Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA Aliuliza:- Je, ni lini mradi wa kusambaza maji Mji wa Njombe kutoka Mto Hagafilo utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa mradi huu kama alivyosema yeye mwenyewe utachukua miezi 24, miaka miwili na wananchi wa Njombe wakati huo wataendelea kupata tabu na kuteseka hasa wakati wa kiangazi maji yanapopotea kabisa. Je, Serikali itakuwa tayari kutekeleza miradi mingine midogo midogo ambayo baadhi imekwishabuniwa na inafahamika na mingine inaweza kubuniwa, kwa vile Njombe tumezungukwa na mito kila upande?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Serikali ilishatekeleza mradi mdogo katika Mji wa Kibena pale Njombe, kwa kupeleka maji mpaka Hospitali ya Wilaya ya Njombe na kuna tanki kubwa sana wamelijenga pale na tanki hilo lina maji mengi na saa nyingine yanabubujika na kumwagika. Kwa bahati mbaya wananchi wa eneo la Kibena ambao wanaishi maeneo yale bado hawana. Je, Serikali haioni kama itakuwa ni busara na jambo jema badala ya maji yale kuwa yanabubujika na kumwagika sasa wakatoa pesa na kuweka mradi mdogo wa kutawanya maji ili wananchi wa Kibena wapate kuwa na maji ya uhakika? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba nijibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwanyika kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa suala la hofu kwa sababu mradi utaanza mwezi Aprili na yeye anapenda visima ama miradi midogo midogo, nipende tu kumwambia kwamba tayari Wizara inafanya mchakato huo na hili linashughulikiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na mradi ambao unapeleka maji kwenye hospitali ya Kibena pale kwa kuhitaji distribution tayari Wizara imetoa maelekezo kwa mameneja walioko pale wanafanyia upembuzi yakinifu ili kuona namna gani kama distribution itawezekana. Naomba kukupa amani Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi huu ambao tunauanza mwezi Aprili, tutaenda kuufanya kwa kasi nzuri na tutaweza kutawanya maji kadri mradi unavyokamilika hatutasubiri mradi ukamilike mpaka mwisho, ukifika hata asilimia 40 wale ambao wanapitiwa na lile eneo ambalo miundombinu imekamilika maji yataweza kutoka. (Makofi)

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA Aliuliza:- Je, ni lini mradi wa kusambaza maji Mji wa Njombe kutoka Mto Hagafilo utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kwanza napenda kupongeza Wizara ya Maji, Mheshimiwa Waziri Aweso na Mheshimiwa Engineer Maryprisca ya kutembelea Mikoa yetu ya Kusini, Mbeya, Songwe, Rukwa, Katavi na Njombe, kazi nimeiona, mmefanya kazi nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu moja la nyongeza, pale Mkwajuni Makao Mkuu ya Wilaya pana mradi mkubwa wa maji wa milioni 760 toka mwaka 2018. Mkandarasi ametumia fedha zake binafsi karibuni asilimia 80 anakamilisha mradi, lakini anakwamishwa na malipo ya Serikali baada ya kumaliza zile kazi, certificate anapeleka lakini halipwi. Galula pana mradi wa maji, Kapalala pana mradi wa maji. Hii miradi mitatu kwenye jimbo langu imekuwa ni kero sana kwa wananchi na wale wakandarasi wameshamaliza lakini wanasubiri certificate ili waweze kulipwa. Je, ni lini Serikali itawalipa fedha zao ili miradi ya maji ikamilike?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, malipo yote ambayo wakandarasi wamefanya kazi na kazi zinaonekana malipo yote yanaendelea kushughulikiwa na hivi karibuni Serikali itawalipa.