Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA (K.n.y. MHE. LIVINGSTON J. LUSINDE) aliuliza:- Kwa kuwa Serikali imehamia Dodoma, je, kwa nini Serikali isijenge Maktaba yenye kumbukumbu za kazi za Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo pia itakuwa sehemu ya utalii kwa watu wa ndani na nje ya Mkoa wa Dodoma?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa majibu mazuri ambayo tumeyapata. Pamoja na majibu hayo, nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, tunaipongeza Serikali kwa uamuzi wa kujenga Kituo Kikuu cha Kumbukumbu Wilayani Kongwa kwa sababu Kongwa ina historia ya wapigania uhuru. Je, kituo hicho kitaanza kujengwa lini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa ushirikishwaji wa wadau huharakisha shughuli za maendeleo na nimeona katika Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wadau wameshirikishwa, Wachina wamejenga majengo mazuri na makubwa pale chuo kikuu Dar es Salaam. Je, Serikali ina mpango wowote wa kushirikisha wadau ili jengo hilo likamike katika uongozi wa Awamu ya Tano?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Felister Bura kwa niaba ya Mheshimiwa Livingstone Lusinde kwa maswali yake mazuri ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilianza na kwanza ameanza kwa kutoa pongezi kwa Wizara, tumepokea pongezi hizo. Vile vile swali lake la msingi la kwanza ametaka kujua, je, ni lini kituo hicho kitaanza kujengwa rasmi. Tayari ujenzi wa hiyo kituo ulishaanza na tulishaanza tangu mwaka 2015 ambapo ukarabati wa hicho kituo ulianza. Hata hivyo, kwa sababu ni suala la kibajeti na kwenye bajeti yetu ya mwaka jana kuna fedha ambayo ilitengwa kwa ajili ya kwenda kukarabati kituo hicho. Kwa hiyo, naomba nichukue nafasi hii kuweza kumhakikishia Mheshimiwa Bura kwamba ukarabati wa hicho kituo na kuweka miundombinu mingine unaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni kwa sababu lengo la Wizara ni kuhakikisha kwamba hicho kituo kinakuwa pia center kwa ajili ya masuala mazima ya utalii. Kwa hiyo mipango ambayo ipo pale ni mikubwa mpango mmojawapo ni kuhakikisha kwamba tunajenga kituo cha ndege lakini vilevile tuweze kujenga hotel za five stars pale ili kiweze kuwa kituo kikubwa cha masuala ya utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake pili ametaka kujua kwamba kuhusiana na kuweza kushirikisha wadau. Kama ambayo nimejibu kwenye jibu langu la msingi ni kwamba sisi kama Wizara suala hili hatufanyi peke yetu tumekuwa tukishirikiana na wadau. Kwa hiyo, nitumie fursa hii kuweza kuwahamsisha wadau mbalimbali waweze kushiriki katika kuhakikisha kwamba tunatunza hizi kumbukumbu za Mwalimu Nyerere. Ahsante.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA (K.n.y. MHE. LIVINGSTON J. LUSINDE) aliuliza:- Kwa kuwa Serikali imehamia Dodoma, je, kwa nini Serikali isijenge Maktaba yenye kumbukumbu za kazi za Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo pia itakuwa sehemu ya utalii kwa watu wa ndani na nje ya Mkoa wa Dodoma?

Supplementary Question 2

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la dogo nyongeza. Kwa kuwa Serikali imetamka Vituo vya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na kadhalika, lakini Mkoa wa Tabora una historia kubwa, nilitegemea kwamba leo Mheshimiwa Waziri atatamka kwamba Tabora nayo iwemo katika orodha ya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa. Nasema hivi kwa sababu uhuru na maelekezo mengine yote ya Baba wa Taifa yalitoka Mkoa wa Tabora, karata tatu zimetoka Mkoa wa Tabora. Baba Taifa ameacha historia kubwa katika Mkoa wa Tabora kwa kusoma na kadhalika.

Kwa hiyo, kwa kutokuweka orodha ya Kituo cha Tabora kukitambua rasmi kwa kweli hawautendei haki Mkoa wa Tabora. Je, ni lini sasa Serikali itaingiza katika orodha ya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa kwenye vituo hivyo ambacho vimetamkwa hivi leo?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Mwanne Nchemba, mama yangu kwa maswali ya nyongeza. Napenda nitumie fursa hii kumhakikishia kwamba kwa suala hili la uhifadhi wa Kumbukumbu za Mwalimu Nyerere kitu ambacho kama Wizara tunafanya, kwa sababu tulitaka tufanye katika mapana makubwa, tunayo sasa hivi Programu yetu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika.

Kwa hiyo, kupitia hiyo pragram Mkoa wa Tabora ni mkoa mmojawapo kati ya mikoa 15 ambayo imeteuliwa na Wizara ili kuweza kuyabaini yale maeneo maalum ambayo yallitumika katika ukombozi wa Bara la Afrika. Kwa hiyo Mkoa wa Tabora upo, lakini ni katika ile Program kubwa ya Ukombozi wa Bara la Afrika. Ahsante.