Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE Aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga reli ya TAZARA kutokea Tunduma kwenda Kasanga ili kuwa na manufaa mapana ya kiuchumi na matumizi mazuri ya Bandari ya Kasanga na kuufungua Mkoa wa Rukwa kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa sababu, iko study ambayo ilifanyika enzi za mkoloni kwamba, kuna umuhimu wa kujenga reli kuanzia Tunduma kwenda Kasanga, lakini kwenda mpaka Ziwa Nyasa kwa maana ya Kyela na study hiyo iko NDC hadi leo ninavyoongea. Je, Serikali haioni umuhimu wa kufuatilia study hiyo ambayo ilifanywa na mkoloni na akaona viability ya mradi huo ili sasa ianze kutekeleza?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa, Mheshimiwa Rais ambaye wakati ule alikuwa Makamu wa Rais, wakati amekuja kuomba kura kwa ajili ya CCM, katika mahitaji ya wananchi wa Mkoa wa Rukwa ilikuwa ni pamoja na ujenzi wa kipande hicho cha reli na akasema amepokea na ambaye leo ndio ndio Rais; na kwa kuwa mahusiano yetu na Serikali ya China hayana shida hata kidogo na kwa sababu, wao ndio walitusaidia katika ujenzi wa Reli ya TAZARA. Je, Serikali haioni umuhimu uleule ili tutumie window ya uhusiano mzuri na China ili vipande hivi viweze kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, study aliyosema Mheshimiwa Mbunge ya mkoloni ni wazi kwamba haiwezi ikatumika kwa sasa. Kitakachofanyika inaweza kuwa tu ni kufanya review ya hiyo study kwa sababu, mazingira yamebadilika sana. Pia kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi ni kwamba, miradi hii ni miradi ambayo inahitaji fedha nyingi sana. Ikumbukwe tu kwamba, kwa sasa hivi kipaumbele cha Serikali ya Tanzania ni kujenga reli ya SGR Awamu ya Kwanza kutoka Dar-es-Salaam mpaka Mwanza ambayo nina hakika ikishakamilika tutakwenda na awamu nyingine. Kwa hiyo, kama Serikali hasa kwa kulingana na ufinyi wa bajeti, naamini hatuwezi kwenda na miradi yote miwili. Ndio maana nimesema upembuzi yakinifu utatuambia gharama ni kiasi gani, ili huo mradi uweze kuanza kutekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Kandege, Mbunge wa Kalambo ameeleza pia kwamba, Mheshimiwa Rais aliahidi kwamba, ujenzi huu uweze kufanyika wa reli na ilikuwa ni ahadi. Nakubaliana naye na hatusemi reli hii haihitajiki kujengwa. Tunachosema ni kwamba, tutakwenda kwa awamu na study ndio itakayotuambia gharama iliyopo, lakini pia itazingatia na vipaumbele vya Taifa, tuanze nini tumalizie na nini. Ahsante.

Name

Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE Aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga reli ya TAZARA kutokea Tunduma kwenda Kasanga ili kuwa na manufaa mapana ya kiuchumi na matumizi mazuri ya Bandari ya Kasanga na kuufungua Mkoa wa Rukwa kiuchumi?

Supplementary Question 2

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa umuhimu wa reli hii ya kutokea Tunduma kwenda Kasanga unafanana kabisa na umuhimu wa barabara inayoanzia Mwandiga na kuelekea Chankere na inayopita nyuma ya Hifadhi ya Gombe na mpaka kwenda kwenye Bandari ya Kagunga. Je, Serikali haioni kuna umuhimu sana wa kuikamilisha barabara hii haraka iwezekanavyo kwa sababu, barabara hii ni barabara kwanza ya kiuchumi, lakini barabara hii pia ni barabara ya kiulinzi kwa sababu, ukanda huu hatuwezi kuwafikia wananchi wetu pasipo kupita nchi jirani ya Burundi. Je, Serikali haiwezi kututoa kwenye utumwa huu wa kupitia nchi jirani kwenda kuwahudumia watu wetu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Makanika, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa barabara maana anayoongelea ni Barabara ya Mwandiga – Chankere hadi Kagunga. Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kusanifu barabara hiyo kwa sababu, barabara hiyo bado haijafunguliwa na tunajua kwamba, ni barabara muhimu sana kwenda Bandari ya Kasanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali inatambua umuhimu wa barabara hiyo kuwahudumia wananchi wa Kagunga. Mheshimiwa Makanika amekuwa anafuatilia sana hii barabara, nimhakikishie kwamba, Serikali inalifahamu na nadhani pia, ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwamba, hii barabara iweze kufunguliwa. Kwa hiyo, Serikali inatafuta fedha kuona kwamba, barabara hii inafunguliwa. Ahsante.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE Aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga reli ya TAZARA kutokea Tunduma kwenda Kasanga ili kuwa na manufaa mapana ya kiuchumi na matumizi mazuri ya Bandari ya Kasanga na kuufungua Mkoa wa Rukwa kiuchumi?

Supplementary Question 3

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya swali la nyongeza. Kwa kuwa, Serikali imejikita katika umaliziaji wa reli ya mwendokasi kwa jina lingine SGR kutoka Dar-es-Salaam awamu ya kwanza mpaka Morogoro na kutoka Morogoro mpaka Makutupora awamu ya pili; na kwa kuwa, TAZARA ni reli ya kimkakati na TAZARA inaanzia Mlimba inachepuka mpaka Kidatu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuendelea na hiyo reli mpaka Kilosa kuungana na hii reli ya mwendokasi, ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo kutoka reli ya kati na reli ya SGR kutoka Kilosa kuja Kidatu? Nashukuru.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Denis Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba, kuna umuhimu mkubwa sana wa kuunganisha reli ya SGR na reli ya TAZARA kuanzia Kilosa hadi Mikumi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Denis Londo kwamba, Serikali ina mpango huo wa kuziunganisha hizo reli, lakini upembuzi yakinifu utafanyika pale tu ambapo Serikali itakuwa imepata fedha, lakini tunaona kabisa ni muhimu kuziunganisha hizi reli kwa ajili ya ustawi wa uchumi wa nchi, lakini pia kuziunganisha hizi reli eneo la Kilosa na Mikumi. Ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE Aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga reli ya TAZARA kutokea Tunduma kwenda Kasanga ili kuwa na manufaa mapana ya kiuchumi na matumizi mazuri ya Bandari ya Kasanga na kuufungua Mkoa wa Rukwa kiuchumi?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Umuhimu wa reli ya kutoka Tunduma kwenda Kasanga ni sawa kabisa na umuhimu wa reli ambayo ilishakuwepo kabla ya Tanganyika kupata uhuru ya kutoka Mtwara – Nachingwea kwa Mikoa ya Kusini. Je, ni nini mpango wa Serikali wa kufufua reli ya Mtwara – Nachingwea mpaka Nyasa kwa manufaa ya kiuchumi na shughuli za kijamii kwa Mikoa ya Kusini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ali Kasinge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mbunge atakubaliana nami kwamba, Serikali ina mpango wa kujenga reli ya Mtwara hadi Mbamba Bay kwa kiwango cha SGR ambapo tayari upembuzi yakinifu umeshakamilika na usanifu wa awali umeshafanyika. Serikali imeshatafuta tayari transaction adviser kwa ajili ya kuandaa andiko ili kutafuta mbia ambapo reli hiyo tunategemea itajengwa kwa mfumo wa PPP. Kwa hiyo, itategemea na kama mbia huyo atapatikana haraka, basi hiyo reli itajengwa. Reli hiyo itahudumia corridor ya Mtwara kutoka Mtwara hadi Mbamba Bay, lakini pia itakuwa na branch kwenda Liganga na Mchuchuma kwa ajili ya kusafirisha madini ambayo tunategemea yatazalishwa katika migodi hiyo. Ahsante.