Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Sera ya Afya ni kuwa na Kituo cha Afya kwa kila Kata na Zahanati kwa kila Kijiji; Tarafa ya Nambis katika Jimbo la Mbulu Mjini haina Kituo cha Afya. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya kwenye Kata za Kainem, Murray, Nambis na Nahasey?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali kupitia Waziri, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa hospitali ya Mji wa Mbulu inategemewa na kata zinazopakana kutoka Wilaya ya Babati, Karatu na hata upande wa Jimbo la Mbulu Vijijini; na kwa kuwa hospitali hii inakabiliwa na upungufu mkubwa wa fedha za uendeshaji hali inayopelekea wagonjwa kujigharamikia wakati wa rufaa na ukosefu mkubwa sana wa dawa. Mheshimiwa Waziri ameshafika mara kadhaa na sasa hivi tuko kwenye mpango wa bajeti wa 2020/2021. Je, Serikali ina mkakati gani wa kusaidia hospitali ya Mji wa Mbulu kwa kuiongezea fedha za uendeshaji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Vituo vya Afya ya Daudi na Tlawi tayari vimeanza kutoa huduma, tunaishukuru sana Serikali. Pia nia ya Serikali ni njema kujenga Kituo cha Afya katika Tarafa ya Nambis ambapo vijiji vyake baadhi vina umbali wa kilomita 30 mpaka 40 kwenda hospitali wa Mji wa Mbulu. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka maombi niliyowasilisha ya gari la ambulance kutafutwa haraka ili wananchi wa kata hizo za Nambis na maeneo mengine ya pembezoni wapate huduma ya usafiri haraka kwenda kupata matibabu? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Zacharia Paul Issay, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge na pacha wake Mheshimiwa Flatei Massay hapa karibuni tulienda kufanya ziara katika Halmashauri hizi mbili na niwapongeze Wabunge hawa wamefanya kazi kubwa sana ya kusimamia miundombinu kwa fedha ambazo tumepeleka kule.

Mheshimiwa Spika, ni kweli hospitali ya Mheshimiwa Mbunge siyo suala la mgao wa fedha peke yake hata hali ya majengo haipendezi. Ndiyo maana kwa ombi la Mheshimiwa Mbunge nilipendekeza na nilielekeza kwamba zile shilingi milioni 500 sasa zianze kuibadilisha Hospitali ya Mbulu kwa sababu tunajua itakapokuwa na mazingira mazuri hata suala zima la ukusanyaji wa mapato litaongezeka. Hata hivyo, ni azma ya Serikali Mheshimiwa Mbunge wala usihofu tutaangalia nini kifanyike kuhakikisha mgao wa dawa katika eneo lile ambapo tunajua fedha nyingi sana zinaenda vijijini kuwasaidia Halmashauri ya Mbulu Mjini kuweza kuongeza ule mfuko wao wa dawa ili waweze kupata huduma vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ajenda ya upatikanaji wa ambulance, naomba nimhakikishie tutashirikiana na dada yangu Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya pale tutakapopata gari aina yoyote tutawapelekea. Kwa kweli nimefika kule na nimeona changamoto kubwa katika eneo hilo lazima tupate usafiri.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Sera ya Afya ni kuwa na Kituo cha Afya kwa kila Kata na Zahanati kwa kila Kijiji; Tarafa ya Nambis katika Jimbo la Mbulu Mjini haina Kituo cha Afya. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya kwenye Kata za Kainem, Murray, Nambis na Nahasey?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, tarafa ya Mtae katika Halmashauri ya Lushoto ambayo ina kata tano ndiyo pekee mpaka sasa hivi haijapata kituo cha afya. Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kujenga kituo cha afya katika Tarafa ya Mtae?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la ndugu yangu Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili amelileta kwa muda na alikuwa na changamoto pale Mnazi na Mtae na ndiyo maana tukaona tuanze katika eneo lingine lakini hii eneo la Mtae lipo katika mpango kazi wetu. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ajenda yetu ipo palepale katika mgao wa fedha tutakaoupata tutahakikisha suala la Mtae linapata kituo cha afya. Kwa hiyo, wala asiwe na hofu, ni jukumu letu kutatua changamoto kwenye maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, Mheshimiwa Shangazi wala asihofu suala hilo liko katika mpango wetu wa kazi.