Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Sekondari ya Lanzoni iliyopo Wilayani Mkinga ilianzishwa mwaka 1995 kwa lengo la kuchukua wanafunzi wa chaguo la pili lakini inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa umeme, maji, usafiri pamoja na makazi ya watumishi:- Je, Serikali ina Mikakati gani ya kushirikiana na Halmashauri ya Mkinga katika kutatua changamoto hizo?

Supplementary Question 1

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama ambavyo aliyejibu swali amekiri kwamba Shule hii ina changamoto nyingi. Shule hii imeanza mwaka 1995 lakini iko ndani la eneo la shamba ambalo lilikuwa la Mkonge la Mjesani Estate, na mpaka sasa tunavyoongea shule hii haina hatimiliki ya lile eneo, kwa hiyo walimu na watendaji pale wamekuwa wanaishi kwenye shule ile kama vile wamepanga. Kwa hiyo nilitaka nifahamu, Wizara ina mkakati gani wa kuhakikisha shule hii inapata hatimiki ya eneo ili iweze kufahamu mipaka ya eneo lake kama Shule?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kama ambavyo amesema Mheshimiwa Waziri. kuhusu suala la maj. Pale kuna Mto Zigi ambao ndio wanaoutumia wanafunzi kuchota maji kwa ajili ya matumizi pale shuleni, na kumeshatokea ajali zaidi ya mbili ya wanafunzi pale kutaka kuuawa na mamba, ule mto una mamba. Je, Serikali kama mdau mkuu kwenye hili suala la elimu wako tayari kushirikiana na halmashauri na wadau wengine kuhakikisha milioni 7.6 inapatikana kwa wakati ili kupeleka maji kwenye shule ile?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Yosepher Komba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tunahitaji maeneo yote ya Umma yapimwe na yapate hatimiliki ili kuwa na uhalali wa eneo hilo lakini pia kupunguza migogoro ambayo inatokana na wananchi kuvamia maeneo hayo ya umma ikiwemo Mashule kama alivyotaja. Naomba nimuelekeze Mkurugenzi wa Halmashauri hii ya Mkinga atume wataalam wapimaji wakapime eneo hilo ili waweze kupata hati na kuondoa migogoro ambayo inaweza kuwepo katika eneo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili anazungumzia habari ya maji. Tumesema kwamba tathmini imeshafanyika, zinatakiwa shilingi milioni 7.6, na Serikali ipo tayari kushirikiana na halmashauri, na pia Mheshimiwa Mbunge ashirikiane na sisi. Sote kwa pamoja tuhakikishe kwamba tumepata maji katika eneo hili na watoto wetu waweze kupata huduma nzuri na masomo yaendelee.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Sekondari ya Lanzoni iliyopo Wilayani Mkinga ilianzishwa mwaka 1995 kwa lengo la kuchukua wanafunzi wa chaguo la pili lakini inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa umeme, maji, usafiri pamoja na makazi ya watumishi:- Je, Serikali ina Mikakati gani ya kushirikiana na Halmashauri ya Mkinga katika kutatua changamoto hizo?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na changamoto za maji na umeme katika shule zetu kumekuwa na tatizo kubwa sana katika shule nyingi nchini hasa Mkoa wa Mara pamoja na Jimbo la Bunda Mjini; tatizo la matundu ya vyoo. Athari kubwa ni kuleta magonjwa ya mlipuko kwa wanafunzi wetu pamoja na shule kufungwa. Sasa ningependa kuiuliza Serikali, ina mpango gani wa kushirikiana na taasisi mbalimbali katika kuhakikisha kwamba matundu ya vyoo yanajengwa shuleni ili kuwafanya wanafunzi wetu wasome wakiwa katika hali ya usalama zaidi wasipate magonjwa ya mlipuko?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya Mbunge wa Bunda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tuna upungufu mkubwa sana wa matundu vyoo nchi nzima kwa shule za msingi na sekondari.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili linapaswa kuwa jambo shirikishi, haiwezi kuwa kazi ya Serikali peke yake. Serikali imetoa Waraka ambao umeanza kutumika, wa mwaka 2016 ambao unaonesha namna ambavyo wadau mbalimbali wakiwepo na wananchi wa kawaida wanaweza kushirikiana kuweza kupunguza changamoto za miundombinu ya elimu. Serikali imekuwa ikifanya kazi hii awamu kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha; na mwaka wa fedha ambao unaanza Julai mwaka 2019/ 2020 tumetenga fedha zaidi ya shilingi bilioni 184 kwa ajili ya kuondoa kero katika miundombinu ikiwepo matundu ya vyoo. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge na wadau wengine tushirikiane; unapokuwa unaweza kuchangia tuchangie ili kuweza kupunguza adha hizi ambazo zipo katika shule zetu, ahsante.

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Sekondari ya Lanzoni iliyopo Wilayani Mkinga ilianzishwa mwaka 1995 kwa lengo la kuchukua wanafunzi wa chaguo la pili lakini inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa umeme, maji, usafiri pamoja na makazi ya watumishi:- Je, Serikali ina Mikakati gani ya kushirikiana na Halmashauri ya Mkinga katika kutatua changamoto hizo?

Supplementary Question 3

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Changamoto hii ya vyoo inawaathiri zaidi watoto wenye mahitaji maalum; watoto wenye ulemavu wanalazimika kutambaa katika uchafu, vinyesi vya watoto wenzao; na hiki ni kilio changu tangu nimeingia Bungeni.

Naomba mkakati madhubuti wa Serikali, wana mkakati gani wa kuhakikisha kwamba watoto wenye mahitaji maalum wanasoma katika mazingira mazuri na tunawaondoa katika hiyo hali hatarishi ya kuweza kupata magonjwa mbalimbali? Ahsante?. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amina Mollel kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba watoto na watu wote wenye mahitaji maalum wanahitaji special treatment ili aweze kuishi pamoja vizuri katika jamii yetu. Serikali imekwishaelekeza majengo yote mapya ambayo yanajengwa, si ya elimu tu, majengo yote ya Umma; wanapojenga jengo la Mkuu wa Wilaya, Mkoa, vituo vya afya zahanati na hospitali za mikoa pamoja na shule zote tunazingatia mahitaji ya watu wenye mahitaji maalum. Lazima kuna chumba maalum cha choo kwa ajili ya watu hao, lakini pia na watoto wa kike wakujisitiri wakati wao wa hedhi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa hiyo, mambo hayo tunaomba yazingatiwe na uongozi wote katika ngazi ya mikoa ya wilaya wafuate maelekezo ya Serikali. Tunapofanya ziara mbalimbali katika mikoa yetu miongoni mwa kazi ambazo tunafanya tunakagua kama kweli katika choo kilichojengwa kuna choo maalum. Maeneo yote tumefanya hivyo na jambo hilo linaendelea kufanya kazi vizuri. Hata hivyo majengo ya zamani yanapofanyiwa maboresho pia na jambo hili lizingatiwe; mahitaji maalum ni muhimu na limekubalika lazima lifanyiwe kazi, ahsante.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Sekondari ya Lanzoni iliyopo Wilayani Mkinga ilianzishwa mwaka 1995 kwa lengo la kuchukua wanafunzi wa chaguo la pili lakini inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa umeme, maji, usafiri pamoja na makazi ya watumishi:- Je, Serikali ina Mikakati gani ya kushirikiana na Halmashauri ya Mkinga katika kutatua changamoto hizo?

Supplementary Question 4

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona, Shule ya Sekondari ya Mumiterama iliyopo Wilaya ya Ngara imeanzishwa mwaka huu na haijawahi kupatiwa fedha yoyote kwa ajili kuendesha.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka pesa katika shule hiyo, kwa sababu ina changamoto nyingi, maji usafiri na makazi ya watumishi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuruku, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nipokee ombi lake, kwa sababu shule inapokuwa inaanzishwa kwanza kuna mambo ya kuzingatia, tunaangalia vigezo mbalimbali, Ofisi ya Rais TAMISEMI, pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Sasa kama shule imesajiliwa imeanza kweli haijawahi kupelekewa fedha naomba Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi cha maswali na majibu tuwasiliane tuone ni kwa nini haijapata na kama kuna ukweli wowote tuweze kuchukua hatua, ahsante. (Makofi)