Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y. MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO) aliuliza:- Idadi ya watu nchini inazidi kuongezeka sambamba na ongezeko la mahitaji ya ardhi kwa ajili ya kilimo na ufugaji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea uwezo wakulima na wafugaji ili kuendeleza shughuli zao kwa tija na kuwaondolea adha wanazozipata?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri kutoka kwa Naibu Waziri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Serikali imekiri kwamba itatoa mafunzo kwa wafugaji na Maafisa Ugani katika Halmashauri zetu, je, ni lini itatoa mafunzo hayo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ambayo wafugaji wanaongezeka kwa kasi kubwa sana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imetenga maeneo kwa maana ya vitalu vya wafugaji mbalimbali vinavyofikia 100; na kwa kuwa wakulima wengi wameshapewa maeneo hayo lakini mpaka sasa hawajaenda. Nini kauli ya Serikali kuhusu hawa wafugaji ambao wameshindwa kwenda kwenye maeneo yale ya wafugaji na kuendeleza migogoro na wakulima mbalimbali kwa mifugo yao kula mazao ya wakulima? Ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mpakate, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ni lini tutakwenda kupeleka mafunzo haya Wilayani Tunduru? Naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba timu yetu iliyoko Kaliua ikitoka huko itakwenda Tunduru na Halmashauri zingine katika nchi yetu kwa ajili ya kutoa elimu hii kwa wafugaji na Maafisa Ugani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili analotaka kujua ni namna gani na tunatoa kauli gani kwa wale waliopata vitalu. Kwanza nataka niwapongeze sana viongozi wote wa kule Wilayani Tunduru kwa kazi kubwa waliyoifanya ya mfano ya kuandaa vitalu wao wenyewe Halmashauri na kuvigawa kwa wafugaji kwa ajili ya kufanya kazi ya ufugaji iliyo na tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kauli ya Serikali ni kama ifuatvyo: Wafugaji wote waliopewa vitalu hivi na wakaacha kuvitumia kwa wakati, tunawapa tahadhari kwamba watanyang’anywa na watapewa wafugaji wengine walio tayari kufanya kazi hii kwa ufanisi.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y. MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO) aliuliza:- Idadi ya watu nchini inazidi kuongezeka sambamba na ongezeko la mahitaji ya ardhi kwa ajili ya kilimo na ufugaji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea uwezo wakulima na wafugaji ili kuendeleza shughuli zao kwa tija na kuwaondolea adha wanazozipata?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Awamu ya Kwanza Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Baba wa Taifa alisambaza mitamba bora katika maeneo yote ambayo yanafanya zero grazing. Kwa kuwa ni muda mrefu sasa na cross breeding imeshafifisha mazao yale ni lini sasa Serikali itaweza kuboresha na kutawanya mitamba bora, vifaranga bora vya kienyeji na vifaranga bora vya samaki katika maeneo ya wafugaji kama Kilimanjaro ambapo kuna wanawake wengi sana ambao ni wafugaji?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shally Raymond, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza swali ni zuri sana juu ya Serikali kuhakikisha kwamba tunasambaza mitamba bora kwa wafugaji hasa akina mama wa Mkoa wa Kilimanjaro na Taifa zima. Progamu hii Serikali tunayo kupitia mashamba yetu ya mifugo yaliyosamba nchi nzima tunafanya kazi hii. Kwa mfano tu ni kwamba hivi karibuni kupitia dirisha letu la sekta binafsi tumewawezesha Ushirika wa Wafugaji wa Ng’ombe wa Maziwa Mkoani Tanga yaani TBCU, wamekopeshwa pesa na Benki yetu ya Kilimo ili waweze kununua mitamba bora 300 ambapo kufikia tarehe 30 ya mwezi huu mitamba ile itaenda kusambazwa kwa wafugaji wote wa Mkoa wa Tanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, tuko tayari kuhakikisha kwamba na wafugaji wengine kote nchini wanapata fursa hii. Shime wafugaji wote wa ng’ombe wa maziwa, kuku hata wale wa samaki wajiunge katika vikundi ili waweze kutumia fursa hii inayopatikana kupitia dirisha letu la ukopeshaji la Benki ya Kilimo.