Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:- Kambi za Jeshi 41KJ, 452 Medium ni miongoni mwa kambi kongwe na zenye mchango mkubwa katika Ulinzi wa Taifa letu. Kutokana na ukongwe huo, kambi hizo zimechakaa miundombinu yake mfano shule na zahanati zilizopo kwenye kambi hizo:- (a) Je, nini mpango wa Serikali juu ya kuboresha miundombinu ya Zahanati zilizopo kwenye kambi hizi? (b) Je, nini mpango wa Serikali wa kuboresha miundombinu ya shule hiyo iliyopo kwenye kambi hizo? (c) Je, nini mpango wa Serikali juu ya kuboresha miundombinu ya Medium Workshop hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza naomba nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake kwa niaba ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza ambalo nilikuwa naomba kujua, kwa sababu kituo hiki cha kanda ambacho kiko 41KJ kinahudumia wananchi wanaotoka maeneo ya Kilimani Hewa, Nampemba, Mtepeche, Mkotokuyana pamoja na Mandai; pamoja na mkakati ambao Serikali imeusema, hebu aniambie ni mkakati gani ambao Wizara wanaweza wakaufanya kwa haraka ili kuhakikisha wataalam wanapatikana katika kituo hiki ili wananchi waendelee kupata huduma pamoja ukarabati ambao tayari umeshafanyika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ambalo nilikuwa naomba kujua, ni suala hili la ukarabati wa kituo cha karakana ambacho kiko pale kikosi cha mizinga. Vijana wengi wa Nachingwea sasa hivi wanakosa sehemu ambako wanaweza kwenda kuendelea na masomo yao. Karakana hii kwa sasa inachukua idadi ndogo sana ya wanafunzi au wanachuo. Nini mkakati wa Wizara ili kuhakikisha jitihada hizi za kuihamisha hii karakara kuipeleka VETA unafanyika au kutoa fedha kwa ajili ya kununua vifaa na kuongeza wataalam ambao watakwenda kutoa huduma kwa vijana wa Wilaya ya Nachingwea?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza kwa dhati kabisa Mheshimiwa Masala kwa jitihada zake mbalimbali ambazo anachukua katika kuwasaidia wananchi wa Jimboni kwake Nachingwea. Amekuwa akifanya hivyo hata kwa taasisi na vyombo vilivyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, katika kujibu swali lake, kwanza kwenye eneo la wataalam kama ambavyo nimejibu katika swali langu la msingi, ni kwamba tayari hivi tunavyozungumza kuna madaktari takribani 300 ambao wanaendelea na mafunzo katika chuo chetu cha Monduli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni imani yangu kwamba madaktari wale watakapokuwa wamekamilisha mafunzo yao, basi miongoni mwao tutawapeleka katika hospitali ile iliyopo katika kikosi cha 41KJ, eneo la Nachingwea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake la mkakati wa kuboresha Chuo cha VETA; ni kweli Chuko cha VETA hiki kinasaidia sana na kitaendelea kusaidia zaidi wananchi hususan kwa maeneo ya Nachingwea na maeneo mengine nchini kitakapokuwa kimeimarishwa. Ndiyo maana dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kwamba inakiimarisha chuo hiki ikiwa kimo katika mpango kazi wa Jeshi la Wananchi Tanzania. Miongoni mwa mambo ambayo tunatarajia kufanya ni kuhakikisha kwamba chuo hiki kinaunganishwa na VETA.

Mhehsimiwa Mwenyekiti, hivi sasa tunavyozungumza, ni kwamba tunatoa huduma ile kwa kuazima Walimu kutoka VETA kuja kufundisha, lakini pale ambapo mikakati hii itakapokamilika, tutakuwa tuna Walimu wa kutosha ambao watakuwa pale pale chuoni muda wote. Mbali ya hiyo, tutakuwa tunaweza kuongeza vifaa pamoja na kuimarisha majengo ya chuo hicho ili kiweze kutoa huduma kwa wananchi wengi zaidi wakiwemo wananchi wa Mheshimiwa wa Jimbo la Nachingwea kwa Mheshimiwa Hassan Masala.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:- Kambi za Jeshi 41KJ, 452 Medium ni miongoni mwa kambi kongwe na zenye mchango mkubwa katika Ulinzi wa Taifa letu. Kutokana na ukongwe huo, kambi hizo zimechakaa miundombinu yake mfano shule na zahanati zilizopo kwenye kambi hizo:- (a) Je, nini mpango wa Serikali juu ya kuboresha miundombinu ya Zahanati zilizopo kwenye kambi hizi? (b) Je, nini mpango wa Serikali wa kuboresha miundombinu ya shule hiyo iliyopo kwenye kambi hizo? (c) Je, nini mpango wa Serikali juu ya kuboresha miundombinu ya Medium Workshop hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imekuwa ikichukua vijana wengi kuwapeleka kwenye mafunzo ya JKT na baada ya mafunzo hayo, vijana wachache sana ambao wanapata ajira na vijana wengi wanakuwa wako mitaani. Kwa nini Serikali isije na mikakati ya hao vijana ambao wanamaliza mafunzo ya JKT kuwatafutia ajira mbalimbali kama vile kwenye migodi na maeneo mengine ili kuweza kupunguza vijana hao kuzurura mitaani na baadaye kuandaa bomu ambalo ni hatari? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza malengo ya kuwapeleka vijana JKT, haina maana kwamba vijana wote watakaopelekwa JKT wataajiriwa na vikosi vyetu vya ulinzi na usalama, ni kwa sababu idadi ya nafasi za ajira zilizopo katika vyombo vyetu hivi ni chache kulinganisha na idadi ya vijana ambao wanaingia JKT. Hata hivyo, kwa kuwa mafunzo haya ya JKT yanaimarisha uzalendo na kujenga ujuzi mbalimbali, kwa hiyo, ni imani ya Serikali kwamba maandalizi ya vijana ambao wanakwenda JKT yatawasaidia kuweza kutumia fursa nyingine zilizopo nchini za kuweza kupata ajira ikiwemo katika taasisi binafsi, taasisi za Serikali, pamoja na kujiajiri wenyewe.

Name

Saada Salum Mkuya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:- Kambi za Jeshi 41KJ, 452 Medium ni miongoni mwa kambi kongwe na zenye mchango mkubwa katika Ulinzi wa Taifa letu. Kutokana na ukongwe huo, kambi hizo zimechakaa miundombinu yake mfano shule na zahanati zilizopo kwenye kambi hizo:- (a) Je, nini mpango wa Serikali juu ya kuboresha miundombinu ya Zahanati zilizopo kwenye kambi hizi? (b) Je, nini mpango wa Serikali wa kuboresha miundombinu ya shule hiyo iliyopo kwenye kambi hizo? (c) Je, nini mpango wa Serikali juu ya kuboresha miundombinu ya Medium Workshop hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. SAADA MKUYA SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na kazi nzuri ambazo zinafanywa na vikosi vyetu hivi vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, kuna maeneo ambako kuna Kambi za Majeshi na kumekuwa kuna uwekezaji ambao unaendelea, hususan kumbi za disco, pamoja na mambo mengine ambayo yanafanana na hayo ambayo mara nyingine zinaleta athari za kiutamaduni na maadili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inasemaje kuhusiana na kambi hizo ambazo zinakuwa zinapigwa disko katika maeneo ya wananchi na hivyo kuathiri utamaduni pamoja na maadili ya maeneo yanayohusika? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi ya kumbi za starehe katika nchi yetu yapo kwa mujibu wa taratibu tulizojiwekea na siyo katika makambi ya Jeshi tu, ni maeneo mbalimbali. Hata kumbi ambazo zipo katika maeneo ya Kambi za Jeshi kwa ajili ya starehe zinatakiwa zifuate utaratibu ule ule ambao tumejiwekea wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sidhani kama ni sahihi kuonyesha kidole katika maeneo ya kambi ya Jeshi peke yake, imani yangu ni kwamba ukizingatia maadili na misingi ya Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania, nadhani itakuwa ni sehemu ya mwisho kuonyeshwa kidole katika ukiukwaji wa sheria hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kama ana kesi mahususi ambayo anadhani inahitaji kufuatiliwa, namwomba Mheshimiwa Saada Mkuya atupatie taarifa ya eneo la kambi ambalo anazungumza ili tufuatilie na kuona hatua za kuchukua.