Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa maji kutoka Mto Mavuji kwa ajili ya wakazi wa Miji Midogo ya Kilwa Kivinje na Kilwa Masoko?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza niishukuru Serikali kwa majibu mazuri na ufuatiliaji na usimamizi madhubuti wa mradi huu, lakini nina swali la nyongeza. Mosi, kwa kuwa mradi huu utachukua miezi 24 tangu kuanza kwa utekelezaji wake maana yake ni miaka miwili, lakini pia utakuwa ni mradi wa kutoka katika chanzo cha maji kuelekea katika miji hii miwili niliyoitaja ya Kilwa Masoko na Kilwa Kivinje, lakini viko vijiji ambavyo vitakuwa mbali na mradi huu. Je, Serikali itakuwa tayari kwa upendeleo wa kipekee kutenga bajeti kwa mwaka huu kwa ajili ya vijiji angalau vitatu vya Nainokwe, Limalyao pamoja na Mandawa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Mohammed Kassinge kutoka Kilwa Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunapoongelea miezi 24 wakati fulani kwa sababu ya changamoto kubwa ya maji ni muda mrefu, lakini naendelea kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo ameendelea kuwa karibu na sisi na kwa hakika namna ambavyo anafuatilia tutahakikisha tunakamilisha vile vijiji sio vitatu, ila kwa sasa hivi kwa mwaka huu wa fedha tutajitahidi tumchimbie kisima kimoja cha maji, lakini hivi vingine vitaingia kwenye Mpango wa Mwaka ujao wa Fedha. Haya maeneo ya vijiji vyake vitatu ambavyo viko mbali na mtandao wetu wa mabomba tutahakikisha tunakuja kuwahudumia wananchi kwa mtandao wa visima.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa maji kutoka Mto Mavuji kwa ajili ya wakazi wa Miji Midogo ya Kilwa Kivinje na Kilwa Masoko?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo la maji lililopo Kilwa linafanana kabisa na matatizo ya maji yaliyoko Jimbo la Ndanda hasa zaidi upande wa Magharibi kwenye Kata za Mlingula, Namajani, Msikisi, Namatutwe pamoja na Mpanyani. Swali langu, je, ni nini hasa mpango wa Serikali wa muda mfupi wa kuhakikisha kata hizi nilizozitaja zinapata maji kabla hatujaingia kwenye kiangazi kikuu kinachoanza mwezi Julai na Agosti. Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwambe kutoka Ndanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Maji wakati wote tunajitahidi sana kuona tunatatua tatizo la maji kwa kutumia vyanzo mbalimbali kwa sababu tuna michakato ya muda mrefu pamoja na kutumia Mto Ruvuma kwa mwaka ujao wa fedha, lakini katika kuona kwamba wananchi tunakwenda kuwapunguzia makali ya matatizo ya maji kwa mwaka huu wa fedha, Mheshimiwa Mwambe kama ambavyo umekuwa ukifuatilia mara zote, tumeongea mara nyingi. Kwa hiyo, hili nalo tukutane tuone tuanze na kisima upande upi ili tuweze kupunguza haya matatizo. Maji Ndanda ni lazima yatoke, mabomba yamwage maji, tuokoe ndoa za akinamama, tutahakikisha hawaendi kukesha kwenye vyanzo vya maji. (Makofi)

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa maji kutoka Mto Mavuji kwa ajili ya wakazi wa Miji Midogo ya Kilwa Kivinje na Kilwa Masoko?

Supplementary Question 3

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nafurahi sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa katika Kata ya Masaka yenye Vijiji vitatu vya Sadani, Wanging’ombe pamoja na Makota havina kabisa maji hata kijiji kimoja. Je, Waziri sasa wakati anaangalia uwezekano wa kupata maji ya kutiririka anaweza hata akatuchimbia visima ili wananchi wa kule waendelee kunufaika na huduma ya maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nipende kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Kiswaga, Mbunge wa Kalenga. Mheshimiwa Kiswaga ni Mbunge ambaye kwa kweli nimeshazungumza naye mara nyingi na tayari tuna mradi kule tumekubaliana nakwenda kuuzindua.

Nipende kumhakikishia katika masuala ya visima Waheshimiwa Wabunge, hiki ni kipaumbele kimojawapo cha Wizara, tutafika Kalenga, tutachimba visima viwili, yeye ndiye atakayetueleza wapi zaidi kuna tatizo sugu ambalo mitandao ya mabomba ya maji ya kawaida hayafiki, basi visima Mheshimiwa Kiswaga atavipata.