Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka maji safi na salama Butiama ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa Baba wa Taifa katika Taifa letu?

Supplementary Question 1

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa ajili ya nafasi hii ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri kwamba, hayaleti matumaini ya moja kwa moja kwa wakazi wa Butiama naomba nijielekeze kwenye maswali kama ifuatavyo; Swali la kwanza; kwa kuwa, miradi hii ambayo Mheshimiwa Waziri ameitaja hapa utekelezaji wake umekuwa ni wa kusuasua sana kwa lugha nyingine umekuwa na mwendo wa kinyonga. Je, nini kauli ya Serikali basi kuhusiana na bili zinazotolewa kwa wakazi wa Butiama bila kupatiwa huduma?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa, kauli mbiu ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kumtua mwanamke ndoo kichwani. Swali langu ni kwamba, ni lini basi Serikali itatekeleza kauli mbiu hii kwa matendo kukamilisha miradi yote ya Serikali nchi nzima ambayo imeonekana kusuasua mpaka sasa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba majibu kutoka kwa Mheshimiwa Waziri.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na masuala ya bills, maeneo mengi yalikuwa na tatizo hili, lakini tayari Wizara tunashughulikia kwa karibu kuona kwamba, mtu anakwenda kulipa bili kulingana na matumizi yake. Tunaendelea kuweka mbinu mbalimbali kama kumhusisha moja kwa moja mtumiaji maji kwa kushirikiana na msomaji mita wataangalia kwa Pamoja, watasaini kadi na hapo sasa yule mlipaji atakwenda kulipa bili kulingana na matumizi yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na kumtua mwanamke ndoo kichwani; hili suala sasa hivi ni tayari linatekelezeka. Maeneo mengi ya Tanzania sasa hivi akinamama wameshakiri hawabebi tena maji vichwani na tayari Wizara tunaendelea kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha maeneo yote ya pembezoni mwa miji kwa maana ya vijijini nao wanakwenda kukamilika katika mpango huu na kazi zinaendelea. Tayari tuna ari kubwa sana kama Wizara na watendaji wetu wametuelewa mwendo wetu ni mwendo wa kasi ya mwanga. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka maji safi na salama Butiama ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa Baba wa Taifa katika Taifa letu?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. changamoto za maji ambazo wanakumbana nazo wananchi wa Butiama zinafanana sana na changamoto zinazowakuta wananchi wa Wilaya ya Nkasi. Natambua kwamba, Serikali imekuwa inapeleka fedha katika miradi mbalimbali katika Wilaya ya Nkasi ambayo haijaweza kumaliza changamoto za maji. Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka wa kutumia chanzo cha Ziwa Tanganyika ambacho ni chanzo cha uhakika ili kuweza kumaliza changamoto za maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza kutoka kwa Mbunge wa Nkasi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Maji tayari tuna mikakati kabambe ya kuweza kutumia mito, maziwa na vyanzo vyote vya maji pamoja na Ziwa Tanganyika. Kwa hiyo, kufikia mwaka ujao wa fedha Serikali tunaendelea kuona namna bora ya kuweza kutumia Ziwa Tanganyika kutatua tatizo la maji eneo la Nkasi.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka maji safi na salama Butiama ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa Baba wa Taifa katika Taifa letu?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. pamoja na majibu mazuri na maelezo mazuri ni ukweli usiopingika kwamba, tatizo la maji katika nchi yetu ni tatizo kubwa na kama ambavyo Mheshimiwa Aida amesema kuhusiana na matumizi ya Ziwa Tanganyika. Je, sio wakati sahihi kwa Serikali kuhakikisha kwamba, Mkoa wote wa Rukwa, Mkoa wa Katavi na Mkoa wa Songwe unaanza kutumia chanzo cha uhakika cha Ziwa Tanganyika, ili kupata maji maeneo yote? Kwani imethibitika kabisa matumizi ya maji kutoka Ziwa Victoria yamekuwa ni ufumbuzi mkubwa katika maeneo mengi, sasa si wakati muafaka kwa hiyo mikoa niliyoitaja kutumia chanzo hicho? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Kandege, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu awali, tayari Wizara tuna mikakati ya kuona maziwa yote ambayo yanapatikana katika nchi yetu tunakwenda kuyatumia kikamilifu katika kutatua tatizo kubwa la maji katika mikoa inayohusika. Hivyo mikoa yote ambayo inapitiwa na ziwa hili tutakwenda kuifanyia kazi na hakuna mkoa utakaorukwa, tutagawa maji kulingana na bomba litakavyopita kadiri mradi utakavyosanifiwa, ahsante.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka maji safi na salama Butiama ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa Baba wa Taifa katika Taifa letu?

Supplementary Question 4

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Naitwa Eng. Samweli Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la maji lililopo Butiama lipo pia kwenye Mji wa Katesh kwenye Jimbo langu; na kwa kuwa Serikali imeshawekeza shilingi bilioni 2.5 kuleta maji mjini na maji yale sasa yapo tayari kutumika. Je, Wizara iko tayari kuongeza fedha kidogo ili maji yaweze kusambazwa kwa wananchi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuongeza fedha katika miradi ambayo ipo katika hatua za utekelezaji ni jukumu la Wizara. Hivyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge fedha zitakuja kwa awamu kama ambavyo imekuwa kawaida yetu kuhakikisha mradi huu unafikia lengo la kupata maji bombani. Lengo la Wizara siyo tu kujenga hizo structures ambazo zipo tayari, tutaleta fedha kuhakikisha maji sasa yanafika bombani.