Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Je, ni lini Kituo cha Misugusugu “Check Point” kitahamishwa, kwani kimekuwa kero kutokana na vumbi linalosababishwa na miundombinu mibovu?

Supplementary Question 1

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Swali la kwanza, ni kwa nini Serikali haikufikiri kabla haijaanzisha mradi huo wa maroli kupaki pale Misugusugu mpaka ikafikia wananchi wa Misugusugu wanapata TB?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, nini mkakati wa Serikali wa dharura kwa ajili ya kuokoa maisha ya wana Misugusugu?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Deo Muro, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza kwa nini Serikali haikufikiri kabla, Serikali siku zote inafikiri, ilifikiri enzi hizo na sasa inaendelea kufikiri ili kuendelea kuboresha maisha ya wananchi wetu hasa hawa wa Misugusugu na ndio maana Wizara ya Ujenzi imeanza kuiboresha barabara ile ili kuondokana na changamoto hii ya vumbi pamoja na kwamba Serikali inatekeleza mradi huu wa Euro milioni 23 kuhakikisha sasa eneo lile la Misugusugu kituo kile kinaondoka na kinahamia vigwaza. Kuonesha kwamba Serikali inaendelea kufikiri na kutenda kwa ajili ya wananchi wake, haya tunayoyatenda Vigwaza yanakwenda kutendwa Manyoni na pia tunakwenda kutekeleza mradi wa aina hii kule Nyakanazi ili kuhakikisha huduma hizi zinafanyika kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, ni mkakati wa dharura, ndio huu ambao nimeeleza kwamba Serikali inaboresha barabara il, lakini tunahakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati. Nitoe wito kwa Watanzania wote kwa ujumla maana ya kuwa na vituo hivi ni kuhakikisha mizigo ile yenye uhatarishi wa upotevu wa mapato tunaendelea kui-control hatua kwa hatua. Hata hivyo, pia wito wangu kwa Watanzania ni kuhakikisha kwamba wao wanakuwa wazalendo zaidi kwa Taifa lao ili mizigo hii ambayo wana- declare kwamba inaenda nchi jirani isiendelee kushushwa ndani ya Taifa letu. Unapoona gari linashusha mzigo ndani ya kijiji chako jiulize mara mbili kwa nini halikushusha mjini na lazima Watanzania wafahamu kwamba hakuna maendeleo bila kodi itakayolipwa na sisi Watanzania wenyewe na Serikali ya Awamu ya Tano imeonesha mfano na tunatenda kwa vitendo kwamba kodi ya Watanzania sasa inapelekwa kwenye miradi inayowafikia wananchi moja kwa moja.