Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Kituo cha Afya cha Kirando katika Wilaya ya Nkasi kinatoa huduma kwa vijiji zaidi ya ishirini katika mwambao wa Ziwa Tanganyika na katika kituo hicho wodi za watoto na akina mama zimekuwa ni ndogo sana ikilinganishwa na idadi ya watoto na akina mama wanaohudumiwa katika kituo hicho. Je, ni lini Serikali itajenga wodi hizo ili kuondoa kero kwa akina mama na watoto wanaohudumiwa katika kituo hicho?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa tatizo hili limeikumba pia hospitali ya Namanyele - Nkasi Kusini na kwa bahati nzuri Serikali imejenga majengo ya wodi. Je, ni lini sasa Serikali itakabidhi na kufungua majengo haya?
Swali la pili, azma ya Serikali ni kuwa kila kata kuwa na kituo cha afya na kila kijiji kuwa na zahanati, je, ni lini vijiji hivi vinavyotegemea hospitali ya Kirando vitapatiwa zahanati?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipende kushukuru kama facilities zimekamilika, sasa bado kuweza kufunguliwa nadhani kikubwa zaidi tutawasiliana na uongozi wa mkoa kuangalia utaratibu tukishirikiana na wenzetu wa Wizara ya Afya, vifaa hivyo vikishakamilika basi hospitali hiyo iweze kufunguliwa. Hilo ni jambo ambalo tunasema kama Serikali tunalichukua kwa ajili ya kwenda kulifanyia kazi ili wananchi waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ajenda ya pili ni jinsi mchakato wa ujenzi wa vituo vya afya ya zahanati ni kweli sasa hivi tuna karibuni ya kata 3390, lakini vituo vya afya tulivyonavyo ni vituo 484 maana yake tuna gap kubwa sana ya kufanya. Ndiyo maana leo hii Waziri wa Afya ata-table bajeti yake hapa ikionyesha mikakati mipana kwa ajili ya kufikia maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukijua wazi kwamba katika hao wenzetu wa eneo hili wanachagamoto kubwa sana na nikifanya rejea ya Mheshimiwa Keissy hapa alishasema mara nyingi sana. Hiki hasa kituo chako cha Kirando na yeye alikuwa akiomba ikiwezekana iwe Hospitali ya Wilaya kwa mtazamo wake. Lakini alikuwa akifanya hivi ni kwa sababu wenzetu wa kule wa pembezoni wakati mwingine wanapata wagonjwa wengine mpaka kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Congo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo Serikali naomba tuseme wazi kwamba tutashirikiana vya kutosha na mimi naomba nikiri kwamba katika maeneo yangu ya mchakato wa kuanza kutembelea nina mpango baada ya Bunge hili la Bajeti kutembelea katika mkoa huu ili kuangalia changamoto zinazowakabili ili kwa pamoja tuweze kuzitatua tukiwa katika ground pale tuone ni lipi linalowakabili wananchi wetu.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Kituo cha Afya cha Kirando katika Wilaya ya Nkasi kinatoa huduma kwa vijiji zaidi ya ishirini katika mwambao wa Ziwa Tanganyika na katika kituo hicho wodi za watoto na akina mama zimekuwa ni ndogo sana ikilinganishwa na idadi ya watoto na akina mama wanaohudumiwa katika kituo hicho. Je, ni lini Serikali itajenga wodi hizo ili kuondoa kero kwa akina mama na watoto wanaohudumiwa katika kituo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru naitwa Bobali, Mbunge wa Mchinga.
Kwa kuwa matatizo yaliyopo katika Mkoa wa Katavi yanafanana kabisa na matatizo ya kituo cha afya ya Chalutamba katika Jimbo la Mchinga kumekuwa na kuharibika mara kwa mara kwa gari ya kituo kile.
Je, Wizara haioni kwamba kuna haja sasa ya yale magari yaliyochakaa kuya-compensate katika vituo vyote ambavyo vina magari yaliyochakaa wakapewa magari mapya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumelisikia suala la Mheshimiwa Bobali, lakini mimi nikijua kwamba hapa tulivyokuwa tunapitisha bajeti tuliona vipaumbele vya kila Halmashauri, wengine walitenga gari, wengine wakatenga vituo vya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwa sababu yale magari yamechakaa lakini nadhani tutaangalia jambo kubwa ni kwamba kama Halmashauri tunapokaa katika priority zake katika mpango wa bajeti ni vema zaidi kuona kwamba kama gari limechaka basi tutenge bajeti maalum kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunapata gari jipya ili kuondoa gharama za matengenezo ya kila siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali tumelisikia hilo, niwahamasishe sasa katika maeneo ya vipaumbele tuangalie lipi hasa ni kipaumbele cha wananchi katika eneo letu husika ili wananchi wapate huduma bora.