Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza:- Je, ni lini Shule ya Sekondari Isike iliyopo katika Kata ya Igombe itafunguliwa?

Supplementary Question 1

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ambayo hayajaniridhisha, naomba niseme kwamba shule ile ilifungwa kwa sababu alizozitaja lakini mpaka dakika hii Shule ya Sekondari Ulyankulu imefurika wanafunzi mpaka wamehamishiwa Shule ya Sekondari Mkindo ambayo sio ya bweni.

Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kuwarudisha wale wanafunzi ambao wanatembea umbali mrefu na kuwaongezea wazazi gharama ambazo hazihitajiki?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, shule ile imefungwa sasa hivi haifanyi kazi ya aina yoyote imekuwa ni makazi ya ngedere na nyani, hali ambayo inasababisha wananchi na Serikali waone kwamba walitupa nguvu zao za bure na za rasilimali fedha pasipokuwa na sababu ya maana.

Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kuirudisha tena kwa sababu mahitaji yamekuwa ni makubwa? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Naibu Waziri wangu kwa kujibu vizuri maswali yote yaliyokuja hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua fursa hii kumpongeza dada yangu Mheshimiwa Rehema Migilla kuwa Mbunge wa Ulyankulu, dada yangu hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lake tumelichukua kwa sababu tunafahamu eneo lile lilikuwa la wakimbizi, lakini wewe ndiyo uko site kule unaona mahitaji yote ya msingi. Hivi sasa namuagiza Afisa Elimu wetu wa Mkoa wa Tabora aende akafanye tathmini ya haraka atuletee majibu ya haraka ili kuhakikisha kwamba tunawasaidia watoto wa eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo siyo shule hiyo pekee, hata ile shule ambayo juzi katika ziara tulipokuwa na Mheshimiwa Rais tumetoa melekezo, shule hizo zifanyiwe harakati za haraka kama ikiwezekana tuzifungue haraka.

Lengo letu kubwa ni Watanzania waweze kupata huduma vizuri. Ahsante sana.