Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kazi ya ujenzi wa mradi wa Mto Msimbazi ambao umetajwa katika Bajeti ya mwaka 2021/2022?

Supplementary Question 1

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru ahsante.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii niipongeze na kuishukuru Serikali ya CCM ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuweza kukubali mradi huu ambao wananchi wa maeneo haya wameteseka kwa miaka mingi sana. Siyo tu kwamba mradi huu unakwenda kupata suluhisho la mafariko kwa watu wa Kigogo, Hananasifu, Magomeni na Mzimuni, lakini pia makazi yao yanakwenda kuboreshwa na uoto wa asili unakwenda kurudi, nina maswali mawili ya nyongeza;

Mheshimiwa Spika, pale Kigogo kuna mito mingine miwili midogo ambayo inaitwa Tenge na mwingine Kibangu, mito hii sambamba na mto Msimbazi wakati wa mvua maji yanakuwa ni mengi sana na wananchi wanataabika sana.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sasa tuko katika hatua za awali za upembuzi wa jinsi gani Mto Msimbazi unakwenda kujengwa; Je, Serikali inakubaliana na mimi ni wakati sasa wa kwenda kupeleka wataalam ili wakausanifu Mto Kibangu uchepushwe maji yake yahamie kwenye Mto Msimbazi ili kuwanusuru wananchi wa maeneo hayo na adha hiyo ya mafuriko?

Swali langu la pili, kwa kuwa katika Kikao cha Tatu cha Mkutano wa Bunge lililofanyika tarehe 29 Aprili mwaka huu, Serikali ilikubali kumpeleka Mheshimiwa Naibu Waziri kwenda kujionea mwenyewe maeneo yale. Je, sasa Serikali iko tayari kuniambia ni lini Mheshimiwa Naibu Waziri nitakwenda naye kule Kinondoni akajionee mwenyewe changamoto hizi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas Mbunge wa Kinondoni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza la Mheshimiwa Mbunge amelileta kama ombi kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI kama tuko tayari kupeleka wataalamu wakafanye tathmini juu ya mito midogo ambayo inapeleka maji ikiwemo Mto Kibangu na Tenge, niseme tu kwamba jambo hili tumelipokea na tutatuma wataalam wakafanye tathimini waone namna ambavyo lile eneo limeathirika jinsi hiyo mito itakavyoleta maji tuone na gharama jinsi zitakavyokuwa na mwisho wa siku, baada ya hapo maana yake tutatoa taarifa kama litafanyika kwa wakati gani kulingana na bajeti itakavyopatikana kulingana na tathimini ambayo tutakuwa tumeifanya.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili Mheshimiwa Mbunge ameomba tuongozane kwenda Kinondoni nafikiri mara ya Bunge hili kuisha tutakwenda tutafanya ziara katika eneo la Kinondoni pamoja na maeneo yete ya Dar es Salaam, kwa hilo niko tayari kwenda kujionea hizi athari zote zinazotokea. Ahsante. (Makofi)

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kazi ya ujenzi wa mradi wa Mto Msimbazi ambao umetajwa katika Bajeti ya mwaka 2021/2022?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, matatizo ya Mto Msimbazi ni sawa kabisa na matatizo ya yaliyoko kwenye Mto Milongo katikati ya Jiji la Mwanza, ninataka tu kufahamu mto huu umekuwa unasababisha maafa mara kwa mara mvua zinaponyesha.

Je, ni lini Serikali inao mkakati wa kuhakikisha mto huu unajengwa upya na kuwekewa tahadhari zote kuepusha maafa yanayowakuta wakazi wa Kata za Mabatini, Milongo, Mbugani pamoja na Kata yenyewe ya Nyamagana. Ni lini Serikali itachukua hatua kuhakikisha mto huu na wenyewe unakuwa kwenye hesabu ya kushughulikiwa. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Stanslaus Mabula Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ameleta ombi jipya la Mto Milongo ambao na wenyewe umekuwa na athari zinazofanana na Mto Msimbazi. Kwa hiyo, tunalipokea kwa sababu Serikali muda wote iko kazini, kama ambavyo tunakwenda kufanyia kazi Mto wa Msimbazi maana yake na la kwake vilevile tunalipokea na tukishalipokea maana yake tutafanya tathimini na katika mipango ya baadaye tutaliweka katika mipango yetu. Ahsante sana.