Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA Aliuliza:- Ni Halmashauri ngapi nchi zimetekeleza kwa asilimia 100 sheria ya utoaji mikopo asilimia 10 ya makusanyo ya ndani kwa makundi ya vijana, akinamama na watu wenye mahitaji maalum?

Supplementary Question 1

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali tayari Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba halimashauri 85 hazijaweza kutekeleza kwa asilimia mia moja utoaji wa mikopo. Je, Serikali haioni sasa ni wakati wa kuanzishwa kwa benki ya vijana ili iweze kusimamiwa na vijana wenyewe?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Serikali ina mpango gani juu ya kuwakopesha vijana mmoja mmoja kwa sababu vijana wengi wanaopewa mikopo hii haiendi kuwanufaisha kwa kuwa mawazo yanakuwa tofauti? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asia Abdukarim Halamga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tumeona tangu kuanzishwa kwa mpango huu wa mikopo asilimia kumi kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kazi ya ukopeshaji katika ngazi ya halmashauri katika miaka mitatu iliyopita imeongezeka zaidi ya mara tatu. Kwa hivyo, kwa hatua hii bado Serikali inaendelea kutekeleza vizuri, lakini ni kweli kwamba bado kuna changamoto kwenye baadhi ya halmashauri kutokana na uwezo wa ukusanyaji wa mapato na ndiyo maana Serikali imeendelea kusisitiza halmashauri kuboresha vyanzo vya mapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na wazo la Mheshimiwa Mbunge kuanzisha benki ya vijana, naomba tulichukue kama Serikali, tukalifanyie tathmini na kuona njia bora zaidi ya kulitekeleza. Kuhusiana na mikopo ya vijana kwa maana kijana mmoja mmoja, pia ni wazo la Mheshimiwa Mbunge na sisi ni kazi yetu kuchukua mawazo ya Waheshimiwa Wabunge, kuyatathmini, kuyafanyia kazi na kuona uwezekano wa kutekeleza hilo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inapokea mawazo hayo na tutakwenda kuyafanyia kazi na kuona njia bora zaidi ya kuyatekeleza.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA Aliuliza:- Ni Halmashauri ngapi nchi zimetekeleza kwa asilimia 100 sheria ya utoaji mikopo asilimia 10 ya makusanyo ya ndani kwa makundi ya vijana, akinamama na watu wenye mahitaji maalum?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Nina swali moja la nyongeza; katika halmashauri zetu zipo SACCOS za vijana na wanawake ambazo zimeundwa na wanawake na vijana, lakini SACCOS hizo hazikopeshwi kupitia Mifuko ya Halmashauri. Sasa, ni lini Serikali italeta sheria Bungeni ili SACCOS hizo za vijana na wanawake ziweze kukopesheka kupitia Mfuko wa Halmashauri?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika naomba kujibu mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika kuhusiana na SACCOS za vijana na wanawake kutokopesha kupitia halmashauri na wazo lake ni lini Serikali italeta sheria ili utaratibu huu uweze kutendeka, naomba nichukue wazo la Mheshimiwa Mbunge, tukalifanyie tathmini kama Serikali na kuona uwezekano wa kutekeleza jambo hili na kuona faida zake na changamoto zake ili tuweze kufanya maamuzi stahiki.