Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Miaka iliyopita Serikali ilikuwa na nia ya kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na za upili. (a) Je, nini kilitokea kwa Serikali katika kutekeleza nia yake hiyo nzuri? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na za Upili ili kukuza uelewa wa wanafunzi katika masomo yao?

Supplementary Question 1

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri Mheshimiwa Waziri wa Elimu amejibu kwa kutumia sera, lakini swali langu mimi hapa lilitumia sheria na bahati nzuri sana amelielezea vizuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Kiswahili kimekuwa na kuwa moja ya lugha mashuhuri sana Duniani ambayo chimbuko lake ni Tanzania. Je, Serikali haioni umuhimu wa Kiswahili kutumika sasa kuwa lugha ya kufundishia katika elimu yetu kwa ngazi zote? Swali la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa Kiswahili sasa kimekuwa na kuwa bidhaa muhimu sana ya kuuza nchi za nje na hivyo kuingiza hela kupitia walimu wa Diaspora. Je, Serikali ina mpango gani wa kukikuza Kiswahili na kukiuza nje ya nchi? (Makofi)

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante ningependa kumjibu Mheshimiwa Almas Maige maswali yake ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuhusiana na lugha ya Kiswahili ambayo hakika ni ligha adhimu na imeendelea kushika kasi, suala la kutumia lugha hiyo kufundishia kama nilivyoeleza katika majibu yangu ya msingi lugha hiyo inatumika katika kufundisha katika shule za elimu ya awali, msingi na vyuo vya ualimu ngazi ya kati na bado Serikali inaona kuna umuhimu wa kutumia lugha ya kiingereza kama ambavvyo nilisema katika majibu yangu ya msingi na ndio maana ukiangalia hata Waheshimiwa Wabunge wengi humu ndani wanawapeleka watoto wao kwenye english medium kwa sababu wanatambua umuhimu wa lugha hiyo, kwa hiyo Serikali itaendelea kutumia lugha zote kama ambavyo imeelezwa katika sera ya elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kukuza Kiswahili, kwanza nshukuru kwamba lugha yetu ya Kiswahili imeendelea kupendwa na baadhi ya nchi wamekuwa wakiomba Tanzania kuweza kufundisha lugha ya Kiswahili katika nchi zao kama vile Sudan Kusini, Afrika ya Kusini pamoja na nchi nyingine. Kwa hiyo ni lugha ambayo Serikali itaendelea kuhakikisha kwamba tunaimarisha na suala la lugha ya Kiswahili sio suala tu la kujua kuzungumza, lakini pia lina suala la usanifu wa lugha ya Kiswahili, kwa hiyo tutaendelea kuhakikisha kwamba tunaimarisha ili fursa zinazojitokeza Watanzania waweze kunufaika zaidi. (Makofi)

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Miaka iliyopita Serikali ilikuwa na nia ya kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na za upili. (a) Je, nini kilitokea kwa Serikali katika kutekeleza nia yake hiyo nzuri? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na za Upili ili kukuza uelewa wa wanafunzi katika masomo yao?

Supplementary Question 2

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi niulize swali la nyongeza kama mwalimu kwa mwalimu mwenzangu Mheshimiwa Profesa Ndalichako.

Kwa kuwa umezungumza kwamba Wabunge wengi, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Mawaziri na watumishi wengi tu wa Serikali, sasa hivi wanapendelea sana kuwapeleka watoto wao shule za english medium. Lakini kwa kuwa hizi shule za english medium zimekuwa zikitoa malalamiko mengi kwamba Serikali haijajenga chuo cha kufundishia walimu special kwa ajili ya kwenda kufundisha hizi shule za english medium.

Ni lini Serikali itajenga Chuo cha Serikali ili walimu wa Tanzania waweze kusoma na kwenda kuwafundisha walimu hao kwa sababu tunatumia walimu wa Kenya na Uganda? (Makofi)

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana ningependa kujibu swali la nyongeza la mwalimu mwenzangu Mheshimiwa Phillipo Mulugo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lake ni la msingi kwamba Serikali iandae walimu ambao watafundisha katika shule ambazo zinatumia lugha ya Kiingereza, na niseme suala hili si lazima tujenge chuo, nimwambie kwamba suala hilo Serikali imelipokea na tutangalia utaratibu ambao tunaweza ndani ya muda mfupi tukaanza kuwa hata kuwa tunatoa hayo mafunzo katika vyuo ambavyo vipo hapa nchini. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Miaka iliyopita Serikali ilikuwa na nia ya kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na za upili. (a) Je, nini kilitokea kwa Serikali katika kutekeleza nia yake hiyo nzuri? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na za Upili ili kukuza uelewa wa wanafunzi katika masomo yao?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, majibu ya Waziri yameonesha kweli Kiswahili kimekua, lakini nchi ya Afrika Kusini wanafundisha Kiswahili na walitupa tender kama Tanzania ili tuweze kuwaandaa walimu wa kuwapeleka katika nchi ile. Lakini mpaka sasa hakuna jambo hilo limetekelezeka na hata nchi ya Kenya sasa wametupiku wamepeleka kule.

Je, Tanzania ina mkakati gani sasa wa kuhakikisha kwamba wana walimu wa kutosha wa kuwapeleka nchi hizo? (Makofi)

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimhakikishie kwamba Serikali au nchi yetu ya Tanzania inao walimu wa kutosha wa Kiswahili ambao ni wabobezi, kwa hiyo suala la upungufu wa walimu wa kutosha ambao wanaweza kwenda kufanya kazi katika nchi za nje hamna tatizo lolote.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la nchi kuamua kwamba inafanya kazi na nani hilo ni suala la hiyari ya nchi yenyewe, lakini kama Tanzania tuko tayari kupeleka walimu wetu wa Kiswahili mahali popote katika dunia hii kwa sababu tunao walimu wa kutosha mahiri na Serikali inaendelea kuimarisha ufundishaji wa somo la Kiswahili kwa sababu kama ambavyo tumeona lugha ya Kiswahili imeendelea kuheshimika na imeendelea kutumika sehemu mbalimbali katika Afrika na hata nje ya Bara la Afrika. (Makofi)

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Miaka iliyopita Serikali ilikuwa na nia ya kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na za upili. (a) Je, nini kilitokea kwa Serikali katika kutekeleza nia yake hiyo nzuri? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na za Upili ili kukuza uelewa wa wanafunzi katika masomo yao?

Supplementary Question 4

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwa kuwa swali la msingi linazungumzia suala la kufundisha Kiswahili na kwa kuwa Mheshimiwa Rais John Joseph Pombe Magufuli anakitangaza Kiswahili dunia nzima na kwa kuwa Serikali inajua umuhimu wa kukitangaza Kiswahili.

Je, kuna mkakati gani wa kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais katika kukitangaza Kiswahili, kwani nchi jirani wanachukua nafasi ya kuonekana wao ndio wamejipanga katika kuuza soko la lugha ya Kiswahili? (Makofi)

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza kwa dhati Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli hakika amekuwa ni Balozi mzuri sana katika kuhakikisha kwamba Kiswahili kinatumika na amekuwa akikitumia katika mikutano hata nje ya nchi na ameongeza chachu ya Kiswahili kutumika katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na hata katika Mikutano ya Umoja wa Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imeendelea kukitangaza Kiswahili kwa kuhakikisha kwanza kinatumika katika shughuli mbalimbali za kiserikali, lakini vilevile hili suala la kwenda kufundisha katika nchi za nje ni mojawapo ya hatua muhimu ya kutangaza lugha yetu ya Kiswahili na hata katika mikutano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki tumeona kimekuwa kinatumika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tutaendelea kuhakikisha kwamba fursa yoyote inayopatikana ya kutangaza lugha yetu ya Kiswahili tunaendelea kuitumia, lakini vilevile Wizara yangu itaendelea kuhakikisha kwamba tunaimarisha ufundishaji wa somo hili la Kiswahili kwa sababu kadri ambavyo tutakuwa na watalaam wengi wa Kiswahili hiyo pia ni sehemu moja wapo ya kutangaza lugha yetu ya Kiswahili.