Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. REUBEN N. KWAGILWA Aliuliza:- Je, ni lini wananchi katika mitaa 30 isiyo na umeme Wilayani Handenni watapatiwa umeme kulipia mradi wa REA?

Supplementary Question 1

MHE. REUBEN N. KWAGILWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza ili yaweze kupata majibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kwa kuwa Wilaya ya Handeni ina majimbo mawili ya uchaguzi na mimi ni muwakilishi wa Jimbo la Handeni Mjini, je, Serikali haioni haja ya kuongeza wigo wa idadi ya viijiji ambavyo havijapata umeme upande wa Handeni Mjini hasa katika Kata ya Mlimani Konje, Kideleko kwa Magome, Kwenjugo, Kwadyamba, Malezi na Mabada?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kumekuwa na hali ya kukatika katika kwa umeme kila mara hali inayopelekea kuwapatia hasara wananchi kwa vyombo vyao vya umeme lakini vilevile kushindwa kufanya shughuli zao za kiuchumi za uzalishaji. Ni lini Serikali itakomesha tatizo hili wananchi wa Handeni Mjini washiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Reuben Mbunge wa Handeni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, awamu ya tatu, mzunguko wa pili wa REA unapeleka umeme katiika vijiji vyote Tanzania Bara ambavyo havikuwa na umeme ambavyo mpaka sasa havizidi 1974. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vijiji vyake vyote ambavyo havikuwa na umeme vitapata umeme katika awamu hii ya tatu, mzunguko wa pili ambayo imeanza tayari mwezi wa nne huu na itakamilika kufikia Desemba, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, hilo linaenda pia kwa Waheshimiwa Wabunge wengine wote wa Tanzania Bara, kwamba vijiji vyote ambavyo havikuwa vimepata umeme vimeingizwa katika awamu ya tatu, mzunguko wa pili na tutahakikisha tunapeleka umeme katika maeneo yote hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali la pili, ni kweli, Tanga kama Mkoa na Handeni ikiwemo imekuwa na matatizo ya kukatika kwa umeme ikiwemo Mikoa wa Mbeya Pamoja na Mkoa wa Kagera. Hata hivyo Wizara kwa kushirikiana na TANESCO imechukua juhudi mbalimbali kuhakikisha inamaliza tatizo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwa Mkoa wa Tanga na hasa Handeni tatizo kubwa lilikuwa ni miundombinu chakavu ambayo ilikuwa inapelekea umeme katika maeneo hayo; na hivyo yamefanyika mambo mawili moja ni la sasa na lingine ni la muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, umeme unaokwenda Handeni unatokea katika kituo chetu cha Chalinze unakwenda kwenye substation ya Kasija, unatoka Kasija unakwenda Korogwe – Handeni – Kilindi, na njia ndefu sana ina km. zaidi ya 500. Kwa hiyo, tumebaini kuna nguzo zaidi ya 1300 ambazo zilikuwa zimeoza zimeanza kufanyiwa marekebisho na kuondolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka tunavyoongea sasa tayari nguzo zaidi ya 500 zimerekebishwa, na tumehakikisha kwamba kufikia mwishoni mwa mwezi wa nne, nguzo zote 1300 zitakuwa zimerekebishwa na kuhakikisha kwamba basi umeme haukatiki hovyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika hatua ya pili ambayo ni ya kudumu na ya muda mrefu tumeshauriana na kukubaliana na wataalam, tumekubaliana tujenge kituo kidogo cha kupoza umeme pale Handeni. Kwa hiyo tutatoa umeme Kasija kwenye kituo cha kupoza umeme cha sasa tutapeleka Handeni, km. 81 kwa gharama ya shilingi bilioni 4nne. Tukishajenga kituo hicho cha kupoza umeme pale Handeni basi tutatoa line moja ya kuhudumia Handeni, tunatoa line moja kwenda Kilindi na line nyingine moja itaenda kwenye machimbo ambayo tumeambiwa itaanzishwa siku si nyingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kufanya hivyo tunahakikisha kwamba basi tatizo la kukatika umeme Wilaya yetu ya Handeni na majimbo yote mawili litakuwa limefikia ukomo na tutakuwa tuna uhakika wa umeme.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri hapo umetoa maelezo marefu na mimi ninakupongeza sana. Sasa hapo umeitaja Mbeya halafu kule hujaeleza tatizo ni nini, maana huko kwingine umesema ni nguzo haya Mbeya unakatika katika kwa nini?

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nilipoitaja Mbeya nikaitaja Kagera kwasababu na mimi natokea Kagera ili utakaponipa nafasi ya kuzungumzia Mbeya basi na Kagera nipitie humo humo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mbeya tunayo matatizo makubwa mawili, tatizo moja kubwa ni radi ambazo zimekuwa zikisumbua mifumo yetu ya umeme kwenye transfoma. Tatizo hilo pia liko Mkoa wa Kagera. Tulichokifanya katika mikoa hii miwili tumeanza kufunga vifaa vinaitwa auto recloser circuit breaker ambayo vinazuia radi isirudi kwenye maeneo mengine ambayo hayajaathirika hilo ni tatizo moja kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia tatizo la pili lilikuwa ni uchakavu wa miundombinu kwenye maeneo hayo. Tumeunda vikosi kazi maalum katika mikoa hiyo mitatu, Mbeya, Tanga na Kagera ya kuhakikisha kwamba kinapitia kila eneo na kubaini tatizo kubwa ni nini ili iiweze kurekebisha. Vikosi kazi hivyo viko kazini, vinafanya kazi; na tunahakikisha kufikia mwezi wa sita, maeneo yote ambayo yalikuwa yana matatizo sugu yatakuwa yamefanyiwa kazi na kurekebishwa.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. REUBEN N. KWAGILWA Aliuliza:- Je, ni lini wananchi katika mitaa 30 isiyo na umeme Wilayani Handenni watapatiwa umeme kulipia mradi wa REA?

Supplementary Question 2

MHE. RASHIDA A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Matatizo ya usambazaji wa umeme vijijini yaliyopo Handeni ni sawa kabisa na yaliyopo kule Lushoto katika Jimbo la Mlalo. Hivi ninavyozungumza tunapoelekea kwenye robo ya tatu ya mwaka wa fedha ambao unakaribia kwisha hakuna hata kijiji kimoja ambacho REA wamesambaza umeme. Sasa tunataka kujua, wananchi wa Lushoto hususan Jimbo la Mlalo wameikosea nini hii Serikali hii ya Awamu ya Tano?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shangazi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Soika, kama nilivyotangulia kujibu kwenye swali la msingi. Maendeleo ni hatua, na tulianza na vijiji vichache na tunazidi kuongeza, na katika awamu ya tatu mzunguko wa pili wa REA vijiji vyote ambavyo vilikuwa havijapata umeme vitapatiwa umeme.

Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Shangazi kwamba kabla ya mwaka 2022 Disemba vijiji vyote vya kwenye Jimbo lake la Lushoto viitakuwa vimepatiwa umeme kama nilivyotoa majibu kwenye swali la msingi.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. REUBEN N. KWAGILWA Aliuliza:- Je, ni lini wananchi katika mitaa 30 isiyo na umeme Wilayani Handenni watapatiwa umeme kulipia mradi wa REA?

Supplementary Question 3

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana Mheshimiwa Waziri wa Nishati alikuja Musoma, na ninamshukuru kwamba tulienda naye pale kwenye Kata ya Bweli, Mtaa wa Bukoba tukaweza kuwasha umeme, na baada ya hapo tukaenda kwenye mkutano wa hadhara akaahidi kwamba sasa maeneo yote ya Musoma Mjini wataweza kupata umeme kwa gharama ya 27,000.

Hata hivyo, kila wananchi walipojaribu kwenda kulipia wanaambiwa mpaka waraka utoke kwa sababu haujapatikana. Sasa napenda kujua ni lini Mheshimiwa Waziri wa Nishati atatoa waraka ili wale wananchi wangu wa Jimbo la Musoma waweze kupata umeme kwa gharama nafuu?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Manyinyi, Mbunge wa Musoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakiri kabisa kwamba maelekezo ya Mheshimiwa Waziri yaliyotolewa yanatakiwa kuzingatia na kusimamiwa kama ilivyo na kwa kuwa tumesikia kuna lalamiko la namna hiyo, naomba tulichukue na tutahakikisha kwamba maelekezo ya Mheshimiwa Waziri yanafanyiwa kazi kama ilivyoelekezwa, hakuna kupindisha maelekezo yaliyotolewa.

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. REUBEN N. KWAGILWA Aliuliza:- Je, ni lini wananchi katika mitaa 30 isiyo na umeme Wilayani Handenni watapatiwa umeme kulipia mradi wa REA?

Supplementary Question 4

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa changamoto ya umeme wa Jimbo la Handeni inafanana kabisa na Jimbo la Arusha Mjini, napenda kuuliza maswali ya nyongeza yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kwamba Jiji la Arusha ni jiji la kitalii, lakini bado kuna kata ambazo zinachangamoto kubwa sana ya umeme Kata kama za Telati, Kata ya Olasiti, Olmoti, Moshono, Mulieti kule maeneo ya Losoito, Sokoni 1 na Sinoni. Ningependa kufahamu, je, Wizara ina mpango gani kupitia Mradi wa Peri-urban ili kuhakikisha kwamba wananchi hawa ambao wapo kwenye Jiji la Kimataifa, Jiji la Utalii wanaondokana na changamoto ya umeme katika jimbo letu?

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili….

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa moja tu, hilo ni la nyongeza.

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gambo, Mbunge wa Arusha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inapeleka umeme katika maeneo mbalimbali kwa programmes tofauti. Ziko awamu za REA ambazo zimeendelea, ziko programme ya densification, lakini ipo programu peri-urban ambayo inapeleka umeme kwenye maeneo ambayo yana asili ya ukijiji lakini yako mjini. Mkoa wa Arusha tayari umeshanufaika na awamu ya kwanza ya densification, peri-urban kupeleka umeme katika baadhi ya maeneo na iko awamu ya pili ya peri-urban ambayo itakuja, inaanza mwezi wa Saba.

Katika maeneo ambayo hayajapata Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Mbeya, Mwanza na Tanga yatapelekewa umeme katika Mradi huo wa pili wa peri-urban. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba awamu hiyo ya pili ikianza basi na yeye maeneo yake yatapatiwa umeme katika awamu hiyo.