Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha uanzishwaji wa hati fungani za Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 1

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, ninashukuru Serikali kwa majibu mazuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Serikali imesema kwamba Halmashauri ambazo zitakidhi vigezo zitaanza kunufaika na hiyo hati fungani, sasa ni vigezo vipi ambavyo Serikali imeviweka kwa Halmashauri kuonekana zinakidhi.

Mheshimiwa Spika, pia kwa kuwa zoezi hili linaanza mwaka huu wa fedha, ni Halmashauri ngapi ambazo tayari zimekidhi vigezo.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bahati Keneth Ndingo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimetangulia kujibu katika swali la msingi, vigezo ni Halmashauri yoyote ambayo ina miradi ya kiuchumi, kimkakati ambayo imefanyiwa upembuzi yakinifu na kuonesha kwamba ina uwezo wa kurejesha fedha na faida. Kwa hiyo, Halmashauri yoyote ambayo itaibua mradi wowote wa maendeleo ambao tayari umefanyiwa upembuzi huo wana uwezo wa kutumia hati fungani ili kushirikisha umma na wadau mbalimbali kupata mtaji na kuwekeza na hatimaye kuhakikisha kwamba wanapata miradi ya maendeleo katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, vigezo ndiyo hivyo, ni ile Halmashauri yenye uwezo kwamba miradi yake ina tija na inaweza ikazalisha faida basi watahusika na utaratibu huu wa hati fungani. Ahsante sana.