Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susanne Peter Maselle

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN P. MASSELE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo Kikuu cha Umma au Vyuo Vikuu vya Umma vyenye hadhi ya juu katika Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 1

MHE. SUSAN P. MASSELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu ya Serikali, ya Waziri, ambayo yanavunja moyo kabisa, kwa sababu hawajatoa commitment ni ni lini watamaliza huo ukarabati na ukizingatia Vyuo hivyo alivyovitaja viko kwenye hali mbaya sana na ukizingatia pia Jiji la Mwanza, ni Jiji ambalo linakua kila siku. Vyuo vingine viko uchochoroni kabisa ambapo ni mazingira mabaya kwa wanafunzi na Wakufunzi katika kufanya kazi. Sasa katika majibu haya nina maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, mwaka jana tuliona Serikali kupitia Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) ikivichukulia hatua Vyuo Vikuu binafsi ambavyo havikuwa na vigezo vya Vyuo Vikuu na kuviacha Vyuo Vikuu vya Umma ambavyo vilevile vilikuwa havina vigezo vya kuwa Vyuo Vikuu kama alivyojibu kwenye swali la msingi. Je, Waziri haoni kwamba zoezi hili lilikuwa linagandamiza Vyuo Vikuu vya binafsi ambavyo vinatoa nafasi kubwa kwa wanafunzi ambao wamekosa nafasi kwenye Vyuo vya Umma na kupata nafasi?

MWENYEKITI: Sema tu straight.

MHE. SUSAN P. MASSELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Serikali ina ndoto ya Tanzania ya Viwanda ni lini sasa itajenga, Polytechnic College katika Mkoa wa Mwanza, ambapo itatoa ujuzi kwa ajili ya mahitaji ya viwanda ukiachilia mbali Chuo cha...

MWENYEKITI: Ahsante, inatosha. Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kwa niaba.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA K.n.y. WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Susanne Maselle, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, si kweli kwamba zoezi hili lililofanyika lilikuwa la ugandamizi na ndiyo maana vyuo ambavyo vilionekana vina matatizo havijalalamika, vimetii masharti, vimeboresha vyuo vyao na wale ambao wamekamilisha wamekabidhiwa kuendelea kufanya kazi. Kwa hiyo, hii siyo kweli lakini na vyuo vya umma pia vinazingatia utaratibu na ubora wa elimu kwa kadri ya miongozo iliyotolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, tumesema nia ya Serikali si kuanzisha vyuo kila mkoa bali ni kuhakikisha vyuo vilivyopo vinaendelea kuboreshwa kwa kuongeza miundombinu na wataalam waliobebea katika nyanja hizo. Vikiimarishwa vinatosha kutoa wataalam kwenye viwanda na kubaki na kutumia utaalam wao nje ya nchi yetu.