Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Mradi wa maji katika Kata ya Mtwango bado haujakamilika:- Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi huo ambao umechukua muda mrefu bila kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. MENDARD L. KIGOLA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, huu mradi wa maji wa Sawala umechukua muda mrefu sana zaidi ya miaka 6 na Serikali mara ya kwanza ilitoa fedha zaidi ya milioni 200 lakini hakuna kitu ambacho kimefanyika. Mara ya pili imetoa milioni 230, hakuna kitu kilichofanyika na wananchi pale sasa wanakata tamaa. Swali langu, ni lini mradi huu utakamilika ili wananchi waanze kupata maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna wakandarasi wawili wameshatolewa, sasa hivi Serikali inatumia mbinu gani ili kuhakikisha kwamba ile kazi inafanyika kikamilifu? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuweza kufuatilia miradi yake ya maji. Kikubwa utekelezaji wa miradi ya maji katika ubora unategemeana na upatikanaji mzuri wa wakandarasi.

Mheshimiwa Spika, nilifika pale Mufindi Kusini eneo lile la Mtwango, moja ya changamoto kubwa mkandarasi ambaye amepewa kazi ile alikuwa wa kibabaishaji (kanjanja) kwa hiyo tulimuondoa mkandarasi yule lakini tumeiagiza TAKUKURU kuhakikisha fedha zile za wananchi walipakodi azitapike mkandarasi yule. Sisi kama wizara tumehukua jukumu sasa la kuwapatia ndugu zetu wa Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) kwa maana ya kufanya kazi ile kwa force account mradi ule ukamilike na wananchi wake waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, ninachotaka kumuhakikishia Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Wizara ya Maji tunatumia forced account katika kuhakikisha mradi ule tunautekeleza kwa wakati na wananchi wako waweze kupata huduma hii muhimu. (Makofi)