Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO Aliuliza:- Jeshi la Polisi linashikilia pikipiki nyingi katika Vituo vya Polisi kwa muda mrefu. (a) Je, Serikali haioni fedha nyingi zinapotea kwa pikipiki nyingi kuchakaa zikiwa katika Vituo vya Polisi na hivyo kuleta hasara kwa Taifa? (b) Je, kwa nini Serikali isiunde Kamati Maalum kila baada ya miaka mitatu kupitia sababu zilizosababisha pikipiki hizo zishikiliwe kwa muda mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimwa Spika, ahsante. Naomba kumuuliza Mheshimwa Naibu Waziri maswalli mawili ya nyongeza pamoja na majibu mazuri aliyoyatoa. Swali la kwanza; ni ukweli usiopingika kwamba kama alivyosema ziko pikipiki ambazo labda wakati mwingine zinaokotwa na zinapelekwa pale. Kwa maana yake ni kwamba hakuna jalada lolote llinalofunguliwa kwenda mahakamani na matokeo yake pikipiki na magari kama hayo yanaweza kukaa zaidi ya miaka kumi.

Je, tunakubaliana kwamba sasa viendelee kukaa hapo na kuozea hapo au ni vizuri vikafanyiwa utaratibu mwingine ili hiyo fedha ikapatikana kwa ajili ya maendeleo ya nchi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wakati tunaunda Sheria ya kuruhusu bodaboda ili waweze kufanya kazi na kupata ajira kilichotokea ni kwamba zilezile faini zilizokuwa zinatumika kwenye vyombo vya usafiri ndio zilizochukuliwa na wakaanza kubandikwa bodaboda, lakini ikumbukwe kwamba bodaboda anabeba abiria mmoja, akikutwa na kosa analipa Shilingi elfu thelathini basi lenye abiria 60 akikutwa na kosa hilo hilo analipa elfu thelathini. Sasa napenda kujua ni lini Serikali itabadili hizi adhabu inayolingana na bodaboda ambayo ni ya chini ukilinganisha na adhabu iliyopo ambayo pia inatozwa kwa magari?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Vedastus M. Manyinyi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza ameulizia, je, Serikali haioni haja ya bodaboda hizi ambazo zimelundikana katika vituo hivyo vya polisi basi ziuzwe au zipigwe mnada ili sasa Serikali iweze kujipatia mapato? Jibu ni kwamba, uwepo wa pikipiki hizi kwenye vituo hivi kama nilivyosema katika jibu langu la msingi ni kutokana na sababu tofauti. Ukiziona pikipiki zimekaa kwenye Kituo cha Polisi usifikirie kwamba zimekaa kwa muda mrefu kwa sababu, utaratibu ni kwamba baada ya miezi sita endapo mwenye pikipiki yake asipokwenda kwenda kuikomboa pikipiki ama kulipa faini au taratibu nyingine akaziruhusu zikaendelea, maana pikipiki ile itaendelea kubakia pale.

Mheshimiwa Spika, baada ya miezi sita itaenda kupigwa mnada. Kwa hiyo inawezekana pikipiki hizo ambazo mnaziona kwenye Vituo vya Polisi ni kutokana na kwamba muda wake haujafika. Kwa mujibu wa taratibu hatutaweza kuipiga mnada ama kuiuza pikipiki ya mtu bila ya muda uliokusudiwa ama uliowekwa katika utaratibu kuwa haujafika.

Mheshimiwa Spika, utaratibu upo na kanuni na sheria zipo; ukiangalia kwenye PGO, ile 304 ukiangalia kwenye kifungu cha (1), (2), (3), (4), (5) na kuendelea imeelezwa Jeshi la Polisi limepewa mandate au limepewa mamlaka ya kuuza na kupiga mnada endapo itazidi zaidi ya miezi sita. Kwa hiyo hizo pikipiki zilizopo huko ni kwa sababu muda wake wa kufanyiwa hivyo haujafika, utakapofika hazitaonekana hizo. Aidha, nipende kusema kwamba tuendelee kushirikiana kutoa elimu huko kwa vijana wetu ili wasiendelee kuzifikisha huko.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa swali la pili, anasema, basi litapakia watu zaidi ya 30 faini yake ni Shilingi elfu thelathini, bodoboda ambayo inapakia mtu moja faini yake ni Shilingi elfu thelathini; sasa Serikali haioni haja hapa sasa ya kufanya marekebisho? Serikali katika hili bado haijaona haya ya kufanya marekebisho ya hili. The way itakavyofanya marekebisho kwa sababu nilivyomfahamu Mheshimiwa tushushe, maana kama basi watatoa shilingi 80,000, maana yake bodaboda watoe shilingi 10,000.

Mheshimiwa Spika, hizi Shilingi elfu thelathini ambazo zimewekwa bado matukio yanaongozeka na lengo letu sio kuwakomoa wananchi ama kuwakomoa vijana watumiaji wa bodaboda na pikipiki, lengo ni watu kufuata sheria kuepuka na kupunguza idadi ya ajali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mpaka kufika Disemba, 2020 ajali za bodaboda ni 164; waliokufa ni 134 ambao wamekuwa injured 129 tu, tukizipunguza hizi tukisema sasa tuweke shilingi elfu kumi, vijana watazidi kufanya zaidi na hapo lengo na madhumuni ana uwezo wa kulipa Shilingi elfu kumi. Kwa hiyo tu niseme hatufanyi hayo kwa ajili ya kuwakomoa, tunafanya ili watu wafuate.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa kuna utaratibu, nimekuwa nauona sana kule Zanzibar, vijana wanajazana kwenye magari makubwa yanaitwa mafuso, wanakwenda ufukweni huko muda wanaorudi huko wanarudi na bodaboda pikipiki hazipungui 30 au 40 njiani, lazima ajali inatokea, sasa kwa sababu analipa shilingi elfu kumi watafanya vyovyote kwa hiyo.

Mheshimiwa Spika, niseme kwamba tunayachukua mawazo tutakapo ona haja ya kufanya mabadiliko ya hii sheria tutafanya lakini kwa sasa naomba tuwe na hili.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO Aliuliza:- Jeshi la Polisi linashikilia pikipiki nyingi katika Vituo vya Polisi kwa muda mrefu. (a) Je, Serikali haioni fedha nyingi zinapotea kwa pikipiki nyingi kuchakaa zikiwa katika Vituo vya Polisi na hivyo kuleta hasara kwa Taifa? (b) Je, kwa nini Serikali isiunde Kamati Maalum kila baada ya miaka mitatu kupitia sababu zilizosababisha pikipiki hizo zishikiliwe kwa muda mrefu?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, swali langu lilikuwa linaendana na haya mahusiano kati ya bodaboda na Trafiki na kule Makete mahusiano ya bodaboda na traffic ni kama Refa ambaye yuko uwanjani ana kadi nyekundu tu, mahusiano yao ni mabaya sana kwa kiwango ambacho Traffic wanatoza faini ya shilingi laki mbili, tofauti na utaratibu wa kawaida. Tumejaribu kufanya vikao vya negotiation kati ya sisi na watu wa Trafiki lakini imeshindikana. Pili, Traffic wanafuata bodaboda wangu mashambani kule Matamba, kule Makete, kitu ambacho ni kunyume na utaratibu. Sasa je, Mheshimiwa Naibu Waziri anatupa kauli gani na maelekezo yapi kwa Trafiki Mkoa wa Njombe hususani Wilaya ya Makete dhidi ya vitendo viovu ambavyo vinafanywa na wao dhidi ya bodaboda wa Makete? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba sasa kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sanga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, utaratibu wetu kwenye PGO na utaratibu uliowekwa kwenye ile sheria au kanuni ya 168 ambayo imefanyiwa mabadiliko mwaka 2002, umesema ni Shilingi elfu thelathini, sasa kama kutatokezea askari au yoyote ambaye anayehusika na hili akawatoza watu zaidi ya kiwango kilichowekwa maana huyo anafanya kosa kwa mujibu wa taratibu kwa mujibu wa Sheria.

Mheshimiwa Spika, watu kuwafuata huko, unajua mtu anapokuwa mhalifu kwa mujibu wa utaratibu vyombo vinavyohusika kumkamata vina uwezo wa kumfuta popote alipo endapo amefanya makosa, lakini sasa hiyo namna ya kumfuata nayo ina utaratibu wake. Kwa hiyo, niseme tu kwamba, kama kutakuwa kuna askari amechukua zaidi ya hizo, maana huyo anavunja sheria, nadhani Mheshimiwa tushirikiane katika hili kuweza kuwakamata na kama tunawajua tuwalete katika ofisi yetu, tujue namna ya kuwashughulikia kwa mujibu wa taratibu. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO Aliuliza:- Jeshi la Polisi linashikilia pikipiki nyingi katika Vituo vya Polisi kwa muda mrefu. (a) Je, Serikali haioni fedha nyingi zinapotea kwa pikipiki nyingi kuchakaa zikiwa katika Vituo vya Polisi na hivyo kuleta hasara kwa Taifa? (b) Je, kwa nini Serikali isiunde Kamati Maalum kila baada ya miaka mitatu kupitia sababu zilizosababisha pikipiki hizo zishikiliwe kwa muda mrefu?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa ili tatizo la mlundikano wa pikipiki kwenye Vituo vya Polisi liko katika mikoa mingi, lakini utaona vijana wengi ambao wanakamatwa kuna wengine ambao hawana makosa yale ya kusema kwamba pikipiki ziwekwe kituoni. Hata hivyo, kuna wengine wameenda kukopa benki ili kama ni ajira kwa vijana, sasa wasema kwamba lazima miezi sita. Sasa ni kwa nini kusiwepo na kitengo maalum kwa sababu limeonekana hili ni tatizo karibu nchi nzima, cha kushughulikia hili tatizo la ukamataji wa bodaboda ili pengine kipindi kiwe kifupi miezi miwili au mitatu kwa sababu mengine ni makosa ambayo sio makubwa sana ya kuweka mpaka miezi sita na wengine wamepata ajali wamekufa na wengine wako hospitali? Ahsante.

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri sana yaliyotolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mheshimiwa almaarufu Chilo, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kabati, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kumekuwa na matukio ya mengi yanayotakana na namna ya uendeshaji wa biashara yenyewe ya bodaboda lakini pia industry nzima hiyo ukilinganisha na hatua zinazochukuliwa katika kupambana katika kuweka utaratibu wa kufuata sheria katika kufanya biashara yenyewe ifanyike lakini pia usalama wa watu.

Mheshimiwa Spika, moja kati ya vyombo vinavyotumika sana kwa sasa kufanya uhalifu ni pikipiki kuliko hata magari na kwa hivyo kumekuwa na sababu tofauti tofauti ambazo zinapelekea ukamataji na wenyewe kuwa mkubwa. Wengine wengi ni rahisi akienda kufanya tukio lenye thamani kubwa au akapora au akafanya nini kuitelekeza pikipiki ni jambo jepesi, kwa hiyo tunajikuta tuna pikipiki nyingi ziko mikononi mwa polisi, lakini wahusika ama hawajulikani walipo wamezitelekeza na ndio maana zinaitwa mali zilizookotwa.

Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba, kwa sababu concern ya Waheshimiwa Wabunge ni kubwa kwenye jambo hili na kwa sababu pengine sababu hizi tatu zilizotolewa katika jibu letu la msingi zinaonekana hazikuwatosheleza Waheshimiwa Wabunge, acha tukafanye tathmini ya kina na tutakuja na matokeo haya tueleze kwa kina katika pikipiki zilizokamatwa nchi nzima zilizopo kwenye Vituo vya Polisi ni ngapi; na ngapi zina tatizo gani na ngapi zina tatizo gani.

Mheshimiwa Spika, kwa hatua ya muuliza swali la msingi kwamba tuone utaratibu wa kuzi-dispose kwa sababu tumesimamisha uchumi na yenyewe ni hoja ambayo ni valid. Tutakachokifanya katika tathmini hiyo tutaona kama tutapata wale waliopo husika, ili tuweze kuzipiga mnada. Kwa hiyo, nadhani tupewe muda, twende tukafanye tathmini ya jambo hili na baadaye tutoe matokeo yake hadharani.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO Aliuliza:- Jeshi la Polisi linashikilia pikipiki nyingi katika Vituo vya Polisi kwa muda mrefu. (a) Je, Serikali haioni fedha nyingi zinapotea kwa pikipiki nyingi kuchakaa zikiwa katika Vituo vya Polisi na hivyo kuleta hasara kwa Taifa? (b) Je, kwa nini Serikali isiunde Kamati Maalum kila baada ya miaka mitatu kupitia sababu zilizosababisha pikipiki hizo zishikiliwe kwa muda mrefu?

Supplementary Question 4

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri na Waziri lakini tumeona kwamba pamoja na faini ya bodaboda kuwa kubwa, lakini bado matukio ya uhalifu yameongezeka kwa hiyo ni ishara kwamba faini haiwezi kuzuia uhalifu, lakini ukiangalia pia katika utaratibu wa kawaida sasa hivi tuna changamoto kubwa ya ajira katika nchi yetu na Serikali yetu imeahidi kutoa ajira milioni nane na miongoni mwa watu ambao wanajiajiri sehemu yao ni bodaboda.

Mheshimiwa Spika, nadhani ni vizuri sasa Wizara ya Mambo ya Ndani ikaleta utaratibu hapa ili tuweze kupitia upya mchakato wa faini hizi kwa sababu tunafahamu mtu leo ukiua una adhabu yake, lakini pia leo mtu ukiiba kuku una adhabu yake, haiwezekani gari ambalo ni milioni mia tatu faini yake elfu thelathini na pikipiki ya milioni mbili faini yake elfu thelathini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa tunasema elfu thelathini kama ni kosa ni moja, bodaboda anaweza kupigwa makosa manne kwa siku akalipa laki na ishirini na pikipiki ile sio ya kwake, inabidi pia apekeleke hela kwa mwenye pikipiki na yeye pia aweze ku-survive. Nadhani Serikali iwaangalie kwa jicho la huruma watu hawa wa bodaboda ili changamoto iweze kuondoka.

Mheshimiwa Spika, swali langu katika eneo hili tumeona watu wa traffic wamekuwa kwa kiwango kikubwa wanawakamata sana bodaboda pamoja na watu wa bajaji. Je, Wizara ya Mambo ya Ndani ina mpango gani wa kutoa maelekezo mahususi kwa watu wa traffic ili sio kila kosa analokamatwa nalo mtu lazima apigwe faini waweze kutoa onyo pamoja na utaratibu mwingine?

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. (Makofi)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kumekuwa kukijitokeza baadhi ya askari wetu kutokuwa waungwana. Unajua shughuli hizi huwezi ukazi-control kwa sheria per se a hundred percent. Kwa hiyo, hekima, busara na hasa unapokuwa mtumishi wa Umma unayewatumikia watu lazima utumie hekima na busara. Enforcement a hundred percent na yenyewe huwa kidogo ina shida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge, lakini pia na Waheshimiwa Wabunge mtusaidie, baadhi ya vijana wetu wanafanya kusudi na ninyi wenyewe mashuhuda, mnaendeshewa vibaya sana bodaboda hata hapa mjini, tukiacha hii hali na yenyewe ni shida pia. Mimi niseme tu, sote tutekeleze wajibu wetu na kwa upande wa askari polisi, hasa wa usalama barabarani wajitahidi kuwa wanatumia busara katika kuhakikisha kwamba wanasimamia sheria siyo kukomoa.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO Aliuliza:- Jeshi la Polisi linashikilia pikipiki nyingi katika Vituo vya Polisi kwa muda mrefu. (a) Je, Serikali haioni fedha nyingi zinapotea kwa pikipiki nyingi kuchakaa zikiwa katika Vituo vya Polisi na hivyo kuleta hasara kwa Taifa? (b) Je, kwa nini Serikali isiunde Kamati Maalum kila baada ya miaka mitatu kupitia sababu zilizosababisha pikipiki hizo zishikiliwe kwa muda mrefu?

Supplementary Question 5

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naona kijembe kimeingia sawasawa. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nami niwapongeze kwa sababu Simba Sports Club wameisadia Tanzania kuonekana vizuri. Pia ule utaratibu wa kuitangaza Tanzania, “Visit Tanzania”, kusema kweli ni jambo ambalo linafaa kuigwa hata na wenzetu wa Young Africans pindi watakapopata nafasi ya kuingia katika mashindano haya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu ni jepesi sana kuhusiana na bodaboda. Ni dhahiri kabisa biashara…

SPIKA: Mheshimiwa Mwigulu Nchemba, umesikia maoni ya Mheshimiwa; muige mambo mazuri tunayofanya. Mheshimiwa endelea. (Kicheko)

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, biashara ya bodaboda ni nzuri sana kwa vijana wetu. Pale Dar es Salaam bodaboda wanafanya vitu ambavyo vinasababisha abiria ambao ni raia wa Tanzania, ni very innocent, wapate ajali, kupoteza miguu, mikono na wengine maisha yao kwa kupita kwenye alama za taa nyekundu bila kujali, kupita no entry bila kujali, kupita katika barabara za mwendokasi bila kujali na mambo haya yanafanyika mbele ya askari wa usalama wa barabarani. Je, ni lini Serikali itasimamia kidete kuhakikisha kwamba biashara hii inaendeshwa kwa utaratibu wa kisheria ili kupunguza na kuondoa ajali ambazo zinawafika watu wetu?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba hawa madereva wa bodaboda kwa kweli ni shughuli kubwa kuwasimamia. Sheria hairuhusu ku-overtake kushoto lakini ukiangalia wote utadhani wana chuo walichojifunza ambapo wamefundishwa ku-overtake kushoto. Nafahamu kwa nini wanafanya hivyo; wanafanya hivyo kwa sababu ku-overtake kulia wanakuwa kati ya gari moja na nyingine, si salama zaidi kwao. Madereva wa magari mtu aki-overtake kushoto jicho lako linakuwa kulia zaidi, ni rahisi kama unakwenda kushoto ukaingia bila kutazama, ndiyo ajali nyingi zinatokea kwa sababu hiyo.

Mheshimiwa Spika, niseme tu, bado tuna kazi kubwa. Nami niwaagize tu Jeshi la Polisi Kitengo cha Traffic kuhakikisha kwamba madarasa yanafanyika ili kutoa elimu kwa sababu watu hawa tunawahitaji. Kuna graduates wanaendesha bodaboda, kuna watu wa masters wanaendesha bodaboda, kwa hiyo, siyo industry ya kuidharau, ni industry inayofanywa na watu wanapata riziki yao, lakini tuwaombe sana kwamba wazingatie sheria kwa sababu wanazifahamu lakini wanafanya kusudi. Jeshi la Polisi upande wa traffic wahakikishe wanatoa elimu kama tunavyofanya katika utoaji wa elimu ya usalama barabarani kwenye vituo vya bodaboda, wafundishwe namna ya kutumia chombo cha moto.

Mheshimiwa Spika, jambo hili nadhani liwe concern ya sisi sote kwa sababu kundi hili ni kubwa, askari wetu ni wachache, hawawezi wakafanya kwa kila mahali. Matajiri wa hizi bodaboda wako na humu ndani, kila mmoja akitekeleza wajibu wake tunaweza angalau kupunguza vifo vya hawa vijana, nguvu kazi kubwa ya Taifa inapotea. Ahsante sana.