Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni Watumishi wangapi wanahitajika na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili Mamlaka hiyo iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuruku, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza, Mheshimiwa Waziri uko tayari kunipatia mchanganuo wa hao wafanyakazi 7,000 wanaohitajika wanatosheleza kwa kiwango gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Swali langu la pili, kwa kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania ndiyo mamlaka iliyopewa wajibu mkubwa wa kukusanya kodi; na kwa kuwa ukirejea hotuba mbalimbali za Wizara ya Fedha utaona kuna upungufu mkubwa sana wa wafanyakazi; na kwa kuwa huko mtaani kuna vijana wengi ambao wamehitimu kwenye masuala mbalimbali ya kodi lakini hawajaajiriwa. Sasa nataka kujua, ni lini Serikali itaajiri Vijana wale ili wapate ajira na Mamlaka ifanye kazi kwa ufanisi kwa maendeleo ya taifa hili? ahsante.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tunza Issa Malapo Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza, anasema nimpatie mchanganuo wa hao watumishi 7,000. Mheshimiwa Tunza nimesema wanaohitajika ni 7,000 ambao tulionao Watumishi walioajiriwa ni 4,751 hawa hata leo hii nikimaliza kujibu maswali haya niko tayari kukupatia hawa 4,751. Kwa hao 7,000 pia niko tayari kukuandalia mchanganuo huo kwa kada zote ambazo zinahitajika na kukupatia ikiwezekana siku ya jumatatu tuwasiliane na nikupatie mchanganuo huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, naomba kwanza niseme, si kwamba Mamlaka ya Mapato ina upungufu mkubwa wa watumishi kama alivyosema, upungufu uliopo ni wa asilimia 28 tu siyo upungufu mkubwa. Kwa hiyo kama nilivyosema tunahitaji 7,000 tulionao ni 4,751 na Serikali ya Awamu ya Tano imejitahidi kwa kiwango kikubwa; tangu imeingia madarakani tayari tumeshaajiri Watumishi 692 na kwa mwaka huu tayari kwenye Bajeti yetu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania tutaajiri watumishi 150. Kwa hiyo tunakwenda hatua kwa hatua mpaka mwisho tutakamilisha wote Watumishi 7,000 wanaohitajika ili kuhakikisha Mamlaka ya Mapato Tanzania inafanya kazi zake kwa ufanisi.