Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KABWE Z. R. ZITTO aliuliza:- Katika kutekeleza mpango wa kutuma fedha za elimu moja kwa moja mashuleni Serikali hutuma shilingi bilioni 18 kila mwezi kwenye akaunti za shule nchini kwa mujibu wa maelezo ya viongozi kwa umma? (a) Je, Serikali imeshatuma kiasi gani cha fedha kati ya Januari – Desemba, 2016, 2017 na 2018 kwenda kwenye shule nchini? (b) Je, Serikali imefanya ukaguzi wa matumizi ya fedha hizo na kama zilizotoka Hazina zilifika kwenye shule husika; Je, Serikali ipo tayari kuleta Bungeni Ripoti za Ukaguzi huo? (c) Kama Serikali haijafanya ukaguzi huo; Je, ipo tayari kuagiza ukaguzi maalum utakaofanywa na CAG na kuweka Taarifa ya Ukaguzi huo?

Supplementary Question 1

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge lako Tukufu kila mwaka linatenga jumla ya shilingi elfu 10 kwa kila mwanafunzi wa shule ya msingi. Katika fedha hizo shilingi elfu sita zinapaswa kwenda moja kwa moja kwenye mashule na shilingi elfu nne zinakwenda TAMISEMI kwa ajili ya ununuzi wa vitabu, lakini Serikali inafahamu kwamba katika mpango wa GEP, Serikali ilipata zaidi ya shilingi bilioni 45 kwa ajili ya kununua vitabu, na kwa jumla ya idadi ya wanafunzi waliopo nchini wa shule za msingi, kuna zaidi ya shilingi bilioni 144 zilipaswa zinunue vitabu na shule hazina vitabu na kuna vitabu ambavyo viliondolewa, Serikali….

NAIBU SPIKA: Uliza swali.

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haioni kwamba, ni muafaka sasa kufanya ukaguzi maalum ili kuweza kutambua jumla ya fedha hizi shilingi bilioni 190 zimetumika namna gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika uchunguzi uliofanywa kwenye jumla ya halmashauri za wilaya 12 hapa nchini, katika shilingi elfu sita inayopaswa kwenda kwenye mashule kwa kila mtoto, fedha inayofika, kwenye hii sample ya wilaya 12 ni shilingi elfu 4200 tu. Serikali haioni haja ya kufanya ukaguzi maalum ili kuweza kufahamu hii shilingi 1200 ambayo haifiki kwenye shule inakwenda wapi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza si kweli kwamba TAMISEMI tunanunua vitabu, tumegawana kazi, suala la vitabu na kiwango chake na ubora wake linafanywa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Kwa kuwa ameuliza swali la kitakwimu na Mheshimiwa Naibu Waziri mwenzangu yupo hapa, basi unaweza ona namna ya kutenda hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la kujibu hapa ni kwamba, Mheshimiwa Zitto, anasema halmashauri zimekaguliwa, sisi kama Serikali hatuna taarifa ambayo anaizungumzia hapa Mheshimiwa Zitto, kwamba fedha
hazifiki katika shule zetu, na Mheshimiwa Zitto Kabwe, bahati nzuri kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali ya LAAC, Halmashauri ya Kigoma Ujiji ambayo ni Halmashauri ya chama chake cha ACT, ndiyo halmashauri ambayo imekuwa na hati chafu miaka minne mfululizo, lakini vilevile miradi ya elimu iliyopo pale, ina hali mbaya kweli kweli. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama kuna halmashauri imekaguliwa tuna takwimu za kutosha ni halmashauri ya Mheshimiwa Mbunge. Jibu ni kwamba, hakuna taarifa ambazo anazitoa, siyo za kweli, hakuna ukaguzi uliofanyika mahususi na hakuna malalamiko ambayo yameletwa kwamba Serikali tufanye ukaguzi maalum, tukipata taarifa hizo na maombi hayo, Serikali itachukua hatua kufanya ukaguzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukaguzi wa fedha ya elimu na miradi ya Serikali inafanyika kila wakati, kuna Kamati za Bunge, imeenda TAMISEMI, imeenda watu wa Ustawi wa Jamii wamekagua na taarifa zipo. Kila wakati tunachukua hatua kabla ya bajeti na baada ya bajeti hii ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Zitto kasema kwamba fedha za Global Partners for Education dola milioni 46 zinatumika kwa ajili ya vitabu. Naomba nimfahamishe kwamba, fedha hizo zinatumika kwa ajili ya kuendeleza sekta ya elimu kwa ujumla na siyo specific kwa ajili ya vitabu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia naomba nimhakikishie kwamba, fedha zote ambazo zinakwenda kwenye vitabu, zimeenda kwenye Taasisi yetu ya Elimu na kwa sasa tumefikia sehemu ambayo karibia vitabu vyote vinapatikana. Kuna vitabu ambavyo tunaendelea kuvichapisha lakini kwa sehemu kubwa vitabu vinapatikana sasa isipokuwa kama kuna changamoto kwenye halmashauri moja moja, inakuwa ni kesi ambayo ni specific lakini kwa ujumla kwa sasa tumeshaondokana na shida ya vitabu, tulichapisha vitabu vipya na tena vitabu ambavyo havina makosa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini zaidi, ninaweza nikakutana na Mheshimiwa Zitto nimueleweshe zaidi kwa sababu takwimu yeye ndiyo kaja nazo ambazo ziyo takwimu za Serikali, kwa hiyo, akitaka ufahamu zaidi anaweza akakutana na mimi nikamfahamisha.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. KABWE Z. R. ZITTO aliuliza:- Katika kutekeleza mpango wa kutuma fedha za elimu moja kwa moja mashuleni Serikali hutuma shilingi bilioni 18 kila mwezi kwenye akaunti za shule nchini kwa mujibu wa maelezo ya viongozi kwa umma? (a) Je, Serikali imeshatuma kiasi gani cha fedha kati ya Januari – Desemba, 2016, 2017 na 2018 kwenda kwenye shule nchini? (b) Je, Serikali imefanya ukaguzi wa matumizi ya fedha hizo na kama zilizotoka Hazina zilifika kwenye shule husika; Je, Serikali ipo tayari kuleta Bungeni Ripoti za Ukaguzi huo? (c) Kama Serikali haijafanya ukaguzi huo; Je, ipo tayari kuagiza ukaguzi maalum utakaofanywa na CAG na kuweka Taarifa ya Ukaguzi huo?

Supplementary Question 2

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, katika kuibadilisha dunia, ku-transform dunia, kigezo cha elimu kimepewa kipaumbele namba nne na kigezo cha elimu bora. Je, fedha hizi zaidi ya bilioni 900 ambazo zimekwenda kwenye shule zetu, kigezo cha kupima zimefanikisha kwa kiasi gani ubora wa elimu na viashiria vyake vyote ukoje!

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tumepeleka fedha zaidi ya shilingi bilioni 900 kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi la swali la Mheshimiwa Zitto, na Mheshimiwa Mbunge anataka kujua vigezo vya kuonyesha kwamba elimu imeboreka ni kwa kiwango gani.

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, fedha hii inafanya mambo mengi sana ikiwepo ni pamoja na uendeshaji wa shule, usimamizi wa elimu Tanzania umeimarika sana. Tumenunua pikipiki katika Waratibu Elimu wa kata zote nchini, sasa wanaweza ku-move kutoka shule moja kwenda nyingine, maana yake ni kwamba hata utoro rejareja umepungua shuleni, kiwango cha watoto kupata mimba na kuchukua hatua, tuna kesi mbalimbali mahakamani na baadhi ya watu ambao wametuhumiwa kuwapa wasichana wetu mimba wameshafikishwa mahakamani na wengine wamefungwa, kesi ziko katika hatua mbalimbali. Hiyo ni kwa sababu fedha hiyo imekwenda, imepeleka vifaa vya utendaji, pikipiki na imewezesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili, tumejenga hosteli maeneo mbalimbali, kitendo ambacho kimepunguza watoto wa kike wengi sasa wanakaa katika shule zetu na utaangalia matokeo mbalimbali, darasa la saba, form four na form six, kiwango cha ufaulu cha watoto wa kike kimeongezeka sana. Tumejenga mabweni na hosteli maeneo mbalimbali, watoto wa kike wengi wanakaa katika maeneo ya shule na usimamizi wao umekuwa ni mzuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini elimu msingi bila malipo, sasa hivi tunapozungumza, vijana wetu wa kidato cha nne wanafanya mitihani. Mwaka 2018 wanafunzi ambao walisajiliwa, watahiniwa wa kufanya mitihani, walikuwa 427,000, mwaka huu ni 485,866, maana yake ni ongezeko la wanafunzi ambao wameingia kidato cha nne zaidi ya asilimia 1.37, huu ni ufaulu mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vijana wengi wa Tanzania maskini ambao walikuwa hawana uwezo wa kusoma wa kike na wakiume, wengine walifanya kazi za house girl, wengine walikuwa makuli kwenye masoko, walikuwa wapiga debe, ninapozungumza hapa, vijana wengi kitendo cha Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kuondoa ada katika masomo yao, watoto wengi wapo mashuleni, hata wananchi ambao wanataka ma-house girls wanapata shida sana kuwapata, vijana, wasichana wengi wanasoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, hayo ni kwa uchache, lakini Mheshimiwa Mbatia ni kweli kwamba, yeye anafahamu, hata matokeo ya form six yameongezeka, elimu ya high school imekuwa ni kubwa sana, kwa sababu ya fedha hizi ambazo zimekwenda kuimarisha huduma. Ndiyo maana, hata wananchi ambao walitoa nguvu zao kuchangia kujenga maboma, tumepeleka fedha zaidi ya bilioni 29, angalia halmshauri zote nchini ili tumalize maboma, watoto wetu waendelee kukaa katika madarasa ambayo yapo sawa na wapate matundu ya vyoo. Ahsante.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. KABWE Z. R. ZITTO aliuliza:- Katika kutekeleza mpango wa kutuma fedha za elimu moja kwa moja mashuleni Serikali hutuma shilingi bilioni 18 kila mwezi kwenye akaunti za shule nchini kwa mujibu wa maelezo ya viongozi kwa umma? (a) Je, Serikali imeshatuma kiasi gani cha fedha kati ya Januari – Desemba, 2016, 2017 na 2018 kwenda kwenye shule nchini? (b) Je, Serikali imefanya ukaguzi wa matumizi ya fedha hizo na kama zilizotoka Hazina zilifika kwenye shule husika; Je, Serikali ipo tayari kuleta Bungeni Ripoti za Ukaguzi huo? (c) Kama Serikali haijafanya ukaguzi huo; Je, ipo tayari kuagiza ukaguzi maalum utakaofanywa na CAG na kuweka Taarifa ya Ukaguzi huo?

Supplementary Question 3

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kumekuwa na matumizi ya hovyo kabisa katika halmashauri zetu na kupelekea halmashauri hizo kupata hati chafu. Kwa mfano, Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga imepata hati chafu kwa mwaka mmoja, mimi najiona kama natembea bila nguo, lakini halmashauri kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri, Halmashauri ya Ujiji ambayo inaongozwa na ACT anapotoka Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe, miaka minne mfululizo imepata hati chafu wakati yeye akishinda twitter na instagram. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifuta halmashauri hizi? (Kicheko)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Ulanga, alikuwa anasema maneno mengi sana hapa Bungeni wakati mwingine akaonekana kwamba ni kituko, lakini naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, kauli ya Mheshimiwa Mbunge wa Ulanga imetusaidia sana TAMISEMI na watu wengi wamewajibishwa katika halamshauri ile na uchunguzi mahususi umefanyika tukagundua kuwa ni kweli kwamba watumishi wetu wamwekuwa wabadhilifu, fedha nyingi zililiwa, kama alivyokuwa analalamika.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni kwamba, ni kweli, Kamati ya Bunge ya LAAC wapo, Mwenyekiti yupo hapa na Wajumbe wenzake wanafamu. CAG alipopitia baadhi ya halmashauri, hata mimi nilishangaa, halmashauri mbili, wamepoteza fedha zaidi ya shilingi bilioni kumi na kitu, lakini Halmashauri ya Kigoma Ujiji, halmashauri hii imekuwa na hati chafu mfululizo miaka minne, lakini tulipowahoji viongozi wa pale, wakatuambia viongozi wetu wa kisiasa, wanaingilia mpaka manunuzi ya kisheria, mpaka tenda ambazo zinagawanywa pale Kigoma Ujiji, wanapewa kwa itikadi za kivyama, hizi ni taarifa rasmi za Bunge, ninazozitoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tumetoa maelekezo, ni kweli kwamba, ile halmashauri ikiendelea kupata hati chafu ya tano na itapewa ukaguzi mahususi, kuna uwezekano mkubwa Mheshimiwa Zitto halmashauri yako kufutwa kwa sababu husimamii vizuri, na wewe ni mtaalam wa mahesabu. Ahsante.