Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLA JUMA aliuliza:- Je, Serikali ina mfumo gani wa kupandishwa daraja askari wenye vyeo vya chini?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLA JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri yaliyosheheni vigezo.

Mheshimiwa Spika, askari wa Jeshi letu la Polisi wanafanyakazi nzuri sana ikiwepo usalama barabarani, usalama wa raia na mali zao na kutuelimisha kutii sheria bila shuruti.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wako baadhi ya askari ambao hawakupandishwa cheo mpaka wamefikia kustaafu, na kwa kuwa kutokupandishwa huko si kosa lao, ni kosa la mfumo; je, Serikali ina mpango gani wa kuwafidia ili wasiwe wamepoteza haki zao na hasa kwa vile sasa hivi wako wastaafu wanahitaji sana fedha hizo?

Mheshimiwa Spika, swali langu lingine; Je, Serikali haioni umuhimu wa kuandaa mfumo na utaratibu uliowazi kabisa unaoonyesha namna gani na vigezo gani vya kuweka nafasi ya kwenda course ili uweze kupandishwa cheo na utaratibu huo uwe wazi na haki kabisa? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Asha Abdalla Juma, Mbunge wa Viti Maalum kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mfumo ambao tunao sasa hivi wa upandishwaji askari vyeo uko vizuri; na nimeeleza katika jibu la msingi vigezo ambavyo vinatumika. Hata hivyo kulingana na wingi wa askari tuliokuwanao na uchache na ufinyu wa nafasi hizo inasabbaisha wakati mwingine askari wengine kutumia muda mrefu zaidi katika kupata vyeo.

Hata hivyo tumekuwa tukifanya jitihada mbalimbali kuhakikisha kwamba wale askari ambao wanatimiza vigezo wanapata fursa ya kupandishwa vyeo; kwa hiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Asha Abdalla Juma kuhusiana na hilo.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusiana na hoja yake, kama nitakuwa nimemuelewa vizuri, ya kuwafidia, nadhani hilo halipo katika utaratibu. Kimsingi tu ni kwamba tutaendelea kuhakikisha tu kwamba askari ambao wenye sifa wanapandishwa vyeo. Katika kipindi cha mwaka huu mmoja, hivi karibuni tulipandisha vyeo askari kwa upande wa Jeshi la Polisi pekee kwa haraka haraka nadhani ni zaidi ya askari 9000 ukiachilia mbali majeshi mengine yaliyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani. Utaona kwamba tunafanya jitihada kama Serikali kuona askari hawa ambao wanafanyakazi vizuri wanapata fursa ya kupandishwa vyeo kadri ya hali na uwezo wa Serikali unavyoruhusu.