Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Serikali ya Tanzania ni mdau mkubwa wa Mradi wa Bomba la Mafuta ghafi kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga na Serikali pamoja na wawekezaji katika mradi huu walishateua eneo la kujenga kiwanda cha kuunganisha na ku-coat mabomba katika Mji Mdogo wa Isaka. Je, ni hatua gani imefikiwa katika ujenzi wa kiwanda hicho?

Supplementary Question 1

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake pamoja na majibu hayo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati utafiti wa awali unafanyika kuhusu maeneo yanayofaa kwa ajili ya mradi huu waliokuwa wakifanya utafiti walifika pia Isaka na Igusule kama ambavyo jibu limesema na baada ya maamuzi kufanyika kwamba mradi huu unajengwa Igusule walisema bado kuna miundombinu muhimu ya Isaka ambayo itatumika ikiwa ni pamoja na Ofisi za TRA, Bandari ya Nchi Kavu, Reli, Umeme pamoja na ofisi zingine za Kiserikali.

Sasa nilitaka kufahamu kwa sababu pia walisema wataweka transit yard pale Isaka nilitaka kujua hatua gani imefikiwa kwa ajili ya upataji wa eneo hilo la transit yard na maandalizi ya wananchi wa Isaka kwa ajili ya kushiriki katika huo mradi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa mradi huu unatoa fursa za kibiashara na ajira kwa wananchi waliowengi sana wa maeneo hayo. Je, ni maandalizi gani ya kiujumla ambayo yamefanyika kwa ajili ya kuandaa wananchi hawa wa Isaka pamoja na Igusule ili waweze kushiriki katika kunufaika na mradi huo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI (K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia mradi huu wa Bomba la Mafuta kutoka Hoima Uganda na namna gani wananchi wake hususan wa Jimbo la Msalala watakavyoweza kufaidika na maswali yake mazuri ya nyongeza na mara baada ya kukubali uamuzi wa wabia wa mradi huu wa eneo la kujenga kiwanda iwe Igusule.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa kuwa maswali yake ya nyongeza yamehusiana na miundombinu mingine ni kweli tafiti mbalimbali zimeendelea kufanyika kuhuisha miundombinu mbalimbali ikiwemo reli, ikiwemo ofisi mbalimbali za kiserikali itakavyotumika katika mradi huu na nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika eneo la Isaka hapo pia vitajengwa ofisi ya mradi huu ya EACOP na miundombinu mingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia wananchi wake na yeye mwenyewe anajua eneo la Igusule ni kama kilometa 5 tu kutoka Isaka. Kwa hiyo, ni wazi kabisa wananchi wa maeneo ya Isaka na maeneo mengine ya Mkoa wa Shinyanga pamoja na Mkoa wa Tabora watapata fursa mahususi kabisa katika mradi huu ikiwemo ajira na masuala mengine ya kibiashara na mpaka sasa mradi huu umeajiri takribani watanzania 229 kwa hizi hatua za awali lakini kuna makampuni nane yanatoa huduma mbalimbali katika mradi huu lakini pia faida zake mojawapo ni utoaji wa ajira utakapoanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikutaarifu tu kwa sasa mazungumzo yanaendelea na kwamba hatua ambayo imefikiwa sasa hivi ni tumefika mbali na tunatarajia mradi huu kuanza mwezi septemba 2019. Kwa hiyo, utakapoanza utaleta tija kubwa na faida kwa wananchi wa mikoa nane iliyopitiwa na bomba hili, wilaya 24, kata 134 na vijiji 280.

MHE. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana yaliyosemwa na Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niwadhibitishie Waheshimiwa Wabunge Serikali kwa kutambua umuhimu wa mradi wa bomba hilo la mafuta na jinsi litakavyoweza kukuza ajira na uchumi wa Taifa letu, Ofisi ya Waziri Mkuu imeandaa programu maalum ya local content na tumeanza mafunzo maalum katika mikoa hiyo yote nane ili kuwahabarisha wananchi katika mikoa hiyo ni namna gani wanaweza wakatumia fursa mbalimbali ambazo zitapatikana katika mradi huo muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe wito kwa Wabunge wote ambao wanatoka katika mikoa ambayo inapitiwa na bomba hilo tuweze kuwasiliana ndani ya Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuwaweka pamoja wananchi wao waweze kufaidika na mradi wa bomba la mafuta katika fursa mbalimbali zitakazopatikana.

Name

Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Serikali ya Tanzania ni mdau mkubwa wa Mradi wa Bomba la Mafuta ghafi kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga na Serikali pamoja na wawekezaji katika mradi huu walishateua eneo la kujenga kiwanda cha kuunganisha na ku-coat mabomba katika Mji Mdogo wa Isaka. Je, ni hatua gani imefikiwa katika ujenzi wa kiwanda hicho?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante pamoja na majibu yaliyotolewa na Mheshimiwa Jenista na Mheshimiwa Naibu Waziri suala la Local content ni muhimu sana katika nchi yoyote ili uchumi ubakie ndani na sio utoke nje. Lakini inahitaji maandalizi kama alivyosema. Sasa hivi sasa tuna sectoral individual locally content policies. Je, Serikali iko tayari sasa kuja na sera kubwa na mabadiliko ya sheria juu ya local content na pia sheria hiyo iwemo na vifungu ambavyo vinaweza kuwawzesha wananchi kifedha ili wafaidi localy content?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

MHE. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa swali la nyongeza lililoulizwa na Mheshimiwa Ally Saleh na Mheshimiwa Ally Saleh anafahamu kwenye Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria tumekuwa tukitoa taarifa hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshaanza hiyo kazi nzuri baadhi ya sheria ambazo zimekwisha kutungwa kwa mfano Sheria ya Mafuta na Gesi, hizo zote zimeshawekewa misingi ya kisera ya local content na imeshaanza kufanya kazi kwenye kanuni na sheria hizo. Lakini naomba nimhakikishie ili kufanya maandalizi hayo muhimu Ofisi ya Waziri Mkuu imeshatoa mwongozo wa local content katika miradi yote ya kimkakati ambayo inaendelea kwa sasa ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hii miradi yote ujenzi wa reli na miradi mingine yote mikubwa ya kimkakati sasa hivi mwongozo wa local content umekuwa ukitumika na sisi kama Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi tunasimamia kwa karibu sana kuhakikisha wazawa wanafaidika na miradi hii mikubwa ya kimkakati ndani ya Taifa letu.

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Serikali ya Tanzania ni mdau mkubwa wa Mradi wa Bomba la Mafuta ghafi kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga na Serikali pamoja na wawekezaji katika mradi huu walishateua eneo la kujenga kiwanda cha kuunganisha na ku-coat mabomba katika Mji Mdogo wa Isaka. Je, ni hatua gani imefikiwa katika ujenzi wa kiwanda hicho?

Supplementary Question 3

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, hili eneo la Sojo Kata ya Igusule ambako pameamliwa kujengwa kiwanda hiki liko jimboni kwangu na wananchi wametoa hekari 400 ili kupisha ujenzi wa kiwanda hichi muhimu. Na kwa kuwa majibu ya Mheshimiwa waziri wamesema mwezi wa tisa ambayo ni miezi minne tu kutoka sasa mkandarasi anakabidhiwa eneo.

Je, nilitaka kujua kwamba Serikali inaweza kutoa commitment kwamba ndani ya kipindi hichi cha miezi minne kabla mkandarasi hajapewa hilo eneo wananchi wote waliotoa hekari 400 watakuwa wamelipwa fidia zao?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI (K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza na yeye pia nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia mradi huu mkubwa wa ujenzi wa bomba hili la mafuta na tija yake kwa wananchi wa maeneo yake hayo, kwa eneo ambalo limechaguliwa kujenga kiwanda cha kuunganisha mabomba.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimdhibitishie Mheshimiwa Mbunge moja ya kazi muhimu ambayo imefanyika ni kutambua mkuza ambako bomba litapita na tunatambua bomba hili ambalo litakuwa na urefu wa kilometa 1445 na zaidi ya kilometa hizo 1147 ziko upande wa Tanzania, Serikali yetu kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi na TPDC imetambua ule mkuza na imeshafanya tathimini ya mali mbalimbali ambazo ziko katika huo mkuza ikiwemo eneo hilo la ujenzi wa kiwanda hichi cha courtyard.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimthibitishie tathmini imekamilika na kwa kuwa tupo katika hatua nzuri ya mazungumzo ya Host Government Agreement baada ya hapo tutaenda Share Holders Agreement na kasha kufanya maamuzi ya investment decision na hatua zote hizi zipo katika mchakato wa miezi hii ambayo imesalia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimthibitishie tu Mheshimiwa Mbunge na kwa utashi wa viongozi wetu Marais wan chi mbili hizi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museven wa Uganda kwamba mwezi wa tisa utakapoanza mradi huu wananchi wote watakaopisha mkuza huu wa bomba watakuwa wamefidiwa kwa sababu tathmini ile imekamilika na sasa yapo tu mapitio ya mwisho ambayo yanafanywa baina ya Wizara ya Nishatu wataalamu, TPDC, Wizara ya Ardhi, Maendeleo Nyumba na Makazi na taasisi nyingine za Kiserikali. Nikushukuru sana.