Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE Aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Masasi – Nachingwea kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali yetu yenye kutia matumaini lakini bado kwa umuhimu wa barabara hii wananchi wa Jimbo la Nachingwea watapenda kusikia commitment ya Serikali. Kwa kweli, katika hili viongozi wengi wanahukumiwa kutokana na barabara hizi pamoja na mambo mengine. Je, nini commitment ya Serikali juu ya kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, viko vijiji vya Ikungu, Chiola kuelekea Ruangwa, hapa tayari walifanyiwa tathmini na wenzetu wa TANROADS. Watu wa TANROADS walikuja wakafanya tathmini wakiamini kwamba barabara itapita upande wa kulia baada ya muda wakarudi tena wakafanya tathmini upande wa kushoto. Kwa hiyo, hawa wananchi wamezuiliwa kwenye maeneo yale wasifanye maendelezo. Ni lini Serikali itakwenda kutoa ufafanuzi wa jambo hili, ili wananchi wa maeneo yale waweze kuendelea na shughuli zao? Ahsante sana.

SPIKA: Hiyo ni kwa barabara ya Nachingwea – Ruangwa?

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, ndiyo.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Chinguile, Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, commitment ya Serikali ni kwamba tayari fedha ya awali za kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami zimeshatengwa. Pia barabara hii imeahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na pia ni kati ya barabara ambayo Mheshimiwa Rais ameahidi kuijenga kwa kiwango cha lami katika kipindi hiki cha miaka mitano.

Mheshimiwa Spika, swali la pili ambalo ameuliza kwamba kuna wananchi ambao wameshindwa kuendeleza maeneo yao kwa sababu ya watu wa TANROADS waliokwenda kupima, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Nachingwea kwamba suala hili linaendelea kufanyiwa kazi. Naomba kama kuna changamoto yoyote tofauti ambayo pengine mimi nitakuwa siifahamu basi tuwasiliane naye ili niweze kujua changamoto halisi ni ipi.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE Aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Masasi – Nachingwea kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sambamba na barabara ya Masasi – Nachingwea, barabara hii vilevile ina jina la Lukuledi
– Liwale yenye jumla ya kilometa 175 kwa maana kutoka Masasi mpaka Liwale kilometa 175. Barabara hii tayari imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Wanaliwale wanataka kusikia barabara Nachingwea – Liwale lini itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja kama nilivyosema tunatambua ni muhimu na zimeahidiwa kujengwa katika bajeti ambayo tutaanza kuijadili. Kwanza ni barabara ambayo ipo kwenye Mpango wa Miaka Mitano na tunategemea katika bajeti inayoanza itatengewa fedha ili ianze kujengwa.

Mheshimiwa Spika, ahsante.