Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Moja ya njia ya kuimarisha uchumi ni kupunguza uagizaji wa bidhaa nje ya nchi, Taifa linatumia fedha nyingi za kigeni kuingiza mafuta ya kula wakati kuna vyanzo vingi vya mafuta kama vile alizeti - Singida na Michikichi – Kigoma. Je, ni lini Serikali itaweka msukumo kwa mazao haya katika mikoa hii kwa faida ya nchi na wakazi wa mikoa hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa kutoka Benki Kuu inaonesha kwamba kuanzia mwaka 2006 mpaka 2015 takribani miaka kumi kila mwaka nchi imekuwa ikitumia gharama ya takribani wastani wa dola milioni 900 ambayo ni sawa sawa na shilingi trilioni mbili katika fedha hizi zinatumika kwa ajili ya kununulia bidhaa kutoka nje. Katika fedha hizi, fedha dola milioni 120…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Jesca uliza swali.
MHE. JESCA D. KISHOA: Nauliza swali Mheshimiwa Mwenyekiti, dola milioni 120 zinatumika kununulia mafuta ambayo ni sawa na takribani shilingi bilioni 250.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali iliyoko madarakani itawakumbuka wananchi wa Singida ambao wamepuuzwa wametelekezwa, lakini wamesahaulika hata katika hili la mafuta? Ninaomba Waziri aje anipe majibu.
MHE. JESCA D. KISHOA: Ni lini bodi itaundwa kwa ajili ya mafuta?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitambue umuhimu wa maswali haya kwa logic, kwa maana ya kwamba Wizara na Serikali, tukishirikiana na Wizara ya Viwanda, tumedhamiria kwa dhati kabisa kuhakikisha kwamba tunajitegemea kwenye sekta hii ya mafuta.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari Mheshimiwa Mwijage, ameshazindua mkakati ambao utatuondoa katika tatizo hilo. Mheshimiwa Jesca mdogo wangu ambaye tuligombea naye Jimbo moja, wananchi wa Mkoa wa Singida hawajapuuzwa, isipokuwa tunalotaka kufanya kama Serikali na Wabunge wote wanaotokea mikoa hii tuwahamasishe na sisi tulisema kwenye hotuba yetu kila familia iwe angalau na ekari moja ya alizeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Kigoma na Mheshimiwa Jesca amewagusa watu wake wote, kaanzia Singida kwa wazazi wake halafu kaenda swali la michikichi kwa wakwe zake alipoolewa kule na Mheshimiwa Kafulila. Tuwahamasishe, hamasa hii ambayo inatoka kwenye alizeti ambayo Mheshimiwa Allan Kiula, Mheshimiwa Kingu na Mheshimiwa Mlata na Aisharose wanafanya pamoja na akina Mheshimiwa Nkamia na Mheshimiwa Ashatu, tuhamasishe walime alizeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kule Kigoma, kama Mheshimiwa Naibu Waziri alivyojibu ya michikichi 137 kwa kila ekari tuwahamasishe walime, baada ya hapo hatua zitakazofuata za Serikali zitakuwa zile za kisera za kuhakikisha kwamba tuna-discourage mafuta kutoka nje na yatumike yale yanayotoka ndani. Tukianza kwanza kwa ku-discourage mafuta ya nje kabla hatujahamasisha watu kulima kitakachofuata bei zitapanda na watu watakosa hiyo bidhaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili linalohusu bodi na lenyewe sasa hivi alizeti itakuwepo kwenye Bodi ya Mazao Mchanganyiko kwa sababu uzalishaji wake haujawa mkubwa, wananchi hawa tusije tukawawekea mzigo ambao wamekuwa wakibeba wengine kwa ajili ya kuhudumia bodi hizi ile hali wao hawajajitosheleza na kuvutiwa zaidi kwa ajili ya zao hilo.

Name

Suleiman Masoud Nchambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Moja ya njia ya kuimarisha uchumi ni kupunguza uagizaji wa bidhaa nje ya nchi, Taifa linatumia fedha nyingi za kigeni kuingiza mafuta ya kula wakati kuna vyanzo vingi vya mafuta kama vile alizeti - Singida na Michikichi – Kigoma. Je, ni lini Serikali itaweka msukumo kwa mazao haya katika mikoa hii kwa faida ya nchi na wakazi wa mikoa hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Namuomba sasa Mheshimiwa Mwiguli na Naibu wake Mawaziri hawa shapu wanaofanya mambo kwa ushapu watumie neema hiyo kwa kutengeneza mabwawa kwa ajili ya umwagiliaji wa mazao ambayo yatawakomboa wana Kishapu.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunalipokea wazo la Mbunge shapu wa Jimbo shapu la Kishapu, ambaye kwa kweli kwa ushapu wake ndiyo maana amekuwa akichaguliwa. Tayari tumeshaandika barua kwa Waziri pacha ambaye kwa leo yupo na heshima kubwa.
Kwa hiyo tutatengeneza hilo ili tuweze kutumia mabwawa hayo.