Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu ya malimbikizo ya madeni mbalimbali ya wazabuni wanaotoa huduma mbalimbali ikiwepo huduma ya kupeleka chakula kwa wanafunzi magerezani na matengenezo ya magari. Je, Serikali ina mkakati gani wa kulipa madeni hayo?

Supplementary Question 1

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, la kwanza, kwa kuwa madeni haya ni ya muda mrefu na imetokea mara nyingi Serikali imekuwa ikilipa madeni yaliyokuja baadaye wanaacha yale ya nyuma. Sijui ni vigezo gani vinatumika kuacha madeni yale ya muda mrefu na kulipa yale ambayo yamekuja baadaye?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wazabuni wengi wanaodai magereza kwa maana wale wanaofanya zabuni ya chakula wengi sasa wana hatari ya kuuziwa nyumba zao hasa wale ambao wamekopa katika taasisi mbalimbali za fedha. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha hawa wazabuni mbalimbali inawakomboa wasiweze kuuziwa nyumba zao na taasisi za kifedha?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, madeni ambayo yanalipwa ni miongoni mwa madeni ambayo tumeshalipa kama ambavyo nimeeleza katika jibu la msingi pia yako madeni ya zamani na nilieleza kwamba madeni mengine ambayo hayajalipwa ni kutokana na kwamba mengine yameshahakikiwa na hivyo basi pale fedha ambapo zitapatikana yatalipwa. Naamini kabisa yatakapokuwa yamekamilika madeni hayo kulipwa kama ambavyo nia ya Serikali ilivyo basi yale matatizo ambayo yanakabiliwa na hawa wazabuni yataweza kupatiwa ufumbuzi. Ni dhamira ya Serikali kuhakikisha madeni haya yanalipwa ili kuepusha usumbufu wowote kwa wazabuni wetu.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu ya malimbikizo ya madeni mbalimbali ya wazabuni wanaotoa huduma mbalimbali ikiwepo huduma ya kupeleka chakula kwa wanafunzi magerezani na matengenezo ya magari. Je, Serikali ina mkakati gani wa kulipa madeni hayo?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, ni dhahiri kwamba Serikali imekuwa haitoi kipaumbele kwenye huduma muhimu za binadamu badala yake wamekuwa wakiwekeza zaidi kwenye vitu.

Mheshimiwa Spika, magereza ni moja ya sehemu ambazo inatakiwa wapewe vipaumbele na wapewe huduma stahiki kama inavyoelekeza. Wazabuni wengi wanadai na wameacha kutoa huduma za vyakula na mambo mengine.

Mheshimiwa Spika, cha kusikitisha zaidi nilitaka nijue, Serikali ni lini itatoa nguo kwa wafungwa ambao mnasema kabisa wakishafungwa wavae yale mavazi. Niliona hiyo nikiwa Segerea, lakini juzi nilivyotembelea Gereza la Tarime pamoja na matatizo mengi ambayo yametokana na kutokulipa madeni ya wazabuni na kuweza kutoa vifaa hivi unakuta mpaka Askari Magereza anachukua nguo zake anavisha mfungwa kama anavyotoka nje.

Ni lini sasa Serikali itaondoa hii fedheha ihakikishe kwamba wafungwa ambao wanastahili kuvaa nguo waweze kupewa zile nguo ambazo wataweza kujihifadhi? Na wajue kabisa kwamba waliopo Serikalini leo magereza ni yao kesho. (Kicheko)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimsahihishe siyo sahihi kwamba Serikali haitoi kipaumbele kwenye huduma mbalimbali ikiwemo za wafungwa. Nimhakikishie kwamba wafungwa hawa tumekuwa tukiwapatia uniform na siyo wote kama ambavyo umetaka ieleweke kwamba hawana uniform, lakini changamoto hii itaendelea kupungua hatua kwa hatua. Hata hivyo, sehemu kubwa ya wafungwa tayari wameshaanza kupatiwa nguo kwenye magereza.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu ya malimbikizo ya madeni mbalimbali ya wazabuni wanaotoa huduma mbalimbali ikiwepo huduma ya kupeleka chakula kwa wanafunzi magerezani na matengenezo ya magari. Je, Serikali ina mkakati gani wa kulipa madeni hayo?

Supplementary Question 3

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, naomba niwakumbushe kuwa tarehe 24 Januari, 2020 Serikali imesaini makubaliano ya kuchukua asilimia 16 kutoka Barrick Gold Tanzania, kwa hiyo sasa hivi Serikali ina 16%, maana yake watu wengi hawajaisikia hiyo, kwa hiyo inabidi tuongeze sauti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Gereza la Ulanga mwaka wa tano sasa hivi mahabusu wanapelekwa mahakamani kwa kutumia bodaboda. Hii ni hatari sana kwa mahabusu kutoroka. Naomba kuuliza swali la nyongeza, je, ni lini Serikali itapeleka gari la mahabusu Gereza la Ulanga? (Makofi/ Kicheko)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mlinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mlinga kwa jinsi ambavyo anaweza kujenga hoja zake kwa msisitizo, sisemi kwamba anatia chumvi, lakini anajenga hoja kwa msisitizo na anatukumbusha mambo muhimu kama ambavyo ametukumbusha hili suala la mafanikio kwenye sekta ya madini.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mlinga kwamba najua anapozungumza bodaboda alitaka tu kuongeza uzito wa hoja yake, lakini tunatambua juu ya changamoto ya usafiri katika baadhi ya magereza yetu nchini na nimhakikishie pale ambapo gari mpya zitakapopatikana, tutampelekea katika gereza hilo la Jimboni kwa Mheshimiwa Mlinga ili kukabiliana na changamoto hiyo ya usafiri.