Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa maji kwenye Vijiji vya Engutukoiti, Losineni, Juu, Losineni kati, Oldonyawasi, Lemanda, Lemengrass, Oldonyosambu, Likurat, Olkeejulbendet, Lenigjape, Olkokula, Lemanyati, Lenjani, Seuri, Ekenywa na Ngaramtoni na Kata za Kimyak, Sambasha Tarakwa, Oloirien, Kiranyi, Likidingla, Sokon II, Olturito, Bangata, Mlanganini, Nduruma, Bwawani, Oljoro na Lahni Musa, Kisango, Mwandet Wilayani Arumeru?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri , lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali ina nia njema ya kutoa huduma ya maji, kulikuwa na miradi ya mwaka 2009 miradi ya Likamba, Musa, Nengu, Olotushura na Loskito, je, ni lini sasa Serikali itakamilisha miradi hiyo ya muda mrefu?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa kulikuwa na ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Maji katika kukarabati Mradi wa Ilmuro inayohudumia Kata za Oljoro na Laroy. Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha ahadi hiyo ya Mheshimiwa Waziri? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Lemburis Saputu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mradi huu ambao ulianza kutekelezwa mwaka 2009, nipende tu kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge miradi hii tunakuja kuitekeleza na nimeshafika eneo lake. Nimwahidi namna ambavyo tuliongea pale site tutakuja kufanyia kazi haraka iwezekanavyo na pamoja na hii ahadi ya Mheshimiwa Waziri aliyepita, ukarabati wa Mradi huo wa Ilmuro pia unakuja kufanyiwa kazi hivi karibuni. Fedha tayari zipo na mgao unaofuata na mgao unaofuata na Mheshimiwa Mbunge yupo na atakwenda kutekelezewa mradi huo.