Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Katika eneo linalopatikana gesi aina ya carbondioxide (CO2) kwenye Jimbo la Busekelo, Kijiji cha Mpata kuna visima ambavyo ni hatari kwa binadamu na viumbe hai wengine kwani huwa wanakufa wakivuta hewa ya sehemu hiyo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kunusuru maisha ya binadamu na viumbe katika eneo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Pamoja na juhudi nzuri za Serikali zilizofanywa pamoja na Kampuni hii ya Tanzania Oxygen Limited kuweza kuzuia baadhi ya wanyama watambaao pamoja na binadamu kwenda kwenye eneo hili la kisima ambacho mara nyingi miaka ya nyuma Wananchi na wanyama wengine walikufa kutokana na kuvuta gesi hii ya carbondioxide. Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itaendelea kutoa elimu kwa wananchi ambao wanazunguka kisima hiki na kwa kuwa nguvu za asili za volcano bado zipo na volcano nii ni hai ili kuzuia madhara yatokanayo na kuvuta gesi hii ya carbondioxide?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa Serikali imeonesha nia njema kwa ajili ya kujenga viwanda hapa nchini lakini kumekuwa kuna changamoto kubwa kuingiza gesi hii ya carbondioxide ndani ya Nchi yetu ya Tanzania tukitambua kwamba carbondioxide gas inatumika katika mazingira ama kwenye vitu vingi ikiwemo vyakula pamoja na vinywaji ili visiharibike. Ni kwa kiwango gani Serikali itavutia zaidi wawekezaji kwenye maeneo mengine ambayo gesi hii ya carbondioxide bado haijaanza kuchimbwa.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri katika majibu ya msingi ya suala la Mheshimiwa Mwakibete, lakini vilevile nimpongeze sana Mheshimiwa Mwakibete kwa kufuatilia masuala haya ya matumizi ya carbondioxide.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwanza ni lini Serikali itaendelea kutoa elimu; Kampuni ya Tanzania Oxygen kwanza imetenga takribani dola milioni tano kila mwaka kawa ajili ya kutoa elimu katika maeneo yao ya leseni. Kwa hiyo shughuli za kutoa elimu zinaendelea, lakini sambamba na hilo Serikali kwa kushirikiana na Tanzania oxygen zimeweka timu mahususi kwa ajili ya mpangokazi wa kutoa elimu kila mwezi katika maeneo hayo. Kwa hiyo shughuli za utoaji wa elimu ni endelevu.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala la pili la kulinda soko la ndani; ni kweli, kwanza kuna nchi ambazo zinzalisha carbondioxide kama Tanzania, mathalani; DRC, Kenya na Nchi ya Msumbiji. Kwa Tanzania tunachofanya kwa sasa tumeunda timu mahususi kwa ajili ya kufanya tathmini ili kuangalia mahitaji ya ndani na uwezo tulionao ndani ya miezi mitatu, tukishajiridhisha kwamba uwezo wa ndani wa carbondioxide unatosha kuzalisha vinywaji kama soda pamoja na vinywaji vya bia, tutazuia kabisa carbondioxide kutoka nje badala yake tutumie viwanda vya ndani.

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Katika eneo linalopatikana gesi aina ya carbondioxide (CO2) kwenye Jimbo la Busekelo, Kijiji cha Mpata kuna visima ambavyo ni hatari kwa binadamu na viumbe hai wengine kwani huwa wanakufa wakivuta hewa ya sehemu hiyo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kunusuru maisha ya binadamu na viumbe katika eneo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi. Vijiji vya Katani, Malongwe, Sintaling, Kana na vinginevyo viko katika Awamu ya III ya kupewa umeme mzunguko wa pili lakini mpaka sasa hatujapata. Je, ni lini mradi huu utaanza?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu spika, nishukuru sana majibu yaliyotolewa upande wa Wizara ya Nishati lakini kwa kusisitiza kwa jinsi alivyouliza Mheshimiwa Atu sisi Wizara ya Madini kwa kushirikiana na TOL…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Malizia kabisa jina lake kwa sababu kule ukikatisha kule kwao anaweza ikajulikana kuna Mbunge mpya humu ndani. Mheshimiwa Fredy Atupele Mwakibete.

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu spika, ahsante sana Mheshimiwa Atupele Mwakibete. Ni kwamba Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Kampuni ya Oxygen Limited katika lile eneo ambalo linatoa ile hewa ya carbondioxide kampuni ya TOL wameweka sensa maalumu kwa ajili ya ku-detect hewa ile inapojitokeza kutambua mapema, na hewa hiyo inapojitokeza zile sensa zinatoa taarifa kwamba kuna hewa chafu inakuja na kwa kweli wanatoa taarifa katika maeneo yale kwa watu wanaozunguka maeneo yale kuweza kukaa mbali na lile eneo na kuhakikisha kwamba hapatokei tena vifo vinavyotokana na watu kupumua hewa hii ya ukaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kuna zile hatua za awali zimeshachukuliwa na kwa kweli Tanzania Oxygen kupitia leseni yao namba 139 ambayo imetolewa mwaka 2002 wako tayari sasa kuhakikisha kwamba wanakwenda katika uwekezaji na kuhakikisha kwamba wanakwenda kuitumia ile hewa ya carbon dioxide katika matumizi mbalimbali ambao yamepangwa ahsante sana. (Makofi)

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli maeneo ambayo ameyataja Mheshimiwa Mbunge yako katika mpango wa pili wa utekelezaji wa mradi wa REA, na kwa kweli katika eneo la Katani na Malongwe imeshaingia kwenye mpango huo na utekelezaji wake unaanza Februari mwaka huu kuanzia tarehe 28. Lakini kuna suala moja ambalo Mheshimiwa hajauliza kule Wampembe umbali takribani wa kilometa 68 kutoka Mjini ni eneo ambalo ni tengefu sana, eneo hili lilikuwa nalo liingie kwenye mpango wa round ya pili lakini badala yake tumeanza kuitekeleza kuanzia wiki iliyopita. Nimeomba nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge ili awape taarifa wananchi wake wananchi wa Wampembe ambao wanahitaji umeme kwa haraka sana ahsante sana.