Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Kusambaza Maji Mji wa Makambako utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali ya nyongeza mawili. Swali la kwanza; kwa kuwa kuna miradi inayoendelea katika Jimbo la Makambako, Mradi wa kwanza mkandarasi yupo Usetule-Mahongole; mkandarasi wa pili yuko Ibatu; na mkandarasi wa tatu yuko Mtulingana, Nyamande na Bugani. Je, ni, lini Serikali itawalipa wakandarasi hawa ili waweze kumalizia miradi hii kwa sababu wanakwenda kwa kususasua ili wananchi waendelee kupata maji yaliyokusudiwa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa mradi huu wa kutoka fedha Serikali ya India miji 28 ikiwemo na Mji wa Makambako. Miradi hii tangu yupo Waziri Profesa Maghembe inazungumzwa na kwa mara ya mwisho alipokuja Rais ambaye ni Marehemu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, wananchi wa Makambako waliuliza ni lini mradi huu utaanza? Sasa nataka kujua kwa sababu kuna baadhi ya watu wanataka kuwekeza viwanda pale, wanakosa kuweka viwanda, tunakosa wawekezaji wengi ni kwa sababu mradi huu haujaanza. Sasa nataka Serikali iniambie hapa na iwaambie wananchi wa Makambako, ni lini mradi huu utaanza ili wananchi waendelee kuwekeza viwanda kama ambavyo wanahitaji pale Mji wa Makambako? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, lini wakandarasi watalipwa? Tayari wakandarasi mbalimbali wameanza kulipwa na Wizara inafanya jitihada kila tunapopata fedha kuendelea kupunguza list ya wakandarasi ambao wanadai Wizara. Kwa hiyo kadri tunavyoendelea kupata fedha, list itakapomfikia mkandarasi huyu na yeye pia atalipwa.

Mheshimiwa Spika, Miji 28 utekelezaji wake kama nilivyojibu kwenye swali lake la msingi, mwishoni mwa mwezi Aprili mwaka huu 2021 utekelezaji wa miradi hii utaanza na itatekelezwa kwa miezi 24.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Kusambaza Maji Mji wa Makambako utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kiu ya wananchi wa Makambko inafanana kabisa na kiu ya wananchi wa Same. Mradi umechukua muda mrefu na wakati wa kampeni alipopita Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli wakati huo akiwa Naibu Waziri na sasa Waziri ndugu yetu Aweso, aje mara moja na yeye akasema yale yale maneno ya kutokushika kidevu lakini uchezee kitambi. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, je, ni lini wananchi hao wa Same watasambaziwa maji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze sana mama yangu Shally Raymond, amekuwa mpiganaji mkubwa sana hususan wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro; Moshi, Same na Mwanga waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, moja ya miradi ambayo ilikuwa imechezewa na wakandarasi wababaishaji ni Mradi wa Same – Mwanga na nilipata nafasi ya kwenda katika mradi ule, tumekwishawaondoa wakandarasi wale. Kubwa kazi hii tumeweza kuwapa wenzetu wa DAWASA kuona tunaweza kuifanya kwa force account, mwisho jana Katibu Mkuu alikuwepo huko, tumewekeza nguvu zetu kuhakikisha mpaka Desemba mradi ule uwe umekamilika na wananchi wale waweze kupata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Kusambaza Maji Mji wa Makambako utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kuuliza swali moja la nyongeza kwa niaba ya wananchi wa Sengerema. Ni kwamba tuna miradi mikubwa, Mradi wa Sengerema ni mradi mkubwa katika nchi hii, una bilioni 23, lakini una deni la shilingi milioni 300 kutoka TANESCO. TANESCO wamekuwa wakikata maji toka mradi huu umefunguliwa na kuna mabomba yako Sengerema pale yanasubiri kusambazwa kwenye hiyo miradi ya maji.

Je, Waziri yuko tayari kukubali wananchi wa Sengerema wauze yale mabomba halafu wakalipie umeme ili tukae salama sisi.

Mheshimiwa Spika, hili jambo ni kubwa na namwomba Mheshimiwa Waziri wa Maji, yuko tayari kufuatana na mimi kwenda Sengerema akaone hii hali?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza ukimuona mtu mzima analia ujue kuna jambo. Sasa niko tayari kuongozana naye lakini hapa niwe muwazi, Serikali eneo la Sengerema imewekeza zaidi ya bilioni 20, imetimiza wajibu wake, lakini ni haki ya mwananchi kupatiwa maji nay eye ana wajibu wa kulipia bills za maji. Kwa hiyo kubwa yawezekana kuna changamoto pia ya kiutendaji kushindwa kusimamia na kukusanya mapato. Haiwezekani uwe na mradi wa bilioni 20, halafu ushindwe kukusanya mapato angalau kulipia umeme, haiwezekani! Kwa hiyo nitafika na tutaangalia namna gani ya kumsaidia. Tukiona mtendaji yule anashindwa kutimiza wajibu wake, tutashughulikiana ipasavyo kuhakikisha wananchi wa Sengerema wanaendelea kupata huduma ya maji. (Makofi)

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Kusambaza Maji Mji wa Makambako utaanza?

Supplementary Question 4

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuweza kuuliza swali la nyongeza kwenye sekta hii muhimu. Suala zima la maji ya Mradi wa India imekuwa ni changamoto kubwa sana katika hii miji 28 na ambayo inasababisha Watanzania wengi kukosa maji. Nataka tu kujua, Mji wa Chemba ambao umekuwa kwenye ahadi ya Miradi ya India miaka nenda miaka rudi, ni lini Serikali itapeleka mradi mbadala wakati Watanzania wanaendelea kusubiri huo Mradi wa India ambao umeshindwa kutekelezeka kwa kipindi cha muda mrefu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nataka nimtoe hofu dada yangu Kunti, Mheshimiwa Mbunge. Serikali haijashindwa, Serikali ipo kwa ajili ya kutatua matatizo ya maji katika Taifa letu na ndiyo maana tuna miradi mikubwa mbalimbali ambayo tunaitekeleza. Katika eneo hili la miji 28, wewe ni mmojawapo ambao sisi umetumia hatua ya kutuita kuona hatua ya utekelezaji wake. Nataka nimhakikishie ukiona giza linatanda ujue kunakucha, timu yetu ya evaluation imekamilisha kazi. Naomba watupe nafasi waone namna gani Serikali hii ya mama yetu Samia Suluhu ambaye ametupa maelekezo mahsusi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunawatua akinamama ndoo za maji kichwani itafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la Chemba pamoja na hiyo miradi mikubwa ambayo ipo kimkakati, Mheshimiwa Mbunge tumekwishakutana nae ametuomba visima vya dharura katika eneo lake la Chemba ili wananchi wake waweze kuapat huduma ya maji. Ahsante sana.