Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Jimbo la Mikumi lina uhaba mkubwa wa Vituo vya Afya na hata pale ambapo kuna Kituo, basi dawa na Wataalamu ni tatizo:- Je, Serikali imejipanga vipi kutatua tatizo hilo sugu la uhaba wa Vituo vya Afya na dawa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu hayo ya Serikali, kwenye Kituo cha Afya cha Ulaya nilishauliza hapa mara nyingi kwamba Serikali itatusaidiaje maana ni kituo cha muda mrefu na kimeshachakaa na Serikali iliahidi kwamba itatupatia fedha za kuweza kukarabati kituo hichi cha Ulaya. Je, ni lini sasa Serikali italeta pesa kwenye kituo hiki cha Ulaya ambacho kimechakaa sana na ni kituo muhimu kinachituhudumia Kata za Ulaya, Muhenda, Zombo pamoja na Masanze?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Kituo cha Afya cha Malolo kinajengwa kwa nguvu za wananchi wakishirikiana na Mbunge na Halmashauri na sasa kimefikia kwenye kiwango cha lenta. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza nguvu za wananchi ambazo sasa hivi zimeonekana ili waweze kujipatia huduma katika Kituo cha Afya cha Malolo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Haule Joseph, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo katika swali lake la nyongeza anaongelea Kituo cha Afya cha Ulaya ambacho kimechakaa, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine wote, ni ukweli usiopingika kwamba vituo vya afya ambavyo vimepatiwa fedha kwa ajili ya ukarabati na ujenzi vinaonekana viko bora kuliko vile ambavyo vilikuwa vya siku nyingi. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba vile vituo vya afya ambavyo vilijengwa miaka hiyo na hadhi yake haiendani na vituo vya afya vya sasa, iko katika utaratibu wa kuhakikisha kwamba vinakarabatiwa ili vilingane na hadhi ya sasa. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge aendelee kuiamini Serikali kama ambavyo tumeweza kupeleka fedha katika hivyo vituo vya afya na zahanati yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, anaongelea jitihada ambazo zinafanywa na halmashauri pamoja na nguvu yake mwenyewe nampongeza kwa sababu suala la afya linahusu jamii yote ikiwa ni pamoja na Waheshimiwa Wabunge. Pale ambapo wananchi wamejitoa kwa ajili ya kujenga vituo vya afya Serikali na sisi tunaunga mkono kwa sababu ndio azma ya Serikali nayo iko kwenye ilani yetu ya CCM.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Jimbo la Mikumi lina uhaba mkubwa wa Vituo vya Afya na hata pale ambapo kuna Kituo, basi dawa na Wataalamu ni tatizo:- Je, Serikali imejipanga vipi kutatua tatizo hilo sugu la uhaba wa Vituo vya Afya na dawa?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kata ya Mnyagala ni kata ambayo ina idadi ya watu wengi na vijiji kadhaa ambavyo hakuna huduma ya kituo cha afya. Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha afya katika eneo hilo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Moshi Sulemani Kakoso, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge wengi wana hamu vituo vya vingi vijengwe na nimepata fursa ya kwenda jimboni kwa Mheshimiwa Kakoso tukaenda mpaka Mwese kule kuna kazi nzuri sana inafanyika ya ujenzi wa kituo cha afya kama ambavyo kazi nzuri imefanyika Kituo cha Afya Mwese, naomba nimtoe wasiwasi kwamba hata hicho kituo ambacho ana-propose kwa kadri nafasi itakavyoruhusu hatua kwa hatua tutahakikisha tunawasogezea wananchi huduma ya kupata matibabu ya afya kwa jirani.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Jimbo la Mikumi lina uhaba mkubwa wa Vituo vya Afya na hata pale ambapo kuna Kituo, basi dawa na Wataalamu ni tatizo:- Je, Serikali imejipanga vipi kutatua tatizo hilo sugu la uhaba wa Vituo vya Afya na dawa?

Supplementary Question 3

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Jimbo la Ikungi Mashariki halina kabisa kituo cha afya. Je, ni lini sasa Serikali itajenga vituo vya afya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Matembe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo anaongelea Ikungi Mashariki wakati mwingine ataongelea Ikungi Magharibi, lakini niombe tu kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo tumekuwa tukitekeleza na tumefikisha hivyo vituo vya afya 352, safari tunayo na tutazingatia maeneo yenye uhitaji mkubwa na sasa kama na eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge analitaja kwamba lipo mbali na lina population kubwa, naomba nimhakikishie kwamba katika awamu inayokuja tutazingatia maombi yake.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Jimbo la Mikumi lina uhaba mkubwa wa Vituo vya Afya na hata pale ambapo kuna Kituo, basi dawa na Wataalamu ni tatizo:- Je, Serikali imejipanga vipi kutatua tatizo hilo sugu la uhaba wa Vituo vya Afya na dawa?

Supplementary Question 4

MHE. SUSAN A. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Sekta ya afya kwa ujumla wake ina tatizo kubwa sana la watumishi, takribani asilimia 48 hakuna watumishi na hii imeathiri zaidi kwa sababu ya zoezi zima la uhakiki wa vyetii feki, ambapo tuliambiwa baadhi ya vituo ya afya vilifungwa. Nataka kujua nini mkakati wa Serikali
pamoja na kwamba wanajenga vituo, wana mkakati gani wa kuhakikisha kwamba vituo hivi vya afya vyote vinapata wataalam ili lipunguze tatizo kubwa la akinamama na watoto ambao wanafariki?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lyimo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba mahali popote ambapo vituo vya afya vinajengwa vinakamilika, zahanati zinajengwa zinakamilika, hayabaki yakawa majengo ambayo tunayatazama, tutahakikisha kwamba vifaa vinapelekwa na wataalam wanapelekwa. Mheshimiwa Lyimo ni shahidi, siku tukiwa ndani ya Bunge hili Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana Mheshimiwa Mkuchika alisema kama yupo Mbunge yeyote ambaye eneo lake zahanati imefungwa au kituo cha afya hakina wataalam kabisa apeleke orodha, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba huduma zinatolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuhakikishie, kuna kipindi ambacho tulitangaza nafasi especially kwa ajili ya Madaktari tuliweza kufanya mopping, hakuna Daktari hata mmoja ambaye alikuwa ame-qualify akabaki bila kuajiriwa. Ikafikia mahali ambapo Madaktari wote wameajiriwa na wengine hawajaripoti. Kwa hiyo pia tuna tatizo juu ya wataalam wenyewe kuwepo maana na demand nayo ni kubwa si kwa Tanzania peke yake, wengine wanaenda kutafuta green pastures outside this country.