Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Mkoa wa Manyara, hususani Wilaya ya Mbulu, umewahi kutoa wanariadha mahiri ambao walililetea Taifa heshima kubwa, lakini cha kushangaza wanariadha hao wametelekezwa:- (a) Je, ni lini Serikali sasa itaandaa utaratibu wa kuwaenzi wanariadha hao? (b) Je, ni lini sasa Serikali itajenga uwanja kwa ajili ya riadha katika Mkoa wa Manyara ili kuwahamasisha wanariadha wapya?

Supplementary Question 1

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Asilimia 90 ya wanariadha wanatokea Mkoa wa Manyara, lakini pia wapo wengi na taarifa iliyosomwa hapo na Naibu Waziri ni kuanzia miaka ya tisini kurudi nyuma, wapo wengi, akina John Yuda Msuri, Fabian Joseph, Andrew Sambu Sipe; wote hawa rekodi zao hazijavunjwa mpaka sasa kwa kuwa walikuwa wameshiriki mbio mbalimbali za kimataifa. Swali langu la msingi lilisema; ni lini utaratibu wa kuwaenzi wanariadha hawa utafanyiwa kazi sasa? Muda mfupi uliopita tulizungumza habari hapa na Waziri wa TAMISEMI alijibu suala la Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanaofanya vizuri kuwa recognized na kupewa vyeti, habari gani kwa ajili ya wanariadha hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, amejibu hapa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba picha zao zitawekwa kwenye jumba la makumbusho, je, hiyo inatosha? Wapo wanariadha wengi ambao hali zao za kimaisha ni duni, naomba kujua wanafanyiwa lini mchakato wa kutambuliwa juhudi zao. Ahsante.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie nafasi hii kuweza kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekuwa ni mfuatiliaji mzuri sana wa masuala ya michezo. Nikianza na swali lake la kwanza, ni kweli kwamba sisi kama Wizara tunatambua kwamba wapo wanariadha wengi sana ambao wanatoka kwenye Mkoa wa Manyara kama ambavyo yeye mwenyewe amewataja, lakini sisi kama Serikali hatuwezi kuangalia tu mkoa mmoja, ni wanariadha wengi ambao wanatoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Kama ambavyo nimejibu kwenye jibu langu la msingi kwamba sisi kama Serikali tunao mpango wa kuanzisha makumbusho rasmi kwa ajili ya kuweka kumbukumbu zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unavyojua sasa hivi sisi kama Wizara tunayo ile kampeni yetu ya uzalendo ambayo kila mwaka tumekuwa tukiifanya na kitu ambacho tunafanya ni kuweza kuwaenzi watu mbalimbali ambao wameliletea heshima kubwa Taifa hili. Mwaka jana nakumbuka tulianza kwa wanamuziki lakini mwaka huu tutajipanga kuangalia namna gani ambavyo tunaweza tukawaenzi wanariadha wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Mkoa wa Manyara, hususani Wilaya ya Mbulu, umewahi kutoa wanariadha mahiri ambao walililetea Taifa heshima kubwa, lakini cha kushangaza wanariadha hao wametelekezwa:- (a) Je, ni lini Serikali sasa itaandaa utaratibu wa kuwaenzi wanariadha hao? (b) Je, ni lini sasa Serikali itajenga uwanja kwa ajili ya riadha katika Mkoa wa Manyara ili kuwahamasisha wanariadha wapya?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii nami niulize swali la wanariadha ambao nao Mkoa wa Singida ni miongoni mwa mikoa ambayo ilikuwa inafanya vizuri sana katika riadha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jimbo ninalotoka mimi kulikuwa na wanariadha miaka ya nyuma, lakini hata mimi mwenyewe nilikuwa mwanariadha. Kwa kuwa ili wanariadha na vijana ambao wapo shuleni waweze kupata hamasa ya michezo ni pamoja na vyombo vya habari ikiwemo TBC kusikika katika maeneo mbalimbali. Je, ni lini sasa Serikali itafanya TBC isikike katika eneo la Itigi ambapo haisikiki kabisa?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie fursa hii kuweza kumpongeza Mheshimiwa Massare kwa sababu swali lake la usikivu wa TBC amekuwa akiuliza karibu kila Bunge, lakini niseme kwamba ni suala la kibajeti na kwa kuwa hili ni Bunge la Bajeti kwa mwaka huu tutaangalia namna gani ambavyo tutaboresha usikivu katika eneo lake la Itigi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Anna Joram Gidarya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Mkoa wa Manyara, hususani Wilaya ya Mbulu, umewahi kutoa wanariadha mahiri ambao walililetea Taifa heshima kubwa, lakini cha kushangaza wanariadha hao wametelekezwa:- (a) Je, ni lini Serikali sasa itaandaa utaratibu wa kuwaenzi wanariadha hao? (b) Je, ni lini sasa Serikali itajenga uwanja kwa ajili ya riadha katika Mkoa wa Manyara ili kuwahamasisha wanariadha wapya?

Supplementary Question 3

MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Natambua juhudi kubwa anayofanya Naibu Waziri. Michezo ni sekta muhimu, lakini pamoja na hivyo, vyuo vyetu vikuu havina vipaumbele vya miundombinu ya viwanja. Mfano mzuri ni mwaka jana, tulikuwa na mashindano ya vyuo vikuu vya Afrika Mashariki, tulikuwa na michezo...

MWENYEKITI: Uliza swali tu Mheshimiwa.

MHE. ANNA J. GIDARYA: …kulikuwa na michezo kumi na tisa, Tanzania tulishiriki michezo tisa tu jambo ambalo
limesababisha nchi yetu kukosa vikombe vingi. Je, ni lini sasa Serikali itaboresha miundombinu na kuipa michezo kipaumbele katika vyuo vyetu?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kuweza kumpongeza Mheshimiwa Anna kwa sababu kwanza ni mwanamichezo mahiri, lakini vilevile ni Kiongozi wa CHANETA Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali lake la msingi, ametaka kujua kwamba ni lini sasa Serikali itaweza kuboresha viwanja vya michezo, hususan kwenye vyuo vikuu. Nikiri kwamba ni kweli mwaka jana tulikuwa tuna mashindano na yeye mwenyewe pia alishiriki, pamoja na kwamba tuna uhaba wa viwanja vya michezo, lakini kama ambavyo tumekuwa tukisema kwamba Sera yetu ya Maendeleo ya Michezo ya mwaka 1995 inasisitiza kwamba suala la michezo sio suala la Serikali peke yake, ni suala la Serikali lakini vilevile tuweze kushirikiana pamoja na wadau.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kuweza kuwaambia na kuwaomba Wabunge wote kuiga mfano wa Mheshimiwa Waziri Mkuu wetu kwa namna ambavyo amefanya maboresho ya kiwanja kule Lindi. Kwa hiyo suala hili la michezo sio suala la kuiachia Serikali peke yake, tuendelee kushirikiana pamoja na Serikali na sisi kama Wizara tuko tayari kuendelea kutoa utaalam pamoja na mafunzo mbalimbali namna gani ya kuweza kuboresha hivyo viwanja.