kwenye maziwa, mito hata bahari ili kuepuka adha ya magonjwa ya milipuko pia na adha kwa wananchi? Ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Felista Deogratius Njau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza alikuwa anaomba kujua upi ni mkakati wa dharura katika eneo la Ununio ambao Serikali imeuweka kuhakikisha tunatatua tatizo hilo la mafuriko. Nimuambie tu kabisa kwamba Serikali iko kazini na baada ya janga hili inafanya tathmini ya mwisho kuhakikisha kwamba tunasaidia maeneo hayo hususan maeneo ya Ununio katika Kata hizo ambazo Mheshimiwa Mbunge ameziainisha.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili Mheshimiwa Mbunge ameuliza ni lini Serikali itaweka mikakati madhubuti kuhakikisha kwamba tunaondoa majanga haya hususan kwa kujenga mifereji. Nimhakikishie kabisa kwamba sasa hivi moja ya mkakati mkubwa ambao Serikali unao katika kila barabara tunayoijenga tunaambatanisha na ujenzi wa miundombinu hususan mifereji. Kwa hiyo, hiyo ni sehemu ya mikakati ambayo ipo na tutaendelea kufanya hivyo. Kwa kadri fedha zitakavyopatikana tutajenga mifereji mikubwa pamoja na midogo kuhakikisha janga la mafuriko nchi nzima katika maeneo yote ambayo tunayasimamia hayapatwi na hii adha ambayo Mheshimiwa Mbunge ameianisha. Ahsante sana.