Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA (K.n.y. MHE. PETER A. LIJUALIKALI) Aliuliza:- Jeshi la Magereza lilikuwa na mpango wa ujenzi wa Gereza Kitongoji cha Nakato na Kijiji cha Kibaoni, Wilaya ya Kilombero. Je, mpango huu umefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kumekuwa na msongamano mkubwa sana kwenye magereza mbalimbali hapa nchini na hasa ukiangalia kwa mfano kama Gereza letu la Ilembo pale Vwawa wafungwa wanaotakiwa kukaa pale pamoja na mahabusu ni 120; lakini mpaka sasa hivi kuna mahabusu pamoja na wafungwa zaidi ya 400 na hili limekuwa ni tatizo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua haya magereza kutokana na mrundikano huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kumekuwa na matatizo makubwa sana katika magereza haya, hakuna zahanati katika magereza yetu na kumekuw ana tatizo kubwa sana la wafungwa kutolewa kwenye haya magereza na kupelekwa kwenda kutibiwa katika hospitali mbalimbali hapa nchini wakati huo magereza hawana magari.

Serikali ina mpango gani wa kujenga zahanti katika magereza yetu yote hapa nchini ili wafungwa na mahabusu katika maeneo haya wawe wanatibiwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna utaratibu wa kujenga magereza mapya, kuongeza mabweni na kupanua kadri ya hali ya fedha inavyoruhusu. Kwa mfano, katika kipindi cha karibuni tumekamilisha ujenzi wa Gereza la Ruangwa, Gereza la Chato lakini pia na kufanya uongezaji wa mabweni katika magareza kadhaa nchini, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pale ambapo hali itaruhusu na Gereza la Vwawa vilevile nalo tutafanya upanuzi wa gereza hilo ingawa upanuzi wa magereza siyo njia pekee ya kupunguza msongamano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtakumbuka hivi karibuni, nichukue fursa hii kwanza kumpongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kutokana na dhamira yake ya dhati ya kuwatumikia wananchi wa nchi hii hususani wanyonge na hasa pale katika jitihada zake za kuona kwamba wanyonge wa nchi hii hawaonewi, alivyofanya ziara katika Gereza la Butimba hivi karibuni alitoa maelekezo nchi nzima ambayo yameshaanzakufanyiwakazi na yamesaidia sana kupunguza idadi ya mahabusu ambayo kimsingi msongamano huu kwa kiwango kikubwa unasababisha na mahabusu ambao ni wengi wakati mwingine wanapita hata idadi ya wafungwa.

Kwa hiyo, baada ya maelekezo yale na hatua ambazo mbalimbali zimechukuliwa sasa idadi ya mahabusu imeendelea kupungua nchini na hivyo kupunguza msongamano.

Lakini kwenye eneo hili la pili la zahanati, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuna utaratibu katika magereza yetu yote kuwa na madakrati pamoja na zahanati. Kwa hiyo, ninachoweza kusema ni kwamba katika maeneo ambayo tunaona labda kuna upungufu wa nguvukazi ya madaktari pamoja na madawa tufanye jitihada za kuongeza ili tuweze kukabiliana na changamoto ya wafungwa wetu na mahabusu ambao wanahitaji matibabu katika magereza. Kwa hiyo, hii kama katika Gereza la Vwawa ni changamoto nitalichukua na nifuatilie ni la ukubwa kiasi gani na tuweze kuchukua hatua stahiki.