Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. MOSHI S. KAKOSO) aliuliza:- Vijijini vya Kapanga, Katuma, Simbwesa, Kasekese, Kungwi na Kabage havina mawasiliano ya simu:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano ya simu?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri yanaridhisha lakini ahakikishe kweli, maana yake vijiji hivi vimekaa porini sana, havina mawasiliano, tena kwenye mbuga za wanyama mtu akijeruhiwa inakuwa taabu hata mawasiliano ya gari kuja kuwachukua.

Mheshimiwa Spika, swali la pili la nyongeza; katika Kijiji cha Kizi ambapo kuna mkongo wa mawasiliano umejengwa na Serikali lakini kijiji hakina mawasiliano, je, Mheshimiwa Waziri, nimemfuata ofisini kwake zaidi ya mara kumi kuhusu Kijiji cha Kizi, vipi anaoneje hilo swali langu?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Keissy kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ametaka nimhakikishie kwamba eneo hilo ambalo limetajwa nitafikisha mawasiliano. Kama nilivyomhakikishia ni kwamba vifaa viko bandarini, sasa hivi tulikuwa tunafanya clearance kwa ajili ya kuvipeleka sehemu husika. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutapeleka hayo mawasiliano kabla ya mwisho wa mwezi wa Sita kama nilivyoahidi.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu Kijiji cha Kizi; tayari nimekwishatembelea kijiji hicho na tulikuwa na Mheshimiwa Mbunge. Kwanza nimpongeze kwa jinsi anavyofuatilia masuala ya mawasiliano, katika majimbo mengi sana hapa nchini, jimbo lake lina asilimia 93 ya kupatikana kwa mawasiliano, nimhakikishie tu kwamba hicho kijiji chake kilichobakia tutakwenda tutashughulikia na tutakiingiza kwenye Mpango wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. MOSHI S. KAKOSO) aliuliza:- Vijijini vya Kapanga, Katuma, Simbwesa, Kasekese, Kungwi na Kabage havina mawasiliano ya simu:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano ya simu?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu yake mazuri, yeye mwenyewe anajua kwamba minara ya Waheshimiwa Wabunge wengi haifanyi kazi ikiwemo mnara wa kwangu Kilolo na ameahidi mara nyingi kufika kuhakikisha kwamba minara inafanya kazi. Sasa je, atakuwa tayari kwenda kabla ya Bunge hili, kufika Kilolo na kuhakikisha kwamba mnara ule unafanya kazi?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Venance Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, niwe mkweli, Mheshimiwa Mwamoto amekuwa akifika mara nyingi sana ofisini kufuatilia masuala ya minara kwenye jimbo lake. Ni kweli pia kuna minara kama mitatu, minne hivi ambayo haipeleki mawasiliano vizuri sehemu kubwa, nadhani ni kwa sababu ya watumiaji wengi sana, kwa hiyo, inakuwa na uhafifu. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutapeleka timu ya wataalam waende wakaiongezee nguvu minara kwenye maeneo yake ili iweze kuwahudumia wananchi kwa ukaribu zaidi.