Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE (K.n.y. MHE. SELEMANI S. BUNGARA) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Kilwa haina Jokofu la kuhifadhi maiti na pia majengo yake mengi ni chakavu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kununua jokofu jipya sambamba na kukarabati majengo ya hospitali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti,swali la kwanza, jokofu hilo la Hospitali ya Kinyonga halifanyi kazkwa sasa na Hospitali hii ya Kinyonga ipo sambamba kuelekea Mikoa ya Kusini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga jengo hilo kwa haraka sambamba na kuleta jokofu lenye uwezo la kuhifadhi zaidi ya mwili mmoja ili kuendana na chochote kinachoweza kutokea ili kukidhi haja hiyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali inampango gani kukarabati Kituo cha Afya Njinjo ambacho hali yake kwa sasa ni mbaya sana? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Ngombale Vedasto,kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge, leo asubuhi kabla sijaingia hapa Bungeni nimefanya utaratibu wa kuwasiliana na Halmashauri na nina taarifa njema, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge leo tarehe 2 Mei, halmashauri inaingia mkataba na mdau wa Pan Africaambao wamekubali kujenga jengo la kisasa kwa ajili ya chumba cha kuhifadhia maiti, lakini kwa makubaliano kwamba na halmashauri nao watatununua jokofu la kisasa ili liweze kumudu hali ya uhitaji wa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili anaomba ukarabati waKituo cha Afya cha Njinjo, naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge azma ya Serikali ni kuhakikisha kwamba tunafanya ukarabati katika vituo vyote vya afya vile vile vilivyojengwa zamani, ili viwe na mwonekano wa sasa. Naye atakiri kwamba, katika nafasi aliyopata kutembelea vituo vya afya ambavyo tunavijenga sasa hivi tumevijenga vizuri, hali kadhalika hata hospitali za wilaya za zamani tungependa zikarabatiwe ziwe na muonekano wa kisasa kama kwa Hospitali ya Kilwa ya mwaka 1965, kwa vyovyote vile hata hali yake hailingani na hadhi ya hospitali ya Wilaya.

Name

Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE (K.n.y. MHE. SELEMANI S. BUNGARA) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Kilwa haina Jokofu la kuhifadhi maiti na pia majengo yake mengi ni chakavu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kununua jokofu jipya sambamba na kukarabati majengo ya hospitali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Hospitali ya rufaa ya Temeke haina mashine ya kufulia nguo, hadi kupelekea mashuka ya wagonjwa kupelekwa katika Hospitali ya Muhimbili ili kuweza kufuliwa. Je, Serikali itapeleka lini mashine ya kufulia nguo katika Hospitali ya Rufaa ya Temeke?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kuhusiana na Hospitali ya Rufaa ya Temeke kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninavyojua Hospitali yetu ya Rufaa ya Temeke inamashine ya kufulia, inawezekana katika kipindi hiki cha karibuni imeharibika na niombe tu baada ya kikao hiki cha Bunge nitafuatilia. Vile vile tumekuwa na utaratibu mbadala katika Hospitali yetu ya Rufaa ya Muhimbili ina mashine kubwa za kuweza kufulia na mara nyingi katika Hospitali za Rufaa za Mikoa katika Mkoa wa Dar es Salaam wanapopata tatizo basi huwa tunatumia Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili kama mbadala. Hata hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, baada ya kikao nitafuatilia kuhakikisha mashine hiyo inafanya kazi.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE (K.n.y. MHE. SELEMANI S. BUNGARA) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Kilwa haina Jokofu la kuhifadhi maiti na pia majengo yake mengi ni chakavu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kununua jokofu jipya sambamba na kukarabati majengo ya hospitali hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza naishukuru Serikali kwa kutujengea Kituo cha Afya Hirbadawna kukarabati Kituo cha Afya cha Simbay, lakini ilituahidi kwamba itatusaidia kukamilisha Kituo cha Afya cha Bassotuna Endasak.Naomba jibu ili wananchi wa Hanang waweze kufurahi. Ahsante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Dkt. Nagu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nipokee pongezi, yeye mwenyewe anakiri kwamba imefanyika kazi nzuri ya ukarabati wa vituo vya afya viwili kwake na ahadi yetu ya kukamilisha ukarabati wa ujenzi wa vituo vya afya kila kata iko pale pale.

Naomba Mheshimiwa Mbunge awaambie wananchi wawe na subira, lakini ni vizuri na wao wakaanza kujitokeza kwa zile kazi ambazo wanaweza kuanza kufanya ambavyo wananchi wake wamekuwa na mwitikio mkubwa waendelee kufanya na nasisi tutaunga mkono, lakini azma ni kuhakikisha kwamba hivyo vituo viwili navyo vinafanyiwa ukarabati.

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE (K.n.y. MHE. SELEMANI S. BUNGARA) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Kilwa haina Jokofu la kuhifadhi maiti na pia majengo yake mengi ni chakavu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kununua jokofu jipya sambamba na kukarabati majengo ya hospitali hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Wananchi wa Bungu wanashida kubwa ya Kituo cha Afya na wenyewe walishaanza kujenga majengo. Je, Serikali ina mpango wa kuunga mkono Kata ile ya Bungu?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kibiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepata fursa ya kwenda Kibiti na tukaenda kutembelea mpaka Kituo cha Afya Mbwera, kituo cha afya ambacho kipo ndani kweli kweli unaenda delta kule, kama mtu anataka kuona jinsi ambavyo Serikali ya CCM inafanya kazi ni pamoja na kwenda maeneo kama delta, naomba nimhakikishie Mbunge na yeye mwenyewe ni shuhuda kazi nzuri ambayo inafanyika, hakika hata huko kituo cha afya ambacho hakijafanyiwa ukarabati kwa kadri fedha zitakazopatikana, tutaenda kukikarabati.