Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha miradi ya umeme Vijijini katika vijiji ambavyo bado havijafikiwa Wilayani Chunya?

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, nimefurahishwa sana na majibu ya Serikali ambayo yanaonesha kwamba vijiji vingi vimepata umeme kwenye Wilaya ya Chunya, wilaya kongwe, na vijiji vilivyobaki vitapata umeme kwenye REA III inayoanza mwezi huu mpaka mwaka kesho.

Mheshimiwa Spika, nataka niweke tu rekodi sahihi kwamba katika Kata ya Sangambi, Kijiji cha Shoga – lakini sio shoga ya watu wa ughaibuni hapana, shoga ya Kitanzania ya urafiki – Kijiji cha Shoga; kwenye Kata ya Upendo Kijiji cha Nkwangu; Kata ya Nkung‟ungu Kijiji cha Nkung‟ungu, Majengo na Magunga; Kata ya Lualaje Kijiji cha Lualaje na Mwiji; Kata ya Matwiga Kijiji cha Mazimbo; Kata ya Mafieko Kijiji cha Mafieko na Biti Manyanga; Kata ya Kambikatoto Kijiji cha Kambikatoto na Sipa, je, vitapewa umeme kwenye REA Awamu ya III inayoanza mwezi huu? Ninafurahi sana na majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, nina swala dogo tu la nyongeza, katika Vijiji vyote hivi ambayo vilibaki kuna Kijiji cha Itumbi ambapo Serikali inaweka central of excellence yaani inaweka shule ya kuwafundisha wachimbaji wadogo na kwenye Kijiji hicho kuna makarasha zaidi ya 100 ya wachmbaji wadogo.

Je, Serikali iaweza ikatumia umuhimu wa pekee kuweza kumpa huyu ukandarasi ana addition BOQ ili Kijiji hicho kipate umeme mapema kuliko Vijiji vingine? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza ni kweli kabisa maeneo yote ya Jimbo lake yanaelekea kupata umeme kufikia mwezi Juni mwaka huu na hongera sana Mheshimiwa kwa kazi kubwa uliyofanya kwa niaba ya wana Jimbo.

Mheshimiwa Spika, katika Kijiji cha Itumbi ambapo central of excellence kwa wachimbaji wadogo itafanyika, mkakati wa Serikali umeshaanza, kwanza mbali na kupeleka Itumbi Mheshimiwa Mwambalaswa aliwaombea migodi ya wachimbaji takribani minne na hivi sasa mradi wa Matundasi ambao na wachimbaji wadogo wameshapata umeme migodi ya Makongorosi nayo imeshapata umeme na pia migodi ya wachimbaji kwa kuwa Sunshine nayo ilishapata umeme. Sasa kazi inayoendelea sasahivi nikupeleka umeme katika Kijiji cha Itumbi ambako kutakuwa na makarasha zaidi ya 128 na tumeshaandaa transfoma sita zenye uwezo wa kilovoti 115 kila mmoja na transfoma moja tutaifunga kwenye Kitongoji cha Matondo karibu kabisa na Itumbi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Kijiji cha Itumbi pamja na wachimbaji wadogo wenye makarasha na pamoja na maosheo watapata umeme tena mkubwa wa wachimbaji kuanzia mwezi Mei mwaka huu, ahsante sana.