Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza:- Vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga bado ni tatizo nchini:- Je, Serikali inafanya jitihada gani kupunguza na ikiwezekana kuondosha kabisa vifo hivyo?

Supplementary Question 1

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi, Serikali ya Awamu ya Tano kwa jinsi ambavyo inajitahidi kuboresha afya ya Watanzania lakini bado nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, pamoja na jitihada za Serikali lakini kuna tatizo kubwa ambalo liko vijijini na mijini, wanawake wengi bado wakiwa wajawazito hawana ile elimu ya kuona kwamba ni muhimu waende clinic. Sasa Serikali mnajitahidi kiasi gani kuhakikisha wanawake wakiwa wajawazito vijijini pamoja na mijini wanakwenda clinic? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, tafiti zilizofanywa katika nchi yetu ya Tanzania, bado watoto ambao wana chini ya umri wa mwezi mmoja baada ya kuzaliwa wanakufa kwa wingi na ukweli tafiti zimeonesha kwamba hawajapungua kabisa, wanaendelea kufa. Serikali mnaniambia nini katika hili? (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpa pongezi sana amekuwa ni champion mkubwa sana katika masuala ya afya ya uzazi wa akina mama na mtoto. Nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi zake hizo.

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nijielekeze katika maswali mawili mawili ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyauliza. La kwanza ni kuhusiana na akina mama kwenda kliniki. Ni kweli, Serikali imewekeza juhudi kubwa sana katika kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za afya. Mwaka 2015 idadi ya akina mama ambao walikuwa wanakwenda clinic ilikuwa ni asilimia 38 kwa mara zote nne katika kipindi cha ujauzito lakini Serikali imeendelea kuweka juhudi, mikakati mbalimbali pamoja na kutoa elimu kwa akina mama, hivi tunavyoongea hadi kufikia Desemba 2019, asilimia 80 ya akina mama wanakwenda kiliniki.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hii nayo ni hatua kubwa sana katika kuhakikisha akina mama wanapata elimu, ushauri katika kipindi chao cha ujauzito na hii inaweza kusababisha hata kupunguza vifo vya akina mama na watoto. Nitoe rai kwa akina mama wote na akina baba kwa sababu masuala haya ya ulezi wa ujauzito ni jukumu la wazazi wote wawili kuhakikisha kwamba kila mama mjamzito anafika kliniki kwa ajili ya kuweza kupata ushauri nasaha na jinsi gani ya kuweza kutunza ujauzito ule.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake la pili vifo vya watoto chini ya mwezi mmoja, ni kweli katika takwimu ambazo hazishuki ni pamoja na hii. Katika mwaka 2015, tulikuwa na watoto wachanga chini ya mwezi mmoja wakifariki 26 kwa vizazi hai 100,000. Sasa hivi tunapoongelea Desemba mwaka jana imeshuka kwa unit moja tu mpaka 25 kwa vizazi hai 100,000.

Mheshimiwa Spika, lakini sisi kama Serikali tunajaribu kuweka hatua, kwanza kuhamasisha akina mama kwenda kliniki; pili kuhakikisha kwamba chanjo zote za msingi za watoto chini ya miaka mitano zinapatikana; kutoa elimu kwa watoa huduma wa afya pamoja na akina mama ikiwa ni pamoja na jinsi ya kutunza watoto njiti. Visababishi vikubwa vya watoto chini ya mwezi mmoja ni zile complication ambazo wanazipata wakati wa kupumua wakati wa kujifungua, maambukizi ya magonjwa ambayo wanayapata wakati wa kujifungua ikiwa ni pamoja na uzito wa chini.

Mheshimiwa Spika, hii ndiyo mikakati ambayo tumejaribu kuifanua kwa kupanua huduma za afya kuhakikisha kwamba akina mama wajawazito ambao wana pingamizi wanapata huduma kwa haraka. Tumepunguza sana maambukizi ya watoto hawa na kuhakikisha wale watoto njiti wanatunza kwa njia ya kangaroo motherhood ambapo kwa kiasi kikubwa tunaamini sasa tutapata matokeo makubwa sana. (Makofi)