Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza:- Uziwi ni moja ya aina ya ulemavu ambao una lugha yake ya ishara (signal language). (a) Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kufundisha Lugha ya Ishara kama moja ya masomo ya lazima Shuleni kwa wanafunzi wote kuanzia Elimu ya Awali ili kuondoa kikwazo cha mawasiliano kati ya wenye uziwi na wale wanaosikia? (b) Je, Tanzania tuna vitabu vya kufundishia Lugha ya Ishara katika lugha ipi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, lakini kabla sijauliza, niseme tu kwamba sijapata majibu kamili ya swali langu kwa sababu nilitaka kujua kwamba elimu ya viziwi itatolewa lini kwa wanafunzi wote wa shule zetu nchini ili kuweza kuondoa hicho kizingiti cha mawasiliano; lakini naona mjibu swali, Serikali inaonekana ina-focus katika kutengeneza mtaala wa kuboresha elimu kwa wale ambao ni viziwi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo naomba niulize maswali haya madogo ya nyongeza; swali la kwanza;

Je, katika nchi yetu tuna shule ngapi zinazotoa elimu kwa viziwi kwenye ngazi ya Msingi, Sekondari na Vyuo?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili ningependa kujua kwamba kwa kuwa katika nchi yetu lugha rasmi zilizo, zinazotumika kwa mawasiliano ni Kiswahili lugha yetu ya taifa nani ya kimataifa pia na kingereza; nikitaka kupata kitabu au Mtanzania akitaka kupata kitabu cha sign language kwa kiingereza na sign language ya Kiswahili atavipata wapi? Ahsante.

SPIKA: Mheshimiwa Kiruswa katika nchi nyingine wanafundisha hivyo compulsory kwa wanafunzi wote kusoma lugha ya alama?

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, kwanza ni-declare interest kwa sababu mimi nimekuwa nikisaidia watoto viziwi kusoma. Nina wachache wanasoma Kenya, nina watatu wanafikia kidato cha nne mwaka huu, na kitabu wanachotumia kinaitwa Kenya Sign Language. Lakini pia nilipokuwa nasoma Marekani nimeona American Sign Language; lakini hapa kwetu nafahamu shule moja ya msingi ambayo inasomesha viziwi iko Moshi -Kilimanjaro - Himo na wale wanasoma kwa Kiswahili. Sasa kunakuwa na crush, kwamba wale watoto walioko Kenya wakija wakikutana na hawa viziwi walioko Tanzania wengine wanaongea sign language ya Kiswahili lakini wenzao wanaongea sign language ya kiingereza. Sasa nilikuwa nataka kujua jinsi ambavyo tungeweza kuwa na hivyo vitabu vya sign language…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana, haya ahsante.

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: …katika lugha hizo ili tuweze kutoa hiyo…

SPIKA: Haya, ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri eneo hili nyinyi ndio wataalam, majibu tafadhali Mheshimiwa Juma Kipanga. (Kicheko)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Kiruswa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ameuliza suala la shule maalum mahsusi kwaajili ya wanafunzi wetu hawa wenye ulemavu wa usikivu. Tuna shule za msingi 14 ambazo ni mahsusi kabisa kwa ajili ya wanafunzi wetu hawa ambao wana matatizo ya usikivu. Pia shule za sekondari zipo 25, lakini vile vile tunachuo cha ualimu maalum kabisa ambacho kiko Patandi.

Mheshimiwa Spika, katika majibu yangu ya swali la msingi nilizungumza kwamba hivi sasa tunaboresha au tuko kwenye mikakati ya kuhakikisha kwamba tunakwenda kutoa elimu hiyo kama alivyoshauri Mheshimiwa Mbunge, kuanzia ngazi ya elimu msingi mpaka chuo. Lakini katika muktadha wa vitabu nimezungumza katika majibu ya msingi kwamba tumetunga kamusi ambayo inatumia hiyo lugha ya alama.

Mheshimiwa Spika, lakini wanafunzi hawa jukumu letu kubwa sana ni kuhakikisha kwamba tunapata walimu wa kufundisha lugha hizi za alama. Kwa upande wa vitabu, vitabu vinavyotumika ni vitabu vya kawaida kabisa kwa sababu wao wanaweza kuona suala lililokuwepo ni namna gani ni kuweza kufundishwa au kufundishika. Kwa hiyo jukumu letu tunaoenda nalo hivi sasa ni kuhakikisha kwamba tunatengeneza walimu wa kutosha wa kuweza kutumia lugha ya alama; na katika chuo chetu kikuu cha Dar es Salaam sasa tunatoa stashahada ya mwaka mmoja katika kipengele hiki cha lugha ya alama ili kuhakikisha kwamba tunapata walimu wa kutosha wakuweza kufanya service delivery na kutoa elimu hii kwa wanafunzi wetu hawa. Ahsante.